Mwisho kamili wa simu za Nokia

Mwisho kamili wa simu za Nokia

Joined
Jun 3, 2014
Posts
28
Reaction score
16
lumia.jpg


Kampuni ya Microsoft imeamua kusitisha matumizi ya jina la Nokia kwenye bidhaa zake. Kuanzia sasa simu kutoka microsoft zitakuwa zinaitwa Microsoft Lumia au Lumia tu badala ya kuanzia na jina la Nokia.

Kampuni ya Microsoft ilinunua kitengo cha simu za mikononi cha kampuni ya Nokia mwaka 2013 kwa dola za marekani bilioni 7.17. Kama sehemu ya dili hilo, Microsoft ilipewa haki ya kuendelea kutumia jina la Nokia kwenye simu zake. Kampuni ya Nokia kwa sasa inaendelea kufanya shughuli nyingine kasoro utengenezaji simu za mikononi kama vile utengenezaji ramani na utengenezaji vifaa vya mawasiliano na mitandao (telecommunications and networking equipments).

Hatua hii maana yake ni kuwa huu ndio mwisho kamili wa kuwa na simu zinazoitwa Nokia. Je utaweza kuzoea kusema Lumia tochi?

chanzo: bofyatz.com
 
kwani hawa microsoft waliinunua nokia kwa mkataba wa miaka mingapi!?
 
Bye bye nokia tochi,
Nw ni microsoft tochi.,,,
 
kwani hawa microsoft waliinunua nokia kwa mkataba wa miaka mingapi!?

Microsoft walinunua haki za kutumia jina la Nokia kwa miaka 10...deal yenyewe hata mwaka haijamaliza Microsoft kapiga u-turn...
 
Unaweza kummaliza mpinzani wako kwa kununua shughuli zake na ukazitelekeza hata kufuta uhai wake kabisa/ Ni mbinu muhimu kibiashara kimkakati inakubalika.

Relevance ya hii statement kwa mada husika ikoje Mkuu?
 
Nokia na shost wake blackberry wanachechemea ile mbaya ila meakani kama atarudi atatonhisha naona android wamewapoteza hawa
 
Nokia na shost wake blackberry wanachechemea ile mbaya ila meakani kama atarudi atatonhisha naona android wamewapoteza hawa

kaka hebu iangalie simu ilivyo changua kitu kimoja kimoja then tafuta kimegunduliwa na nani.

anza na 3g, 4g, 2g, bluetooth, wifi, display, technology za camera, nfc, nk
then utaona hawa kina iphone, huawei and co hawajaleta chochote duniani bali wanatumia vitu vya kina nokia, samsung, alcatel(wazamani), erricson na wengineo.

china ana protect makampuni yake na kuyaruhusu yaibe yanavyotaka, wengine wanamiliki ubongo wa watu (apple) kila wanachofanya kinafanikiwa japo si vyao.

hebu jiulize swali toka android na ios ziwe ndio main os umeona kitu gani kipya cha kushtua zaidi ya kuongeza specs kila mwaka?
 
kaka hebu iangalie simu ilivyo changua kitu kimoja kimoja then tafuta kimegunduliwa na nani.

anza na 3g, 4g, 2g, bluetooth, wifi, display, technology za camera, nfc, nk
then utaona hawa kina iphone, huawei and co hawajaleta chochote duniani bali wanatumia vitu vya kina nokia, samsung, alcatel(wazamani), erricson na wengineo.

china ana protect makampuni yake na kuyaruhusu yaibe yanavyotaka, wengine wanamiliki ubongo wa watu (apple) kila wanachofanya kinafanikiwa japo si vyao.

hebu jiulize swali toka android na ios ziwe ndio main os umeona kitu gani kipya cha kushtua zaidi ya kuongeza specs kila mwaka?

Ni kweli Chief yaani juzi jukwaa moja kulikuwa na ubishi kati ya iphone 6 na samsung s5 ipi imekuja na jipya...kwa kuangalia mjadala mimi niliona spec za iphone 6 zinazidiwa kiasi fulani hadi s4 ukiacha s5 sasa uliibuka mjadala juu ya ram na processor za simu hizi 2 sasa mimi sina maarifa sana na hayo mambo

hemu nipe darasa juu ya ilo swala maana wadau wanasema iphone ipo fasta sana kufunguka kuliko simu zote za android.....hemu nipige brush kidogo mkuu.
 
Relevance ya hii statement kwa mada husika ikoje Mkuu?

Kwamba microsoft wamenunua functions Fulani za Nokia ili wazitumie kwenye biashara zao, na kumfanya Nokia afanye shughuli zingine; kisha Microsoft wakaachana na matumizi ya manunuzi yao ilali Nokia hafanyi tena. Huoni ndio mwanzo wa mwisho wa Nokia?
 
wamba micosoft wamennua fctions Fulani zaNokia ili wazite kweny biashra zao nakumfanya Nokia afny shughulizngi kaha hiz alizoa; kishaMicrooft wanfut atumizi yamanunuzi yake ilali Noki hfanyi tena. Huoni ndiomwzo wa mwiso waNOia?

Ulikimbizwa... dah!
 
Relevance ya hii statement kwa mada husika ikoje Mkuu?

Microoft wamenunua shughuli za Nokia na kumfanya Nokia aachane na shughuli alizouza kwa jina lilelile. Microsoft wanabadili jina la bidhaa ambayo kuwapo kwake lilikuwa linamtangaza Nokia. Huoni anaondoa jina la nokia masikioni mwa watu na ndio kifo cha asiyesikika?
 
Unafikiri hawana mipango na mikakati katika maamuzi wanayotoa?
Microoft wamenunua shughuli za Nokia na kumfanya Nokia aachane na shughuli alizouza kwa jina lilelile. Microsoft wanabadili jina la bidhaa ambayo kuwapo kwake lilikuwa linamtangaza Nokia. Huoni anaondoa jina la nokia masikioni mwa watu na ndio kifo cha asiyesikika?
 
Back
Top Bottom