Mwinyi ndiye Rais bora kuwahi kutokea katika Taifa hili, anaondoka wala hatuna kinyongo nae

Semi mojawapo za Mzee Mwinyi RIP ilikuwa, ombi la mkubwa ni amri.

Nilipenda kusikiliza hotuba zake sababu ya semi kama hizo.

Apumzike kwa amani.
 
Mbona mnamtolea fungu la kumi,Hana hela!?..mnamsaidia kuhubiri badala ahubiri mwenyewe huko tumsikie,au ni kibogoyo!?..Mara anataka sadaka ya kuteketeza,anapenda nyama choma na Hana wanyama!?
Kwa mujibu wenu waliotoa sadaka za kuteketezwa ni kina Musa ambao mnadai ni ndugu zenu katika Imaan.
 
Tafakuri Jadidi:

Mzee Mwinyi Anaondoka Na Hatuna Kinyongo Nae..

" Kila zama na kitabu chake"- Ali Hassan Mwinyi.
Na leo Watanzania zimetufikia habari za kuhitimishwa kwa Sura ya Mwisho ya Kitabu Cha Mzee Mwinyi. Ameifariki Dunia.

Umma umegubikwa na simanzi. Mzee Mwinyi tulimpenda sana.

Naam, kwamba ‘ Kila Zama Na Kitabu Chake’ maneno hayo yalipata kusemwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi. Ni miaka mingi iliyopita.

Kwenye kila zama na kitabu chake, Mzee Mwinyi anazungumzia juu ya nyakati. Uwezo wa kusoma alama za nyakati. Mwanafalsafa Benjamin Di Israel alipata kuzungumzia juu ya dhana ya kiongozi mzuri.

Kwamba kiongozi mzuri ni yule anayejijua mwenyewe na nyakati zinazomzunguka- He who knows himself and the time that sorounds him. ( Zilikuwa nyakati nyingine, siku hizi Kiongozi Mkuu aweza kuwa mwanamke kama ilivyo kwetu.)

Na ilivyo kwa mwanadamu, hata anapogombea nafasi ya juu ya uongozi wa nchi, mbali ya matarajio ya chama kilichomteua, naye, kama mwanadamu, huwa na matarajio yake ya anayotaka akumbukwe nayo pindi atakapotoka madarakani. Inahusu legacy.

Kwa mtazamo wangu, na wengi wenye kufuatilia masuala ya kisiasa, Mzee Ali Hassan Mwinyi alikuwa ' Mliberali'.

Alipoingia madarakani alikutana na jamii iliyozoea ' marufuku' ya hiki na kile. Mzee Mwinyi akaja na ' ruksa' kwa watu kufanya mambo yao alimradi wanafuata sheria. Ndio msingi wa kuitwa " Mzee Ruksa'.

Naam, zama za Mzee Mwinyi zilikuwa ni ' Zama za Ruksa'. Ni zama zilizofungua milango ya watu kufanya biashara na upana wa demokrasia ikiwamo uhuru wa watu kujieleza ikiwamo magazeti na hata Televisheni.

Na kwenye utawala wake, Mzee Mwinyi alivumilia maneno mengi dhidi yake. Mwinyi hakuishia kusemwa tu, kuna hata waliodiriki ' Kumtukana matusi ya nguoni' kama alivyotamka mwenyewe kwenye moja ya hotuba zake miaka ile ya 90 mwanzoni.

Lakini, Mzee Mwinyi hakuyumbishwa katika yale mema aliyoazimia kuwatendea watu wake.

Siku moja kabla ya kukabidhi madaraka kwa Benjamin Mkapa, Mzee Mwinyi, akiwa chini ya shutuma nyingi dhidi yake kwenye vyombo vya habari na hata Wana- CCM wenzake, alichagua kwenda kuzungumza na Wananchi pale Manzese.

Ndio, Mwinyi aliongea na wananchi wa hali za chini kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Ukombozi; eneo la Manzese Uzuri. Nilikuwepo pale viwanjani kushuhudia tukio lile.

Mzee Mwinyi kwenye hotuba yake alianza kwa
kuwashukuru wananchi na baadae akasema;

" Ndugu zangu,

Nilipoingia madarakani niliwakuta mkipanga foleni ya sukari, unga, na hata mkinunua bidhaa muhimu kwenye ' Maduka ya Kaya, kweli si kweli?"

" Kweliii...!" Umma uliitikia.

"Je, leo mnapanga foleni ya sukari au kwenda kununua bidhaa muhimu kwenye maduka ya kaya tu?" - Mwinyi aliwauliza wananchi wale.

Jibu likawa la sauti ya jumla;

" Hapanaa!"

Mwinyi akaendelea na kuwapa mifano mingine kadhaa ya hali aliyoikuta akiingia madarakani, na kuwauliza wananchi wale kama hali imebaki hivyo hivyo kwa wakati ule akiondoka madarakani. Na majibu yakawa ni ' Hapanaa!"

Na siku ikawadia. Ni siku ya kwenda Uwanja wa Taifa kukabidhi mamlaka ya uongozi wa nchi kwa Benjamin Mkapa. Kuna wananchi waliojipanga kutoka Ikulu ya Magogoni kumpungia mikono ya kumsindikiza Mwinyi akielekea Uwanja wa Taifa.

Na pale uwanjani Mwinyi alipokewa na sauti za ' Ruksaa, Ruksaa!" Ni kutoka kwa Wananchi.

Naam, kila zama na kitabu chake.

Kwaheri Mzee Wetu Mpendwa, Alhaj Ali Hassan Mwinyi.

PS:

Na kwenye moja ya hotuba zake za kuwaaga Wananchi wake Mzee Mwinyi alisikika akisema;

" Na wote walonitukana, hata matusi ya nguoni mie sina kinyongo nao."
Nasi twasema, hatuna kinyongo na Mzee wetu Ali Hassan Mwinyi.
Hakika huyu mzee ndiye aliyefanya mageuzi makubwa ya kidemokrasia na kiuchumi hapa nchini.mungu ailaze roho ya mzee ruksa mahali pema pepon.amina.
 
Mbona mnamtolea fungu la kumi,Hana hela!?..mnamsaidia kuhubiri badala ahubiri mwenyewe huko tumsikie,au ni kibogoyo!?..Mara anataka sadaka ya kuteketeza,anapenda nyama choma na Hana wanyama!?
Sasa nyie hamtoi fungua la kumi? Hivi unaelewa maana ya zaka? Hiyo ya kutekezwa Haina nguvu kwa sisi majirani zenu.... Kafara ya msalaba ina nguvu sana na inatosha.... Kuhubiri ni majukumu yetu, hatupendi nyie mpotee... Ndio maana tunawahubiria... Ila hatuwalazimishi kwa kuwapiga mabomu na kuwateka... Tunawafunulia kweli mkiikataa basi tunawaacha itajulikana baada ya maisha ya duniani kufika kikomo
 
Aisee nakumbuka aliuza Loliondo na mwandishi mchunguz wa habari hiyo aliitwa Katabaro, akauliwa. Sijui huyu mzee alitubu? Halafu kwa, kuwa amekufa mnamuita, Rais Bora. Kabla hajafa alikuwa sio mstaafu Bora.
Kuna Mwarabu mmoja alikuwa akitembeza bahasha mjini kama hana akili.

Huyo mwarabu alishafukuzwa kwa tabia zake za rushwa lakini alijipenyeza tena wakati wa mzee ruksa.

Akaachiwa tu, na inavyosemekana kwa maagiza ya kutoka juu?



Walichukuliwa viongozi kupelekwa kule misituni wachague na vitalo vyao kuwinda na kulishwa nyati mpaka wakalegea-huyo mkulu alikuwa akiyajua yanayoendelea?

Huo ndio ulikuwa mwanzo.

Sasa baada ya Mama Sitti kuchukua usukani wa maamuzi ya Kibiashara(inavyosemekana) the rest is history.

Wamasai wanaangamizwa na wanateseka sana.

Wametiwa Umasikini wa kutupwa.

Apunguziwe mateso kaburini.
 
Tafakuri Jadidi:

Mzee Mwinyi Anaondoka Na Hatuna Kinyongo Nae..

"Kila zama na kitabu chake"- Ali Hassan Mwinyi.
Na leo Watanzania zimetufikia habari za kuhitimishwa kwa Sura ya Mwisho ya Kitabu Cha Mzee Mwinyi. Ameifariki Dunia.

Umma umegubikwa na simanzi. Mzee Mwinyi tulimpenda sana.

Naam, kwamba ‘ Kila Zama Na Kitabu Chake’ maneno hayo yalipata kusemwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi. Ni miaka mingi iliyopita.

Kwenye kila zama na kitabu chake, Mzee Mwinyi anazungumzia juu ya nyakati. Uwezo wa kusoma alama za nyakati. Mwanafalsafa Benjamin Di Israel alipata kuzungumzia juu ya dhana ya kiongozi mzuri.

Kwamba kiongozi mzuri ni yule anayejijua mwenyewe na nyakati zinazomzunguka- He who knows himself and the time that sorounds him. (Zilikuwa nyakati nyingine, siku hizi Kiongozi Mkuu aweza kuwa mwanamke kama ilivyo kwetu.)

Na ilivyo kwa mwanadamu, hata anapogombea nafasi ya juu ya uongozi wa nchi, mbali ya matarajio ya chama kilichomteua, naye, kama mwanadamu, huwa na matarajio yake ya anayotaka akumbukwe nayo pindi atakapotoka madarakani. Inahusu legacy.

Kwa mtazamo wangu, na wengi wenye kufuatilia masuala ya kisiasa, Mzee Ali Hassan Mwinyi alikuwa ' Mliberali'.

Alipoingia madarakani alikutana na jamii iliyozoea ' marufuku' ya hiki na kile. Mzee Mwinyi akaja na ' ruksa' kwa watu kufanya mambo yao alimradi wanafuata sheria. Ndio msingi wa kuitwa " Mzee Ruksa'.

Naam, zama za Mzee Mwinyi zilikuwa ni ' Zama za Ruksa'. Ni zama zilizofungua milango ya watu kufanya biashara na upana wa demokrasia ikiwamo uhuru wa watu kujieleza ikiwamo magazeti na hata Televisheni.

Na kwenye utawala wake, Mzee Mwinyi alivumilia maneno mengi dhidi yake. Mwinyi hakuishia kusemwa tu, kuna hata waliodiriki ' Kumtukana matusi ya nguoni' kama alivyotamka mwenyewe kwenye moja ya hotuba zake miaka ile ya 90 mwanzoni.

Lakini, Mzee Mwinyi hakuyumbishwa katika yale mema aliyoazimia kuwatendea watu wake.

Siku moja kabla ya kukabidhi madaraka kwa Benjamin Mkapa, Mzee Mwinyi, akiwa chini ya shutuma nyingi dhidi yake kwenye vyombo vya habari na hata Wana- CCM wenzake, alichagua kwenda kuzungumza na Wananchi pale Manzese.

Ndio, Mwinyi aliongea na wananchi wa hali za chini kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Ukombozi; eneo la Manzese Uzuri. Nilikuwepo pale viwanjani kushuhudia tukio lile.

Mzee Mwinyi kwenye hotuba yake alianza kwa
kuwashukuru wananchi na baadae akasema;

"Ndugu zangu,

Nilipoingia madarakani niliwakuta mkipanga foleni ya sukari, unga, na hata mkinunua bidhaa muhimu kwenye ' Maduka ya Kaya, kweli si kweli?"

"weliii...!" Umma uliitikia.

"Je, leo mnapanga foleni ya sukari au kwenda kununua bidhaa muhimu kwenye maduka ya kaya tu?" - Mwinyi aliwauliza wananchi wale.

Jibu likawa la sauti ya jumla;

" Hapanaa!"

Mwinyi akaendelea na kuwapa mifano mingine kadhaa ya hali aliyoikuta akiingia madarakani, na kuwauliza wananchi wale kama hali imebaki hivyo hivyo kwa wakati ule akiondoka madarakani. Na majibu yakawa ni ' Hapanaa!"

Na siku ikawadia. Ni siku ya kwenda Uwanja wa Taifa kukabidhi mamlaka ya uongozi wa nchi kwa Benjamin Mkapa. Kuna wananchi waliojipanga kutoka Ikulu ya Magogoni kumpungia mikono ya kumsindikiza Mwinyi akielekea Uwanja wa Taifa.

Na pale uwanjani Mwinyi alipokewa na sauti za ' Ruksaa, Ruksaa!" Ni kutoka kwa Wananchi.

Naam, kila zama na kitabu chake.

Kwaheri Mzee Wetu Mpendwa, Alhaj Ali Hassan Mwinyi.

PS:

Na kwenye moja ya hotuba zake za kuwaaga Wananchi wake Mzee Mwinyi alisikika akisema;

"Na wote walonitukana, hata matusi ya nguoni mie sina kinyongo nao."
Nasi twasema, hatuna kinyongo na Mzee wetu Ali Hassan Mwinyi.
Tunamdai Loliondo, alimuuzia mwarabu
 
Back
Top Bottom