Usemi huu sasa umeanza kujidhihirisha kutokana na mienendo ya viongozi wa cdm na wafurukutwa wao, kila pembe ya nchi hii ukiwakuta wanajadiri hawawezi kusema sentesi tano hajaweka matusi, kashfa, kutaja ccm, neno katumika, kahongwa na magamba, msaliti n.k.
Usemi huo una maana hii ; mtu akibeba mzigo mzito sana kuzidi uwezo wake, na mbaya zaidi mzigo unakuwa hauna faida yeyote kwa yule aliyeubeba wala kwa watu ndani ya jamii inayomzunguka, mtu huyu akichoka hutafuta mahali akautua ili apumzike, kwa sababu ya uchovu mkubwa mtu huyu huamua kuutua mzigo wake na kuegemea jengo moja bila kujua ni jengo la nini mara maumivu makali humkuta na kukatisha uhai wake! watu wapita njia hupita na kukuta mtu kafa ili hali kaegemea jengo hilo, mtu mmoja husikika akisema "mtu huyu kafa ameegemea choo", Ndivyo itakavyokuwa kwa wafurukutwa wa CDM, hawajatambua kuwa cdm ni mzigo usiobebeka, na hauna tija kwa Taifa jema la Tanzania. Wanatakiwa kujitambua vinginevyo "watakufa wakiwa wameegemea choo".