hivi karibuni tumeona mwigulu nchemba ukimvalisha mbwa bendera ya chadema, lakini kabla haujafanya hivyo ebu shughulikia yafuatayo halafu ukipata majibu yake endelea kufanya hivyo. Huu ni ushauri wa bure
1. Kwanini miaka ya 1970 kulikuwa na viwanda vingi ukilinganisha na nyakati hizi za ulimwengu wa sayansi na teknolojia-vimefirisika katika utawala upi?
2. Kwanini reli zote za zimeacha kufanya kazi- isipokuwa ile inayokwenda zambia?
3. Kwanini tanesco imefikia hatua ya kuzalisha umeme kwa kutumia generator na kuingizia nchi hasara ya mabilioni ya pesa kwa siku kwa kununua mafuta mazito?
4. Kwanini serikali ya chama chako inaendelea kulipa symbion tsh milioni 152 kwa siku tena kwa siri kubwa wakati bunge lilizuia kupitia ripoti ya mwakyembe . Na mnajua kwamba pesa hii ni ya watanzania maskini?
5. Kwanini wakulima wa jimbo lako la iramba wanaendelea kulima kwa jembe la mkono na kula mlo mmoja (ugali wa mtama) baada ya miaka 50 ya uhuru?
6. Kwanini mawaziri ndani ya chama chako wanakuwa na uwezo wa kumiliki nyumba ya milioni 700 ndani ya muda mfupi na hakuna anaewafuatilia?
7. Kwanini viongozi ndani ya ccm wanaweza kuchangia milioni 100 katika harambee ndani ya mwezi mmoja wakati wao ni watumishi wa umma-hizo pesa wametoa wapi?
8. Kwanini viongozi ndani ya chama chako wanamiliki bilioni 315 uswisi- wamepataje?
9. Kwanini aliyeiba pesa za epa hawatajwi na matokeo yake serikali inanunua watu ili iwavalishe kesi za danganya toto?
10. Kwanini kampuni ya ndege ya serikali (atcl) nayo imesimama kama ilivyo kwenye treni?
11. Kwanini serikali yako inalipa wabunge tsh 200,000 kwa siku huku mkijua kwamba watanzania waliowengi hawajui hata kesho yao?
12. Kwanini wabunge ndani ya chama chako wanaingia mikataba na tanesco na kusuply matari mabovu, kuiuzia tanesco mafuta mazito, kuiuzia tanesco nguzo za umeme toka iringa na kudanganya kuwa zimetoka africa kusini hivyo kuwauzia kwa mamilioni ya pesa?
13. Kwanini hamsemi nani anamiliki richmond na dowans?
14. Kwanini watumishi wa halmashauri walioiba mabilioni ya pesa kama ilivyo ripotiwa na cag serikali yako haiwachukulii hatua?
15. Kwanini kodi ya madini inazidiwa na kodi ya machinga?
16. Kwanini hospital nyingi hazina x-ray na ct scan, pia wagonjwa wanalala chini?
17. Kwanini hadi leo wanafunzi wanakaa chini?
18. Kwanini rushwa ya rada mmeibatiza jina tamu la chenji ya rada
19. Kwanini watanzania wanakwepa kupitishia mizigo yao kwenye bandari ya dar na kuhamua kupitishia ya mombasa?
20. Kwanini wezi wa mabilioni adhabu yao huwa ni kujiuzuru bila kuchukuliwa hatua?, tena hujiuzuru kwa kulazimishwa na bunge na siyo chama tawala
najua kuna mambo mengi ya kukueleza lakini ebu anza na hizo point kumi ndiyo ufanye maamuzi