Mhariri wa gazeti la JAMHURI Deodatus Balile amedai kushangazwa na hatua ya Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba kushambulia vyombo vya habari bungeni kwa madai kuwa vyombo hivyo kazi yake ni kufanya uchochezi.
Akizungumza katika kipindi cha Tuongee Asubuhi cha Star TV asubuhi hii Balile amewapongeza wabunge Peter Serukamba na Jenister Mhagama wa CCM walioungana na wale wa upinzani kulaani mswada wa serikali wa kuzidi kukandamiza wanahabari.
Mwigulu Nchemba akichangia Mswada huo bungeni kwa kutumia lugha kali na ya kuudhi alivishambulia vikali vyombo vyote vya habari na hasa magazeti kwa madai kuwa lengo lao kubwa ni kutaka nchi isitawalike.Pia alilaani Chadema kwa kutoa hotuba ya upinzani iliyokuwa inatetea wanahabari.
Mwigulu alifika mbali kusema kwamba serikali ifanye haraka kuchunguza pasi za kusafiria wale wote wanaopinga mswada huo wa kukandamiza waandishi wa habari.Kwani alidai yeyote anayepinga mswada huo sio mzalendo!
Hata hivyo bunge liliukataa mswada huo kwa kauli moja hali iliyomsononesha sana Mwigulu Nchemba.
Akizungumza katika kipindi cha Tuongee Asubuhi cha Star TV asubuhi hii Balile amewapongeza wabunge Peter Serukamba na Jenister Mhagama wa CCM walioungana na wale wa upinzani kulaani mswada wa serikali wa kuzidi kukandamiza wanahabari.
Mwigulu Nchemba akichangia Mswada huo bungeni kwa kutumia lugha kali na ya kuudhi alivishambulia vikali vyombo vyote vya habari na hasa magazeti kwa madai kuwa lengo lao kubwa ni kutaka nchi isitawalike.Pia alilaani Chadema kwa kutoa hotuba ya upinzani iliyokuwa inatetea wanahabari.
Mwigulu alifika mbali kusema kwamba serikali ifanye haraka kuchunguza pasi za kusafiria wale wote wanaopinga mswada huo wa kukandamiza waandishi wa habari.Kwani alidai yeyote anayepinga mswada huo sio mzalendo!
Hata hivyo bunge liliukataa mswada huo kwa kauli moja hali iliyomsononesha sana Mwigulu Nchemba.