Mkuu wangu tatizo ni UBEPARI..Na nitakwambia kwa lugha nyepesi zaidi pasipo kufikiria sana it's just Logic.
Tanzania ni taifa changa kama mtoto anayeanza maisha tofauti na Marekani au nchi zilizokwisha endelea. Wao wana kila sababu ya kuwa Mabepari kwa sababu tayari wameshakua kiumri kuvaa suti, wana mtaji na wamepitia maisha ya utoto na ujana as a nation kufika kuchukua Ubepari kama ndio mfumo wa maisha yao. KIla hatua ya Ubepari inalenga umri na maisha yao sio sisi wachanga kiumri tunataka kuishi kama wao wakati hatuna Afya wala elimu ya kutuwezesha.
Sisi akina Yakhe tuliposikia Ubepari tumeuvamia pasipo kuwa na umri wa kuvaa suti, hatuna mtaji, elimu wala ujuzi wa biashara hizo, ndio maana kweli tuna Hospital nyingi, shule na kadhalika lakini hizi zote haziwezi ruhusiwa ktk nchi nyingine yeyote kwa sababu they are below the standard! - Madawa feki na vifo vimezidi kuliko wakati wowote ule, hawana facilities zakutosha hata usafiri tu hawana. Huko mashuleni tumefikia kupeleka secondary hata walio fail na huko vyuo vikuu ndio usiseme, wanajengwa kina kujua huku hawajui kama hawajui kwa kujua wanajua wao zaidi - copy and paste materials - samahani lakini.
Haya ndio maendeleo ya kuwapa watu elimu na huduma ya Afya kweli ili mradi leo tuna vingi kuliko wakati wa Nyerere hali watu hao wanatoka mashuleni kabuntas na wagonjwa wakifa kwa maradhi madogo sana yanayotibika.
Leo hii NGOs wana Hospital na shule nzuri kuliko za serikali kwa watoto wetu hivi kweli tunategemea nini kama sii kujaribu kuvaa suti hali sisi bado tunatambaa.. Na hakika mkuu wangu kati ya watu 10 wanaoishi Ulaya leo ukiwaambia kuhamia Bongo kitu cha kwanza wao kufikiria ni ELIMU na AFYA zao hivyo 7 hurudi Ulaya, na wawili huondoka kwa sababu ya Usalama..That is a fact, na huyo mmoja anayebakia TZ leo hii hana hila isipokuwa mvuto wa Ufisadi kulipwa mshahara wa juu zaidi ya ujuzi na elimu yake..Tunajenga Taifa la Wagagagigikoko!
Mkandara, Tatizo si UBEPARI, tatizo ni ubinafsi, Rushwa, Kulindana, kutokufuata kanuni na sheria za kazi, kutokuwa na elimu bora ya Uraia kwa wananchi nakadhalika.
Haijalishi kama nchi ni ya KIJAMAA au KIBEPARI kama kuna matatizo ya kupita kiasi ya hayo ninayoyaelezea hapo juu kamwe haiwezi kupiga hatua. chukulia mfano huu, Kuleta makampuni binafsi ya uchimbaji wa madini ni kitendo cha kibepari, lakini kuandaa sheria mbovu na mikataba mibovu si kitendo cha kibepari, bali ni cha kijinga.
au tazama mfano huu, Serikali kumiliki mashamba makubwa kilikuwa ni kitendo cha ujamaa wetu, lakini kuiacha ardhi tupu isiyozalishwa wakati kuna watu wenye uwezo wa kuizalisha halikuwa jambo zuri.
Sasa mambo kama hayo, ukichunguza kwa makini ndo maana utaona, yule mwanzilishi wa kimageuzi ya China, Mzee Deng Xiaoping akasema, "Haijalishi panya ni wa rangi gani, yule anayekamata panya ndiyo paka mzuri". akaenda mbele mpaka kuzi"dilute" sera za mzee Mao.
Zipo nchi ambazo mwanzoni mwa miaka ya sitini hali zetu zilikuwa hazitofautiani sana, mfano South korea, hawa waliamua kufuata njia ya Kibepari lakini ona sasa pale walipo, Kufanikiwa kwao si kwa sababu walifuata Ubepari kama ideology, wamefika hapa kwa sababu misingi ya ubepari wameifuata vizuri, na pia utawala wa sheria, wananchi wanajituma wanachapa kazi kisawasawa, sasa wewe jiulize katika nchi yetu leo tunajipa masiku mengi ya kutokufanya kazi, mfano Nyerere day, Karume day, maduka mijini saa kumi na mbili jioni yeshafungwa, wakati wenzetu wanaendelea kufanya biashara mpaka saa nne usiku na wengine zaidi, katika hali ya namna hii hata kama Serikali itamiliki Njia kuu za Uchumi kama hapo zamani hatuwezi kufika, kwa sababu vitakufa tena.
Mimi ninadhani badala ya serikali kumiliki vitu kwa niaba ya wananchi, wananchi wavimiliki wao moja kwa moja, kupitia mtindo wa hisa, hii ina tija zaidi, kwa sababu watu wanaiona faida ya juhudi yao moja kwa moja, watu wanakuwa responsible na hivyo vitu, watavilinda vizuri.
Ila cha msingi cha serikali kufanya, ni kutunga sheria nzuri za kuwalinda wananchi wao dhidi ya wawekezaji wa kigeni, na hivi ndivyo China walivyofanya hapo awali, huwekezi mpaka utafute mbia mzalendo mwekeze wote.
Serikali iendelee kuboresha miundo mbinu, elimu bora na si bora elimu.