ofisa
JF-Expert Member
- May 15, 2011
- 4,362
- 4,101
Komando anakufa?
amekufa YESU sembuse komandoo
Komando anakufa?
Mwili wa marehemu LT.RA MLIMA utawasili Uwanja wa ndege wa kimataifa wa DAR leo jioni 1925hrs kwa ndege ya KQ 486.Mwili wa kijana wetu shujaa utapokewa kwa heshima zote kijeshi.Ikumbukwe marehemu alifariki akiwa mission ya UN alias MONUSCO tarehe 27 oct.Shujaa Mlima alikua commando aliyesomeshwa u-commando nje ya nchi na vile vile alikua mkufunzi wa makomandoo pale 92KJ.
Nchi imepoteza rasilimali muhimu na ya gharama sana katika masuala ya Ulinzi na Usalama.Marehemu alifariki papo hapo baada ya kupigwa risasi na sniper.
Vijana aliokua nao walijibu shambulizi hilo kwa nguvu kubwa na kufanikiwa kuondoka na marehemu (evacuation) na kuelekea kwenye ngome kwa usalama zaidi.mapambano yalikua makali lakini vijana
walipigana kishujaa kwa covering fire huku wakihakikisha hakuna majeruhi mwingine.
Marehemu ataagwa kesho Lugalo saa nne asubuhi, sala ya kumuombea marehemu itafanyika msikiti wa Mamulu Upanga, baada ya hapo, marehemu atazikwa makaburi ya Kisutu.
RIP, SHUJAA.UMEKUFA UKISAIDIA JIRANI YAKO AISHI KWA AMANI. U DIED WAVING TANZANIAN FLAG UP HIGH, SACRIFICING YOUR LIFE FOR OTHERS! THATS OUR JOB.RIP COMMANDO MLIMA.
Si unajua tena hao jamaa zetu...Wanadhani wao ndio pekee wanajua na kustahili kila kitu wengine ni maamuma tuMkuu "comrade" unakusudia nini au ndio hii hii ninayoijua mimi
nakupa 100, hakuna comando fake labda tz. Kuna comando wa kigoma anaitwa kimondo- muha? Alitoka jeshini bila taarifa. Jesh lilitumia nguvu nyingi kumtrace?alivopatikana walisema asiguswe hovyo kwani dogo alikuwa amemaliza mafunzo cuba.wanasema angeweza kupambana na zaidi ya watu 00. Nakubaliana nawe kuwa hatuna commando yebo labda wanyarwanda
Komando anakufa?
Akisikia commando akili zote zinahamia Hollywood.
Ni Mnyamwezi wa Tabora, na jina la Rajabu ni jina la utotoni unalopewa ukizaliwa ambalo ni la babu yake Rajabu Tambwe
kumbe ndiyo huyu ambaye ndugu yake ni huyu balozi mstaafu mzee tambwe niliyenae jirani kabisa hapa makonde mbezi beach? ila huyu mzee " mkaksi " balaa.
kuna komando chizi pale mwanza anaitwa malima mbona anatoa siri za jeshi na sioni hatua zozote kuchukuliwa
Mkuu nini tena, sijakupa "MKAKSI" una maana gani, nielimishe
Weye ndo mjinga kabisa niliewahi kumsoma, hivi unamjua sniper wewe?? Basi commando Yoni Netanyahu nae aliuwawa pale entebbe na sniper alikua takataka?? Kweli kuna watu na viatu,. Ww ni kiatu.. RIP commando Mlima.
Techno zimeongeza idadi ya mabwege humu ndani. Pole sana maana kwa akili hizo zinatosha tu kuendea haja kubwa hazina msaada kwa taifa
Kawaulize navy seal kilichowakuta Somalia.Ushawahi kuona mtu anatahiriwa makalio kwa kuburuzwa na jeep mitaani? Anyway,kwani makomandoo wako bongo tu? Unajuaje uwezo wa kijeshi wa huyo sniper na wenzie? Laiti mngejua haya makundi ya kigaidi na waasi yalivyojaa askari wenye mafunzo ya hali ya juu mngeelewa hatari inayoikabili dunia.Wewe ukisikia al shabaab, FDLR unawaza wavaa vipedo wa mtambani, laiti ungelijua wanapewa mafunzo gani na who is behind them!Even if you think JW ni the best, , don't forget that people like Kagame wamepitia humo humo na ndio hao wanajenga majeshi huko.So they know your ABCs.Jiulize why mara nyingi mmarekani hutumia sana special forces anapoendesha operations dhidi ya makundi kama haya.