Mtu mzima na Verified ID unakuja na Uzi ambao unaanza mstari ukiandika "INAONEKANA kuna maelekezo maalum"!!?????Inaonekana kuna maelekezo maalum ya kumsadia Kitila Mkumbo kuwa Mbunge la Iramba Magharibi jimbo linaloshikiliwa hivi sasa na Mwigulu Nchemba.
Kwenye mizunguko yangu jimboni humo, jimbo mojawapo kati ya majimbo machache yaliyobakia kutumia fedha za vijiji kufanyia siasa za CCM, Mwigulu amebaki kupiganiwa na watu wachache dhidi ya kundi kubwa linaloonekana linapokea maelekezo toka ngazi za juu ndani ya chama hicho.
Kitila Mkumbo inaonekana anazidi kukaza kitanzi kitakachomuua kisiasa Mwigulu Nchemba kwenye jimbo analoliongoza hivi sasa
Inaonekana na nani au wakina nani!? Una ushahidi pasi na Shaka wa hii taarifa yako!? Unatumia hisia zako binafsi kuwalisha watu Ugoro wa Chuki na rosti la Uzandiki kwa manufaa ya kina nani!?
Wewe mwenyewe inaonekana Hauna hata chembe ya uhakika na huu upuuzi wako na ndio Maana ukaanza kwa kuandika INAONEKANA. Otherwise undeanika hayo maelezo maalum kutoka huko mnakokuita JUU ya kumsaidia huyo Kitila Mkumbo.
Jitafakari kamanda. Propaganda Uchwara Hazina nafasi awamu hii.
Nasubiri ushahidi wa hayo "MAELEKEZO KUTOKA JUU".....