Mwigulu Nchemba: CHADEMA itakufa 2015

Mwigulu Nchemba: CHADEMA itakufa 2015

Kadri mtu unavyozidi kushikwa ugoni,ndivyo na uwezo wako wa kufikiri unavyozidi kupungua.Nakushauri bro achana na wake za watu itakusaidia kufikiri kwa kutumia kichwa tofauti na sasa unavyofikiri kwakutumia tumbo.kabla sijaliona anguko la CHADEMA nitaliona kwanza anguko la ccm na wachumia tumbo wote ukiwemo wewe na babu yako Wasira!!endeleeni kuwa watabiri lakin kumbukeni akina sheikh Yahaya leo wakowapi waliowatabiria watu kufa wakafa wao.
 
Mwigulu njoo cdm huwe dereva wa zzk hila lazima tukuapishe kwanza kuliko kuendelea chama ch Ukweli kitakufa kivipi nyie mna rais gani wakuteua mwenye thamani ya Silaa wote hamkubaliki utaona tu 2015
 
Atakiufa yeye na Chadema itabaki ikiwa chama tawala.
nchemba.jpg

Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba

CHAMA Cha Mapinduzi kimekitabiria kifo Chadema baada ya uchaguzi wa 2015 kikieleza kuwa CCM ikishinda, chama hicho kitakuwa hakina nguvu tena kwa kuwa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa atakuwa amechoka.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba aliliambia gazeti hili jana kuwa chama hicho kinapoteza umaarufu kadri siku zinavyokwenda hasa kutokana na siasa zake za uchochezi na mwaka 2015 ndio itakuwa mwisho wa chama hicho.


Alisema kitakufa na kitasahaulika kabisa, akisema sasa hivi vijana wameshaanza kuwakimbia, na kwamba anaamini pia baada ya 2015 hakuna diwani ambaye atagombea kupitia chama hicho.


Alisema pia ni mwaka ambao Katibu wa Chadema Willibrod Slaa amestaafu kwa kuwa alishatangaza asiposhinda atastaafu na Chadema haiwezi kushinda hivyo mwisho wa Dk Slaa ndio utakuwa umefika kwa kuwa nyota yake haitang’aa tena.


“Nguvu ya Dk Slaa aliyokuwa nayo miaka miwili iliyopita sio aliyonayo sasa na mpaka mwaka 2015 atakuwa ameisha kabisa.” alisisitiza.


Pia Mwigulu aliyataka makundi yaliyojichomoza ndani ya CCM ikiwa ni harakati za kuwania urais mwaka 2015 kuheshimu ilani ya chama hicho kwa kuitekeleza na kuisimamia kwa kutoleta vurugu ndani ya chama wala kujenga chuki kwa wale ambao hawawaungi mkono.


|”CCM ina utaratibu wake wa kupata mgombea na hatumzuii mtu kugombea, sisi kama kamati ya utendaji tunatekeleza maagizo aliyotoa mwenyekiti tutayasimamia kwa nguvu zote anayetaka kugombea ahakikishe havurugi chama na asitengeneze chuki kwa ambao hawamuungi mkono.”


Wakati huohuo Naibu Katibu huyo wa CCM na Mbunge wa Iramba Mashariki aliwataka wakazi wa Mtwara kuachana na propaganda zinazoenezwa na wapinzani kuhusu rasilimali ya gesi na badala yake wafanye kazi kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.


“Rasilimali iliyopo ni ya taifa na watafaidika, hakuna rasilimali ya wilaya fulani, bomba la gesi ni lazima lijengwe tutawaelimisha wakazi wa Mtwara, kwani hata Ziwa Victoria bomba lilijengwa kwenda Shinyanga badala ya Kwimba, kwa nini basi halikujengwa kwenda Kwimba wakati pale ni karibu zaidi.


“Utajiri unategemea na jitihada, wasitegemee kwa vile tuna rasilimali ya gesi basi wakae wategemee watapata utajiri bila ya kufanya kazi haiwezekani, wasisubiri kupewa vya bure, ni kama mikoa yenye madini halafu wakazi wa pale wategemee Serikali itawapa vocha za kuweka kwenye simu kwa vile madini yao kwao, haiwezekani ni lazima wafanye kazi.

Source: Mwananchi

My take:

- Attention ya CCM ni Dr. Slaa.
 
Kweli Dr.Slaa na Chadema ni kiboko ya magamba kila kukicha Chadema si wanyamaze tuu au ni ile ya hatawakishinda tumewatisha. Tanzania inaelekea kukombolewa.
 
Hadidhi ya fisi kumfuata binadamu akifikiri atadondosha mkono.
 
Kwani CHADEMA inawategemea vija hao masalia? kuna vijana wengi sana ambao wanaakili kuliko hao walioondoka..........hilo la vijana hujafanikiwa ni kama mwigulu anacheza mchiriku pole sana.
 
Msigwa alisema :

1. Mchumi anayedai ukitaka kutatua matatizo ya uchumi basi uombewe, huyu Mchumi ni wa kuombea.

2. Yeye na wenzake wanaombea Wazinzi, wanaokamatwa na wake za watu.

Hivi ni nani alikamatwa na mke wa mtu????

 
Last edited by a moderator:
aka mkosa chama tatizo la Watz tunashabikia tusilolijua kwani hamjua vita iliyopo cdm? kama hamjui hicho chama cha wachaga mtadanganyika mpaka lini fuatilieni mtaona au ni chama cha mzee Mtei
Hii imepitwa na wakati kama ulivyopitwa wewe.
 
Kwani walishasema nani anagombea? Kumbuka waligangaza dakika za majeruhi. Ni siasa uchwara kuombea mwenzako afe. Hivi ulishaona timu ya mpira inaomba wapinzani wafe? Si wanatak wawepo ili wawashinde bila ulalamishi? Tanzania inahitaji vyama imara ili kukuza demokrasi iwe ni cdm, nccr, cuf au ccm
 
Mwigulu,tuambie chanzo cha kupanda kwa gharama/bei za unga, mchele, maharage, mafuta ya kula, nishati, sukari, unga wa ngano, kodi ya nyumba, maji, umeme, vifaa vya ujenzi nk. Hii serikali inaweza kuvunja vibao vya matangazo ya biashara halali yaliyowekwa kwa kibali lakini ikaacha mabango ya waganga wa jadi yakining'inia kwenye nguzo za umeme huku yakihimiza watu wakapate msaada wa nguvu za kiume na yakaachwa tu; serikali ya loliondo! kwa karne hii kuwa na mawazo ya miaka 52 iliyopita ni hatari. Mabango haya yanawapa karama ya unabii kina mwigulu na mzee wa siesta (usingizi baada ya kushiba mchana) wasira kutoa unabii....watashindwaje wameambiwa na wataalam? Naifagilia chadema mno. Viva chadema! Viva viongozi! Viva wanachama na wapenzi wa chadema!
 
Mwigulu kapewa ulaji ccm kwa kuwa ni ndugu wa damu wa rizzy, ni mtoto wa mama mkubwa wa rizzy, mnapeana madaraka kindugu.
 
mimi naamini kuwa mungu amewapiga upofu ccm kiasi kwamba hawamjui wala hawamuoni adui yao wa kweli, wamefocus kwa dr na chadema. Adui wa ccm kwa sasa sio dr wala chadema bali ni umma wa watanzania na mungu wa watanzania. Hii ndiyo nguvu ama nyota ya dr na chadema. Hii ndiyo maana hata ccm walipojaribu kutumia pesa, mapandikizi na masalia kumchafua dr, wamejikuta wakitawanywa na wamebaki wakiangaliana na kuulizana "what happened?"

what i can say is mr mchemba's way of analysing issues is questionable, he is supposed to know that we are no more kids we see more than he can imagine, my advise be very very very careful to give us the proper candidate for the up coming elections, who is serious, clean by the real meaning, real loves and afeaid of god, auzike na msafi wa kweli, short of that you will live to remember this post.
 
Huuu ni" utaahira" wa wana CCM
Huu ni upeo finyu kabisa wa CCM
Huu ni "ujuha" wa viongozi wa CCM...

Mtu wanaedai kuwa ni mwanachama wao....wanamougopa kiasi hiki?...wanaombea astaafu!!!
Kumbe wanapo sema Zitto anafaa kugombea wanajua kuwa hana ubavu wa kuiongoza CDM!!

Wametusaidia kuwashtua wenye mashaka na uanachama wa Dr Slaa kwa CHADEMA!
 
Nadhani amekosea
2015 ni mbali sana , i THINK THIS 2013 NDIO MWISHO WENYEWE
 
Maneno yakisemwa na mpuuzi,halafa mwenye akili timamu akayashabikia mtu yule hatofautiani na kumwona mwehu kavua nguo naye akavua kisa eti ushabiki! NINAJUA,MNAJUA Kuwa Nchemba ni naibu katibu mkuu si kwa sababu anajua siasa ila kwa sababu alitoa MATUSI MENGI 2011 Kule Igunga na 2012 kule Arumeru,sasa kuropoka ndiyo kilichompa cheyo.Jimboni kwake hakuna maji,hakuna majosho kwa wafugaji,akina mama wanajifungulia sakafuni hakuna vitanda! Hayo ndiyo angezungumza kama angekuwa na akili Timamu,ADUI WA WATANZANIA SIYO CHADEMA angesema kabla ya 2015 ataua mafisadi,elimu duni,deni la taifa,wakwepa kulipa kodi, Ningemuelewa!
 
nchemba.jpg

Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba

CHAMA Cha Mapinduzi kimekitabiria kifo Chadema baada ya uchaguzi wa 2015 kikieleza kuwa CCM ikishinda, chama hicho kitakuwa hakina nguvu tena kwa kuwa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa atakuwa amechoka.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Mwigulu Nchemba aliliambia gazeti hili jana kuwa chama hicho kinapoteza umaarufu kadri siku zinavyokwenda hasa kutokana na siasa zake za uchochezi na mwaka 2015 ndio itakuwa mwisho wa chama hicho.


Alisema kitakufa na kitasahaulika kabisa, akisema sasa hivi vijana wameshaanza kuwakimbia, na kwamba anaamini pia baada ya 2015 hakuna diwani ambaye atagombea kupitia chama hicho.


Alisema pia ni mwaka ambao Katibu wa Chadema Willibrod Slaa amestaafu kwa kuwa alishatangaza asiposhinda atastaafu na Chadema haiwezi kushinda hivyo mwisho wa Dk Slaa ndio utakuwa umefika kwa kuwa nyota yake haitang’aa tena.


“Nguvu ya Dk Slaa aliyokuwa nayo miaka miwili iliyopita sio aliyonayo sasa na mpaka mwaka 2015 atakuwa ameisha kabisa.” alisisitiza.


Pia Mwigulu aliyataka makundi yaliyojichomoza ndani ya CCM ikiwa ni harakati za kuwania urais mwaka 2015 kuheshimu ilani ya chama hicho kwa kuitekeleza na kuisimamia kwa kutoleta vurugu ndani ya chama wala kujenga chuki kwa wale ambao hawawaungi mkono.


|”CCM ina utaratibu wake wa kupata mgombea na hatumzuii mtu kugombea, sisi kama kamati ya utendaji tunatekeleza maagizo aliyotoa mwenyekiti tutayasimamia kwa nguvu zote anayetaka kugombea ahakikishe havurugi chama na asitengeneze chuki kwa ambao hawamuungi mkono.”


Wakati huohuo Naibu Katibu huyo wa CCM na Mbunge wa Iramba Mashariki aliwataka wakazi wa Mtwara kuachana na propaganda zinazoenezwa na wapinzani kuhusu rasilimali ya gesi na badala yake wafanye kazi kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.


“Rasilimali iliyopo ni ya taifa na watafaidika, hakuna rasilimali ya wilaya fulani, bomba la gesi ni lazima lijengwe tutawaelimisha wakazi wa Mtwara, kwani hata Ziwa Victoria bomba lilijengwa kwenda Shinyanga badala ya Kwimba, kwa nini basi halikujengwa kwenda Kwimba wakati pale ni karibu zaidi.


“Utajiri unategemea na jitihada, wasitegemee kwa vile tuna rasilimali ya gesi basi wakae wategemee watapata utajiri bila ya kufanya kazi haiwezekani, wasisubiri kupewa vya bure, ni kama mikoa yenye madini halafu wakazi wa pale wategemee Serikali itawapa vocha za kuweka kwenye simu kwa vile madini yao kwao, haiwezekani ni lazima wafanye kazi.

Source: Mwananchi

My take:

- Attention ya CCM ni Dr. Slaa.

Mwigulu sikiliza. Wote walioiombea chadema kifo walikufa wao na wakaiacha ikishamiri.
Hivyo utakufa wewe tutakuzika singida na chadema itaendelea kustawi.
Wahaya wana msemo kuwa kadri unavyozidi kuombea mama yako wa kambo kifo hapo ndipo mama yako mzazi anapokufa
 
Mwigulu nchemba atakufa na chadema maana hana ajenda ya kitaifa au ya maendeleo kila siku anaweweseka na cdm,siku zinakwenda utabiri hautimiii!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom