Mwisho wa Daudi Ballali

Mwisho wa Daudi Ballali

Watanzania wengi tunahitaji kuamka.. CCM ilipotufikisha imetosha...
Tutakuja kuulizwa na watoto wetu na wajukuu zetu..tulikuwa tunafanya nini..?
Mtu ameiba billions..na yeye Balali ni mhusika mkuu..akisaidiana na viongozi wakubwa sana ndani ya serikali..eti ameenda Marekani na kufia huko..na kuzikwa kimya kimya.. Hivi hii inaingia akilini..?

CCM walipotufikisha basi..deni la taifa kila siku linaongezeka.. sasa hivi tuna Escrow..

Na bado movies

CCM ni chaguo la Mungu.
 
Mwanzoni hata alipozikwa mlikuwa hamjui...sasa mwandishi na kampuni yake kafanya utafiti wake na bado mnamdharau.

Nani alikua akijua Balali alizikwa wapi?? tuache dharau
 
Kwa nnavyoijua bongo, hii habari very likely ina link na uchaguzi mkuu ujao. Stay tuned........

BTW toka lini Balali alianza kuitwa Ballali, just asking, au ndiyo yale yale ya Martin kuitwa Martine (Kuna kipindi kalizuka sana haka katabia). Fanyeni hata research hata kwa google to kuhusu jina Balali.

Kama vile Zitto, Sitta, Lissu &Co!
 
balali.jpg

Mkazi wa Kijiji la Luganga, Wilaya ya Mufindi, Iringa, alikozaliwa Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali analazimika kutumia saa 32 kufika katika kaburi la kiongozi huyo lililopo eneo la Silver Spring, Maryland nchini Marekani.

Ndugu wa Ballali wanaweza kutaka kwenda kuona kaburi la ndugu yao, kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawakuwahi kupata fursa ya kumzika Gavana huyo ambaye alikuwa kiongozi wa juu kabisa wa taasisi kubwa inayosimamia masuala ya fedha na uchumi wa nchi.

Mwandishi wa gazeti hili alisafiri kwa saa 24 kutoka Dar es Salaam hadi Washington, Marekani ambako alithibitisha pasi na shaka kwamba Ballali alizikwa Mei 21, 2008 katika makaburi ya Gate of Heaven, baada ya kufariki dunia akiwa nyumbani kwake Maryland, Mei 16, mwaka huo.

Safari hiyo ya siku kumi, ilianza Alhamisi Juni 26, 2014 hadi Jumapili, Julai 6. Mwandishi wa habari hizi aliligundua kaburi hilo baada ya kwenda makaburi ya Gate of Heaven kwa siku tatu mfululizo.

Siku ya kwanza, mwenyeji wa mwandishi ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sasa alimfikisha katika makaburi hayo, lakini kaburi la Ballali halikuonekana na hata mwandishi alipokwenda siku ya pili peke yake, kaburi hilo pia halikuonekana kwa kutokana na ukubwa wa eneo hilo.

Siku ya tatu, Mwandishi wa Mwananchi alilazimika kuomba msaada wa Ofisi ya Makaburi ya Gate of Heaven, ambayo ilimsadia kuonyesha eneo lilipo kaburi hilo, hivyo kuwezesha kupata picha zake.

Kaburi lake liko katika msitari wa mwisho kabisa na Ukanda wa Kijani wa miti iliyozunguka makaburi ya Gate of Heaven, likiwa limeandikwa jina la kiongozi huyo, pamoja na maneno ya Kiingereza yanayosomeka “When the heart weep for what it has lost, the soul rejoices for what it has found”.

Maana ya maneno hayo ni kwamba “wakati moyo ukiomboleza kwa kile kilichopotea, roho hufurahi kwa kile kilichopatikana”. Kaburi hili limezungukwa na makaburi mengine kadhaa ambayo si ya Watanzania, kwani kwa haraka kutokana na mazingira yalivyokuwa, Mwandishi wa Mwananchi hakuweza kuona kaburi jingine lenye majina yenye asili au kuwa na mwelekeo wa asili ya Tanzania.

Uthibitisho huu ni tofauti na hekaya za miaka nenda rudi zilizogubika kifo cha kiongozi huyo, ambaye tangu alipoondoka nchini kwenda Marekani Agosti 2007, hakuwahi kurejea na badala yake zilisikika taarifa za kuugua kwake, kifo chake na baadaye mazishi yake yaliyokuwa ya siri kubwa yakiwahusisha ndugu wa karibu pekee.

Kutokana na mazingira hayo, kumekuwapo na uvumi kwamba Ballali hakufa na pengine amefichwa kusikojulikana, madai yanayochagizwa na mtu aliyejitokeza katika mitandao wa kijamii ya Twitter na facebook, akidai kwamba yeye ni Ballali na kwamba hajafa, huku akisisitiza kuwa wakati ukiwadia ukweli utafahamika.

Mtu huyo asiyefahamika hadi sasa alianza kujitokeza Twitter, Oktoba Mosi, 2012 pale aliposema “Nitakutana na Rais Kikwete (Jakaya) na ujumbe wake wiki hii hapa Marekani”. Mtu huyo alidai kwamba alikuja nchini Tanzania na kukaa karibu na Hoteli ya Hyatt Kempinski Kilimanjaro na baadaye kuondoka ghafla kwa kile alichokiita sababu za kiusalama.

Novemba 13 mwaka huo alituma ujumbe akisema:“In Dar es Salaam, Hyatt Regency Dar es Salaam, The Kempinski Kilimanjaro Hotel. Feels good to be close to my former office, BoT,” akimaanisha kwamba niko Hoteli ya Hyatt Regency Dar es Salaam, najisikia vizuri kuwa karibu na ofisi yangu ya zamani BoT.

Mtu huyo ambaye sasa tunaweza kuthibitisha kuwa ni feki amekuwa akiendelea kutuma ujumbe akijitambulisha kwa jina hilo la Ballali.

Ballali alifariki dunia kama ilivyotagazwa, lakini ilikuwaje akaenda safarini Washington, ugonjwa wake na hata kifo chake kilikuwaje? Je ndugu zake wanasemaje, safari ya kwenda Marekani ilikuwaje? Fuatilia mfululizo wa habari hii itakapoendelea kesho.

Source: Mwananchi

Nina mashaka hiyo Picha ilipigwa marekani maana wamarekani wanatunza sana bustani zao hasa sehemu kama hizo za Makaburi. huwezi kuta viraka vya majani kwenye bustani zinazotunzwa.
 
hv nyie serkali kitendo mnachokifanya kwa watz Si kizuri,Mungu atakwenda waumbua mchana kweupe,mambo ya kifo sio ya kuchezea.na mambo ya mwenyezi mungu,dhoruba litakumba serikali kwa kufanya mambo yanayokiuka utu,
 
Chacha Wangwe aliuawa kwa sababu ya kutaka kuwasilisha hoja binafsi bungeni juu ya uwepo wa Daud Balalli kwani alikuwa na ushahidi lakini kwa kuondoa soo wahusika wakafanya juu chini na kumuondoa duniani na kuchukua document zote. na leo hii wamekuja na kihoja kingine cha kujenga kabuli na kupiga picha na huyu mwandishi alipelekwa na gharama kutoka kwa nani? na je kwa nini imekuwa hivi sasa na sio wakati wa mazishi yake? huu ni UPUUZI usiovumilika.
 
Uongo huu waambie watoto wako..technolojia gani inapiga mtu picha akiwa kaburini?acha mahekaya ya abunuwasi hayo

we Kigogo (sio lugha bali cha mti) jaribu kupitia forensic anthropology kuna subsurface radar ambapo baadae hutengenezwa 2D na 3D maps. Sema gharama (if at all it pays) na kupata kibali cha kufanya kazi hiyo (from the ethical point of view).
 
Ukitaka kujua huu ni uongo usio na shaka mi pale mwandishi anaposema eti alitumia siku mbili kutafuta bila mafanikio ila siku ya tatu ndo akakumbuka kwenda kwa mamlaka inayohusika wamsaidie..hivi kwa jinsi mwandishi alivodiscribe ukubwa wa ilo eneo sidhani kama mtu alieko katika mission kama hiyo tena kwa safari zaidi ya masaa 30 kutafuta ukweli eti angeanza kuangaika kutafuta ilo kaburi bila kushilikisha wausika.. nadhani mwadishi anajaribu kutengeneza na kuulemba uongo wake uwe mlefu na jua toleo lijalo litanunulika vya kutosh kwa sababu ya huu uongo.

Asante kwa mchango wako!

Kwa kuongezea, Hii issue imekomaliwa na gazeti la mwanachi mwandishi akiwa ni Nevile Meena pamoja na gazeti la Mtanzania.

Kituko! Gazeti la Mtanzania liliandika Balali alijulishwa kuwa angefariki baada ya mwezi mmoja; kesho yake gazeti la mwananchi likaripoti eti angefariki ndani ya wiki 2 tangu apatiwe vipimo!

Haya magazeti mawili watueleze walienda Marekani kwa ufadhili wa nani?
 
kaburi lenyewe mbona limekaa kisanii sana? Yaani lipo peke yake limejitenga kiukweli sijaelewa kabisa hii sinema haina mvuto.
 
Yaani mwandishi anasafiri kutoka hapa mpaka marekani anepiga picha inaonyesha kaburi mojatu ?
hapo hakuna makaburi mengine ? mbona hatuyaoni ?

kunasiku Balali atakufa kweli alafu mtatueleza
 
Back
Top Bottom