Nadhani Mhe Nchemba amekurupuka,anayopendekeza yalishawahi fanyika huko nyuma,ingekuwa vema kabla ya kuchangia akauliza kwanini serikali iliacha kuajili wahitimu wa fani zisizo za ualimu wa vyuo vikuu kuwa walimu.Mwalimu huwa amekamilika kufundisha somo husika,kama anazo elimu zifuatazo.
- Common Content Knowledge-ajue somo husika
- Specialized Content Knowledge-awe na mbinu za kuwasilisha somo kwa mwanafunzi
- Knowledge at Content Horizon-awe na elimu ya ziada ya somo husika,ajue mizizi ya kila mada
- Knowledge of Content and Student-awajue wanafunzi vyema,wanavyofikiri,wanavyokosea na namna ya kuwasaidia
- Knowledge of Content and Teaching-ajue taaluma ya ufundishaji akizingatia learners centres approach
- Knowledge of Content and Curricullum-aelewe vyema masuala yote yanayoihusu mitaala ya somo husika.
Rejea Prof Ball and Bass,(2009) Michigan University;Mathematical knowledge for teaching.Pamoja na utaalam huo unauhusu utaalamu wa uwasilishaji mitaala,mwalimu hufundishwa masomo mengine kama,psychology ya mwanadamu,sociology,philosophy na masuala ya uongozi na mipango.
Mtu asiyesomea ualimu atakuwa na Domain moja tu,COMMON CONTENT KNOWLEDGE basi.Atawaanda wanafunzi kukariri ili wafaulu mitihani na sio kupata elimu.Matokea ya kukariri badala ya kuelewa ndiyo yanayosababisha kupata wasomi uchwara kama Mhe Nchemba.Utafiti ulioendeshwa na wizara ya elimu wakati huo,ulionyesha mapungufu makubwa kwa wahitimu wa vyuo vikuu wasiosomea ualimu katika ufundishaji,ndio maana serikali ilisimamisha kabisa ajila kwa wahitimu wa vyuo wasio waalimu.Waliokuwa wameajiliwa walipelekwa vyuo vya ualimu wakasomee masomo ya ualimu.Serikali pia ilishauriwa kuongeza muda wa masomo ya shahada ya ualimu kuwa miaka 4 au 5 badala ya 3 iliyopo sasa.Kwa waliopo kazini ilipendekezwa mafunzo kazini yaendeswe mala kwa mala.Bahati mbaya serikali sikivu ya CCM haikufanya hivyo, ndio maana Mhe Sugu kasema serikali ya CCM ni ya wapumbavu.
Yapo mambo mengi yanayoporomosha elimu nchini,yamewekwa wazi kwenye riport ya 2010,kayasome Mhe,unachojaribu kupendekeza ni kitanzi kwa elimu nchini,labda ungeshauri watu hao wapelekwe vyuo vya ualimu kwanza ndipo waajiriwe.Kishauri chama chako cha CCM,kisiidharau elimu,itakuja kukiangamiza.NAWASILISHA