Mwili haujaoza miaka sita tangu ulipozikwa, mama mtu alikuwa akiota mwanaye yupo hai

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Julia Petta alifariki mwaka 1921, baada ya hapo alizikwa kwenye Makaburi ya Mount Carmel yaliyopo Chicago nchini Marekani.

Alizikwa akiwa na gauni lake la harusi, inadaiwa kuwa mara baada ya msiba huo, mama wa marehemu, Filomena alianza kuota ndoto akiona Petta anamwambia kuwa yeye (Petta) bado yupo hai.

Inaelezwa kuwa ndoto hizo ziliendelea hadi miaka mitano tangu Petta alipozikwa.

Miaka sita tangu msiba, familia yake ikiwa imeshahama Chicago na kuishi Los Angeles, Filomena akaamua kurejea Chicago na kuomba ruhusa ya kufukua kaburi la mwanaye.

Baada ya kufungua wakakuta jeneza bado zima japo kuna sehemu lilikuwa limeshaanza kuoza, walipolifungua wakakuta mwili wa Petta upo vilevile, mama mtu akapiga picha mwili huo kisha wakafunika na kurejesha udongo.

Picha hiyo ikaweka kwenye maeneo ya makumbusho na ipo hadi leo hii.

Tangu alipoona mwili wa mwanaye kwa mara nyingine, akaamua kubaki Chicago hadi naye alipofariki mwaka 1945.

petta.jpg
 
hata kigoma kuna kazee walikuta hakajaoza, na Dar makaburi mnayaita sijui ya kinondoni niliona youtube jamaa wanasema kuna mtu walienda kuchimbua kaburi lake ili wazike mwingine wakakuta mwamba hajaoza licha ya kuzikwa zamani sana

Kwanza hii habari ya kufukua kaburi na kuzika mtu mwingine haijakaa sawa. How?
 
Kwanza hii habari ya kufukua kaburi na kuzika mtu mwingine haijakaa sawa. How?
kuna ufinyo wa sehemu za kuzikia huko Dar, sasa wahuni ambao ni vijana wanaoshinda makaburini kwa lengo la kujipatia kipato wakipewa pesa wanafukua kaburi then wanatoa mifupa na kuizika sehemu nyingine au kuifukia chini zaidi alafu maiti mpya inawekwa juu
ukiingia youtube utapata maelezo kamili mkuu,hasa hasa wanafanya kwenye kaburi ambalo limetelekezwa
 
Kuharibika au kutokuharibika kwa mwili kunategemea na jinsi mwili ulivyotunzwa(kwa kuhifadhiwa kwa dawa au la) kabla ya kuzikwa.

Pia aina ya ugonjwa uliosababisha kifo ni sababu nyingine mwili kuharibika mapema.
 
Wanaokufa bila dhambi hawaozagi kwani kadiri ya Imani ya wakristo kuoza ni matokeo ya dhambi kwani dhambi huleta uharibifu.
 
Huyo wa amerika hajaoza watu hawaamini hadi waone

Huku kwetu watu wanakufa, wanaombolezewa, wanazikwa na matanga yanaisha kisha baada muda wanapatikana wakiwa hai; lakini hatuamini wala baadhi yetu hatuamini kuwako kwa mapambano ya nguvu za shetani na zile za Mungu



Hatari sana

 
Natamani na Mimi nipate hii neema
yaani niwe Kama nimelala.
Nikiona mifupa ya wafu uwa naogopa sana
Hata kigoma kuna kazee walikuta hakajaoza, na Dar makaburi mnayaita sijui ya kinondoni niliona youtube jamaa wanasema kuna mtu walienda kuchimbua kaburi lake ili wazike mwingine wakakuta mwamba hajaoza licha ya kuzikwa zamani sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom