Karakana ya Luban yasaidia vijana wa Afrika kutimiza ndoto zao

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
W020231120546249018440.jpg

Miaka 600 iliyopita, baharia wa China Zheng He aliongoza kikosi cha majahazi kusafiri hadi kwenye pwani ya mashariki ya Afrika mara nne, na kwamba Njia ya Hariri Baharini ilishuhudia historia ndefu ya mawasiliano kati ya China na Afrika.

Miaka 600 baadaye, karakana za Luban zilipewa jina la fundi maarufu wa kale wa China zikikita mizizi barani Afrika, na kufanya bara la Afrika linalojaa matumaini na fursa za maendeleo kuwa changamfu zaidi katika mchakato wa China na Afrika kujenga kwa pamoja "Ukanda Mmoja, Njia Moja". Hivi majuzi, karakana mbili zaidi za Luban zimezinduliwa rasmi nchini Tanzania na Rwanda.

Lu Ban ni fundi maarufu wa kale wa China na anajulikana kama "babu wa ufundi wote". Mwaka 2018, Rais Xi Jinping wa China alipendekeza katika Mkutano wa Kilele wa Beijing wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika kuanzisha karakana 10 za Luban barani Afrika ili kutoa mafunzo ya ujuzi kwa vijana wa Afrika.

Mwaka uliofuata, karakana ya kwanza ya Luban barani Afrika ilifunguliwa rasmi nchini Djibouti. Aisha, kijana mwenye umri wa miaka 22, ni mmoja wa wanafunzi wa kwanza wa karakana hii ya Luban nchini Djibouti.

Baada ya miaka mitatu ya masomo, yuko tayari kuwa mfanyakazi wa kiufundi kwenye Reli ya Addis Ababa na Djibouti, inayosifiwa kama "Reli ya TAZARA katika Enzi mpya" iliyojengwa na kampuni ya China. Akikumbusha miaka mitatu ya uzoefu wa masomo katika karakana ya ufundi ya Luban, Aisha alisema kwamba hapa ni pahali palipompelekea kuwa karibu zaidi na ndoto yake.

W020231120546253815884.jpg

Hivi sasa, China imejenga zaidi ya karakana kumi za Luban barani Afrika, "vituo hivi vya teknolojia" ambavyo ni "vidogo lakini vizuri, vinavyotoa matokeo haraka, na vinaboresha maisha ya watu" vimetoa mafunzo kwa maelfu ya wanafunzi barani Afrika, sio tu katika sekta za jadi kama vile kilimo na uhandisi, bali pia inahusisha nyanja mpya kama vile uchumi wa kidijitali, akili bandia, na magari ya umeme.

Kupitia Karakana ya Luban, China imeleta elimu ya juu ya ufundi stadi na bidhaa, teknolojia na vifaa vya hali ya juu barani Afrika. Rais Ismael Guelleh wa Djibouti aliwahi kusifu kwamba "Karakana ya Luban ni zawadi bora zaidi inayotoa China kwa Afrika."

Kinachostahiki kutajwa ni kwamba Karakana ya Luban sio tu imeimarisha ushirikiano wa teknolojia na vipaji kati ya China na Afrika, bali pia kuongeza urafiki wa kina kati ya watu wa China na Afrika.

Mwanzoni, Karakana ya Luban ilianzishwa na mji wa Tianjin, na baada ya kuinuliwa ngazi hadi kwenye taifa, serikali za mitaa za China zimeshiriki kikamilifu katika mradi huu, na kuwaunganisha watu wa China na Afrika katika ngazi ya mitaa.

Gazeti la Washington Post hivi majuzi liliwahoji walimu, wanafunzi na wahitimu wa Karakana ya ufundi ya Luban nchini Ethiopia na Afrika Kusini na kusema kwenye makala yake kuwa, "Hawajui waishukuru vipi China, Karakana ya Luban imeongeza chachu kati ya watu wa China na Afrika."

Mwaka huu ni kumbukumbu ya miaka 10 ya ujenzi wa pamoja wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja", na kutokana na pendekezo hilo, China na Afrika zimepata fursa ya kuunganisha sekta zao za kiviwanda.

Hivi sasa, ikiwa hatua muhimu ya kutekeleza pendekezo hilo, Karakana ya Luban imejikita kwa kina katika nyayo za China na Afrika katika kutafuta maendeleo kwa pamoja. Mbali na kusaidia vijana wa Afrika kutimiza ndoto zao, Karakana ya Luban imewezesha kijiti cha urafiki wa China na Afrika kuendelea kupokezwa kizazi kwa kizazi.
 
Back
Top Bottom