Mwigulu Nchemba: CHADEMA itakufa 2015

Mwigulu Nchemba: CHADEMA itakufa 2015

anafikiri kuwa cdm itakufa kama alivyoua jina lake la asili la lameck?
 
Mwigulu Nchemba tupinge kati ya ccm na chadema ni nani marehemu mtarajiwa.
 
kumbe Dr.Slaa anawanyima usingizi hawa magamba.!
 
Lameck lete CD yetu uliyotuahidi maneno mengi wa nini tumekuchokaaaa.
 
Mbona kifo cha CHADEMA kinazidi kuahiliswa?tuliambiwa itakufa 2012,ikavuka salama,sasa tunaambiwa 2015!kulikoni?????????????

Wanaona mgonjwa ana roho ngumu!!! Ndio mana kila siku wanabadilisha malaika mtoa roho!!!
 
  1. Foolish mind discuss people but Intelligent mind discuss issues.
  2. A foolish man shall say anything,anywhere,anytime while a wiseman shall always choose a particular word and time to say.

Nimeanza nanukuu hizo kutaka kuonyesha huyu jamaa Mwigulu Lameck Mchembe ni mtu wa aina gani! Hii inadhihirisha kuwa CCM hailali usingizi kwasababu ya Dr. Wilbroad Slaa. Huyu Bwana Mchembe badala ya kuzungumzia issues za kitaifa anaanzisha character assassination dhidi ya Dr. Slaa! Huu ni ujinga,ujuha na uzezeta wa Mchemba na CCM yake. Inashangaza kuwa mtu anaweza kuitisha Press conference kumzungumzia MTU anayeitwa Dr. W.P.Slaa na akashindwa kuzumgumzia matatizo ya kiuchumi yanayoikabili Tanzania na watu wake! Hakika huu ni ubabaishaji wa hali ya juu!!

Mimi nafikiri ifikie mahali vyombo vya habari(Media) wafike mahali wakatae kuandika habari hizi za kipuuzi! Unless media watuambie wanalipwa kuandika habari hizi za kijinga. Wewe utaandikaje habari za mtu kuhusiana na Uchaguzi wa mwaka 2015 miaka 2 mbele na wala huna hakika kama atakuwa mgombea wa Urahisi mwaka huo???

Media acheni upuuzi huu. Tunataka kusikia habari za mipango ya kuwainua Watanzania kiuchumi kutokana na raslmali lukuki tulizonazo. Tuambieni kuhusu mchakato wa Katiba mpya,kuhusu Gesi ya Mtwara kwanini ipelekwe Dar bila ya kuwanufaisha Watanzania.

Tuambieni kwanini Dhahabu,Almasi na Tanzanite inahamishwa na wawekezaji Uchwara toka Tanzania bila ya kuwanufaisha kwanza Watanzania kwenye maeneo yao na nchi kwa ujumla.

Acheni porojo zenu na huyo Nchembe wenu.
 
Hivi CCM wamelogwa? Huwezi kuamini chama kilichoshikilia mpini kuongea kijinga kijinga na kijuha juha kama hivi. Hivi kusema kwamba Chadema itakufa baada ya 2015 itsaidia vipi nchi yetu kuondoka kwenye lindi zito la umaskini ujinga na maradhi? Kuna sababu nyingi za kuikataa CCM isiendelee kuongoza serikali na mojawapo ni kuwapa nafasi kubwa na nyeti watu wasiostahili nafasi hizo. Kwa kauli hizi, Mwigulu na watu wa aina yake hawakustahili kuwa wawakilishi wa kitu kingine chochote kinachohusu umma wa Tanzania. Naanza kuamini sasa kwamba siasa ni muhimu sana kutoachwa mikononi mwa wapuuzi.
 
aka mkosa chama tatizo la Watz tunashabikia tusilolijua kwani hamjua vita iliyopo cdm? kama hamjui hicho chama cha wachaga mtadanganyika mpaka lini fuatilieni mtaona au ni chama cha mzee Mtei

Masalia wewe hujambo.?
 
CDM inawaumiza sana kichwa kumbe,kila kukicha ndo kimewajaa mdomoni? Fikirieni namna ya kuwakomboa watz ktk dimbwi la umaskini etc

Mkuu Mzalendo, CHADEMA imewabinya ccm vilivyo hata Tanga ambako wanachi wa huko wameukubali kuwa Mazombi wa ccm, Henly Shekfu kupitia gazeti la Mwananchi la leo analia m.a.p.u.m.b.u yake kubinywa na anawaomba vijana wa Tanga waendelee kuwa Mazombi wa ccm ili apate unafuu wa mmbinyo wa CHADEMA.
 
Kauli za makada wengi wa CCM kwa maoni yangu yanazalilisha chama na kukifanya kionekane sera zake zimeshindwa kuwakomboa watanzania. Mimi bado naamini CCM ina sera nzuri ukilinganisha na vyama vyote vingine. Tatizo kubwa ni utekelezaji unaokwenda kwa matakwa ya watu na siyo matakwa ya sera hilo la kwanza. Lakini la pili ni hii tabia ya kila siku viongozi wanaamka asubuhi na matamko ya CHADEMA itakufa itakufa kwa maoni yangu inadhalilisha chama na viongozi husika.

Hivi CCM tumefilisika kufikiria jinsi ya kuwaletea maendeleo watanzania na kubaki na mawazo ya kufa CHADEMA tu? CHADEMA kwetu inaleta changamoto gani? kwa nini tusitafakari kwa nini watz wanaunga mkono chama fulani na siyo sisi? Leo hata viongozi wetu wakuu wanaogopa kuitisha mikutano ya hadhara kama wafanyavyo CHADEMA kwa hofu ya kutohudhuriwa na wananchi. HATUJIULIZI MASWALI hapa kwamba watz wamekasirika nini? nilitegemea kamati tendaji mpya itakisaidia chama lakini kila siku ni ndoto za CHEDEMA kufa na DK Slaa kuchoka hii ni sahihi kweli kwa KAMATI iliyo kama THINK TANKERS ya chama? kamati inayotarajiwa kumshauri vizuri Mwenyekiti wa chama na Rais wa nchi katika masuala mbambali yahusuyo nchi inawaza MTU na CHAMA!! Haya ndiyo inayomshauri MWENYEKITI/RAIS?

Kwa kweli huwa nakasirika sana na uendelezaji wa siasa za hovyo unaozidi kukiua chama badala ya kukijenga. NAMWOMBA MWENYEKITI WA CHAMA (CCM) AWE MAKINI NA KAULI ZA BAADHI YA MAKADA. vita vya CHADEMA plus DK SLAA haviwezi kukivusha chama badala yake vitatuletea madhara ya kukataliwa na WATANZANIA huko tuendako. TUWE MAKINI tutafute wapi tumejikwaa badala ya kukesha na CHADEMA na DK SLAA
 
upumbavu wenu wa kishabiki ukichanganya na ujinga mnapata majibu yenu kwamba uko wapi nyinyi washabiki tu! walaji wengine huo ndo ukweli, subiri nina waraka wa kikao cha siri kilichofanyika kwa Mtei ndipo utaamini nini ninachomaanisha soon nitaweka hewani kwa utaratibu nyie si akina Thomaso?

Upumbavu ni wa kwenu pamoja na masalia, unadhani chadema ni kama nyie mashoga mnaoendesha vikao vya siri kuwaua watu kwa makusudi.
mliendesha vikao vya siri kiwaua watu igunga mkawaua kweli, mlifanya vikao vya siri nyamongo mkawaua watu kulinda maslahi yenu na mwekezaji.
upumbavu ni wakwenu tuachieni chadema yetu tukomboe nchi.
 
Mojawapo ya sifa za kuwa mwana CCM ni kuwa na mtindio wa ubongo, sasa huyu anayejiita mchumi daraja la kwanza anatoa upuuzi kama huu sasa tutegemee nini toka ule mtambo wa matusi wa mtera?
 
Huko ni kuweweseka kwake Lameck Mkumbo aka Mwigulu Nchemba, kwani anajua baada ya CDM kuingia madarakani 2015 miongonî ya watu watakaopandishwa mahakamani napema kabisa ni wale viongozi waliokuwa wabafoji majina yao. N'a kwa kuanzia watatinga mahakamani yeye Lameck Mkumbo n'a rafiki yake Amimu Augustino aka Philipo Mulugo!!!
 
Nilikuwa sijajua kwamba Mwigulu ndiye aliyemrithi Sheikh Yahya Hussein!!!! Sasa nimejua.

Tiba
 
CHAMA Cha Mapinduzi kimekitabiria kifo Chadema baada ya uchaguzi wa 2015 kikieleza kuwa CCM ikishinda, chama hicho kitakuwa hakina nguvu tena kwa kuwa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa atakuwa amechoka.

Kwa kweli leo hii wameamua kusema kile wanachodhani kuwa ni tatizo kwao kuwa ni mtu anayeitwa Dr. Slaa. Wanaombea nguvu za mzee huyu ziishe wakidhani kuwa hakutakuwa na mwingine wa kuwapa tabu. Hivi hawajiulizi kwa mafano Zitto akaamua kutulia akazidi kuijenga imani ya wanacdm juu yake unadhani moto wake utakuwaje si wanaweza wakasema heri hata zama za Slaa. Hivi hawajiulizi majembe kama kina Mnyika, Lissu, Godbles Lema yatakuwa wapi kipindi hicho. Na zaidi ya yote ambao ndio mtaji mkubwa wa CDM je hali ngumu ya maisha ya Watanzania itakuwa imefikia kiwango gani. Kiukweli sijataka hata kuendelea na utoto wa Chemba baada tu ya kusoma aya ya kwanza. Slaa kwa sasa ndiye aliyedhihirisha kuwa na uwezo kama wa kina Kagame. Tumuunge mkono afumue huu mfumo wa kulena na kukumbatiana unaoongozwa na uamini katika ufisadi. Tanzania bila mtua wa aina ya Slaa haiwezekani!
 
Back
Top Bottom