Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,185
- 17,706
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba leo, Ijumaa, Aprili 17, 2026, ametoa maagizo mawili kwa wanaosimamia mradi wa ujenzi wa Uwanja wa soka wa Arusha utakaotumika kwa Fainali za AFCON 2027.
Maagizo hayo ni uharakishwaji wa mradi huo pamoja na matumizi stahiki ya fedha za ujenzi wa uwanja huo.
Amesema uwanja huo unatakiwa kukamilika mapema ili kuendana na muda wa maandalizi waliopewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
“Kaguzi zitakuja mapema zaidi ya hapa. Fanyeni kazi usiku na mchana. Tusiweke dosari ambazo hazihusiani na maandalizi ya viwanja. Ongezeni vitendea kazi, ongezeni nguvu kazi ili tutekeleze mapema huo muda ambao tumeuweka.
“La pili tuendelee kuzingatia thamani na viwango vya fedha. Tutimize mahitaji na matakwa ya waendesha shughuli wa AFCON lakini lazima tuwape thamani ya viwango Watanzania ambao ndio watoa fedha ya ujenzi,” amesema Mwigulu.
Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo katika ziara yake ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Uwanja huo jijini Arusha.
Maagizo hayo ni uharakishwaji wa mradi huo pamoja na matumizi stahiki ya fedha za ujenzi wa uwanja huo.
Amesema uwanja huo unatakiwa kukamilika mapema ili kuendana na muda wa maandalizi waliopewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
“Kaguzi zitakuja mapema zaidi ya hapa. Fanyeni kazi usiku na mchana. Tusiweke dosari ambazo hazihusiani na maandalizi ya viwanja. Ongezeni vitendea kazi, ongezeni nguvu kazi ili tutekeleze mapema huo muda ambao tumeuweka.
“La pili tuendelee kuzingatia thamani na viwango vya fedha. Tutimize mahitaji na matakwa ya waendesha shughuli wa AFCON lakini lazima tuwape thamani ya viwango Watanzania ambao ndio watoa fedha ya ujenzi,” amesema Mwigulu.
Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo katika ziara yake ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Uwanja huo jijini Arusha.