Mwiba wa chuma(Zuki Gadu)

Mwiba wa chuma(Zuki Gadu)

Daudi Nyuso alikuwa kwenye vazi lake la suti ya bei ghali kutoka Uturuki, sigara mkononi na kikombe cha kawaha mezani. Miguu yake aliibebanisha na mgongo wake aliuegemeza kwenye sofa la sufi, macho yake yakilitazama dari. Alikuwa anatafakari jambo kuhusu mgeni aliyekuwa kwenye moja ya vyumba vya nyumba yake, mgeni ambae kwa taarifa alizokuwa nazo ni kwamba alikuwa Entebe kwa sababu yake na alitakiwa kuondolewa uhai wake na huyo mgeni ambae alitambulika kwa jina la Zuki Gadu, raia wa Tanzania. Mbali na yeye kuwa sebuleni, walinzi wake aliowaamini na wao walikuwa wamegewana kona za sebule kuhakikisha ulinzi madhubuti kwa bosi wao. Alimtazama mmoja kati yao, akamuita kwa ishara.
“Ondoa vitu vyote hapa mezani.” Alimwambia huku akizima sigara yake na kuitupia kwenye kitezo, kabla mlinzi hajaanza kufanya alichoalekezwa tayari yeye alishainuka na kuiweka suti yake, akapiga hatua kuelekea kwenye chumba kilichomhifadhi mgeni wake wa ajabu.
“Bakini hapa sebuleni.” Aliwaamuru walinzi wake waliotaka kumfuata. Agizo lake ni sheria na hakukuwa na wa kulipinga. Alikifikia chumba alichokikusudia, akafungua mlango ambao ulifungwa kwa nywila. Akaingia ndani ya chumba kilichokuwa na giza, akawasha taa na mwanga ukatamalaki. Chini ya sakafu iliyomwagiwa maji kulikuwa na kiumbe aliyelala usingizi mzito na asijue amelala kwenye maji. Alimtazama kwa zaidi ya dakika mbili pasipo na kufanya lolote, mawazo yake yalikuwa juu ya mgeni wake huyo ambae alikuwa bado hajarejewa na fahamu zake.
“Una sura ya upole isiyoendana na harakati zako. Sifa zako na wewe ulivyo ni vitu viwili tofauti.” Daudi aliongea kwa sauti ya chini huku akichuchumaa na kumgusa Zuki Gadu ambae bado alikuwa kwenye usingizi wa kifo.
“Una roho ngumu sana sijapata kuona, unaweza kumuua mtu kwa meno yako licha ya kuwa hukuwa na nguvu. Mmh! Ona ulivyojipakaza damu za mwanaume mwenzako mdomoni mwako.” Aliendelea kuongea huku akiwa anayachota maji kwa mkono wake na kuyamwaga kichwani kwa Zuki Gadu ambae alionesha mguso wa maji ulikuwa ukimpa hisia kwa kuwa alikuwa akitikisika kila matone ya maji yalipokuwa yakimgusa.
“Amka basi tuzungumze! Amka nikuoneshe mi nae ni mwanaume kama wewe.” Daudi alisema huku akiwa bado anaendelea na zoezi lake ambalo lilianza kuonesha kufanikiwa, mtu wake alikuwa akihangaika kuyafumbua macho yake.
“Utanichelewesha!” Alisema huku akiinuka, akatazama kwenye kona ya chumba kile kulipokuwa na meza iliyokuwa imebeba sanduku kubwa la chuma, akapiga hatua na kuifikia na moja kwa moja akalifungua sanduku. Macho yake yakakutana na vifaa mbalimbali vya kutesea, akavutiwa na nyaya za umeme, akazichukua na kulifunga sanduku kisha akaenda kuzichomeka sehemu maalumu ukutani,kisha akazichuna kidogo na kuzitupa chini kabla ya kuwasha ili kuruhusu umeme kuzitembelea. Hakuwa na wasiwasi kuhusu yeye kwa sababu alikuwa na viatu ambavyo havikuwa rafiki wa kupitisha umeme, alikuwa na raba zenye ufito mzito wa mpira. Kitendo cha nyaya za umeme kugusana na maji, umeme mkali ukasambaa haraka hadi alipokuwa Zuki Gadu na kumshitua kwa nguvu kubwa kiasi akazinduka haraka huku akiwa hana cha kufanya zaidi ya kuzisilikizia nguvu za umeme zilivyoutesa mwili wake.
“Hapo sawa.” Daudi alisema huku akizima umeme na kutulia akimtazama mgeni wake ambae alikuwa akihema kwa nguvu kubwa mithili ya mwenda mbio za masafa marefu.
“Naitwa Daudi Nyuso!” Alijitambulisha huku akichuchumaa kando ya uso wa Zuki ambae alianza kurejewa na nguvu zake baada ya hekaheka za kuamshwa na nguvu ya umeme. Mwili wake bado ulikuwa unatetemeka lakini aliweza kuinua macho yake na kumtazama mtu aliyejitambulisha kwake.
“Najua unaitwa Zuki Gadu au tuseme unaitwa Miguu ya kuku.. nitapenda kukuita hivyo.” Daudi alisema huku akiyarusha macho yake kwenye miguu ya Zuki, akaachia tabasamu la dharau.
“Inawezekanaje wembamba wa vimiguu vyako hivyo uwe tishio kwa maisha ya watu? Yaani hata kuku wangu wa kisasa wanasupu miguuni kuliko wewe... Hahaaaa. Au mpo wawili?” Aliuliza swali akimalizia kwa kucheka kicheko cha kinafiki.
“Miguu ya kuku.. hebu nambie umetumwa na nani kuniua.” Alisema huku akimgusagusa.
“Simjui.” Zuki akaiapata sauti yake.
“Humjui? Unawezaje kufanya kazi ya mtu usiyemjua?” Daudi alimuuliza.
“Si kanuni yangu kumjua anaenituma ila ni kanuni yangu kumjua niliyetumwa.” Zuki alijibu huku akifanya jitihada za kuinuka na kukaa kitako bila kujali alikuwa akikaa kwenye dimbwi la maji.
“Basi nipo hapa. Unaweza kuniua.” Daudi alisema huku akijipiga kifuani na macho yake makali yakitua usoni mwa Zuki ambae bado alikuwa anatazama chini pasipo na kumtazama mwenyeji wake.
“kama umepata nafasi kama hii, hakikisha umeniua. Usiponiua sasa hakika litakuwa kosa lako ambalo hutawahi kulijutia.” Zuki alisema huku akiinua uso wake na kumtazama Daudi Nyuso.
“Umelipwa shilingi ngapi? Nitakulipa mara saba zaidi ili umuue aliyekutuma.” Daudi alirusha ndoano yenye mnofu. Zuki Gadu alitabasamu kwa dhihaka kisha akamalizia kwa cheko kubwa.
“Nina kanuni zangu chache zenye manufaa. Nikishapokea pesa huwa sigeuki. Hata ungenipa utawala wa Uganda bado sitaweza kubadili maamuzi yangu. Kama unayonafasi ya kuniua, hakikisha umefanya hivyo na si janjajanja unayotaka kuifanya.” Zuki alimuonya.
“Basi sawa. Ngoja nikuoneshe mimi ni nani.” Daudi alisema huku akiinuka, akapiga miguu chini mara mbili na likatokea kitu ambacho Zuki Gadu hajawahi kufikiria kukutana nacho maishani mwake, wala hakuwahi kudhani zile soga za zamani enzi ya sungura na fisi zitakuwa na uhalisia kwenye maisha ya kidijitali.
“Ni nini hiki!!” Zuki alisema huku akiinuka haraka pale alipokuwa amejibweteka, ule uchovu na maumivu yote hakujua viliishia wapi, alichosikia kwa wakati huo ni mapigo ya moyo wake yalivyokuwa yakipiga kwa kasi kubwa mithili ya mdundo wa ngoma kwenye tamthilia za Ottoman.
Daudi Nyuso alikuwa amepotea kimaajabu mbele ya uso wake na hakujua alielekea wapi.
“Amewezaje? Huyu ni mtu ama jini?” Alijiuliza huku akikimbilia ukutani na kuegemea, macho yakapata nafasi nzuri ya kukitazama chumba kizima na asimuone.
“Mimi ni zaidi ya jini bwana mdogo. Utajisumbua bure kupambana na mimi.” Sauti ilisikika lakini mzungumzaji asionekane, hata upande sauti ilipotokea haikubashirika ni kama mzungumzaji alikuwa ameondoa mwangwi kwenye sauti yake kiasi kwamba usingeliweza kujua alikuwa akizungumza akiwa upande gani.
“Jito...” Zuki Gadu alitaka kusema kitu lakini haikuwezekana kabla ya pigo moja zito kutua kifuani kwake, aliyempiga hakumuona. Wakati akijiuliza mpigaji alikuwa upande gani, akashangaa akivutwa kwa nguvu na kutupwa chini kirahisi mithili ya gunia la mchicha. Akiwa anataka kuwahi kusimama akashangaa anakula konde lingine safi lililoyatikisa meno yake ya mbele na kumuacha akichuruzikwa na mchuzi wa damu.
“Leo ni siku ya furaha kwangu, sitaki nikuue. Endelea kukaa humu ndani hadi usiku wa leo nikuoneshe kwa nini niliwahi kuwa IGP wa muda mfupi zaidi kwenye historia ya Dunia. Jiandae pia kunambia aliyekutuma.” Sauti ilisikika na kufuatiwa na vishindo vya mtu aliyekuwa akitembea kwenye maji, muda mfupi baadae mlango ulikuwa unabamizwa kwa hasira. Na kwa sababu ya kubamizwa huko ukashindwa kujifunga vema na ukabaki wazi.
“Hii ni nafasi yangu pekee ya kutoka humu ndani, la sivyo huyu mchawi ataniua leo.” Aliwaza huku akiharakisha kukimbilia mlangoni, alifanikiwa kutoka na kuanza kutembea kwa tahadhari kuifuata korido ndefu iliyopambwa kwa mwanga mkali wa taa zenye kutumia kiasi kikubwa cha umeme. Hatua zake sita zilitosha kumfanya afurahie wazo lake la kujikomboa kabla hatua yake ya saba haijatowesha furaha hiyo. Zuki Gadu alibaki akiwa amekodoa macho na asielewe ni kitu gani kilichokuwa kimetokea kwenye maisha yake. Alijikuta akiwa amerudi kwenye chumba cha mateso na asijue alirudije. Ni kama alikuwa akitembea ndani ya chumba na si kutoka nje kama alivyodhani.
“Haiwezekani!” Zuki aliwaza kwa sauti huku akiruka hatua ndefu na kuufikia mlango ambao bado ulikuwa wazi, akaugusa na kuutikisa, ukatikisika kama alivyotaka. Akatoka nje na kugeuka kuutazama kama kweli ulikuwa nyuma yake na yeye alikuwa akitazamana na korido ndefu yenye mwanga wa kutosha. Ni kweli mlango ulikuwa nyuma yake kumaanisha alishatoka ndani ya chumba. Akapiga hatua moja ndefu, hatua ya pili kikatokea kitu kingine ambacho hakuwa akimedhania wala kukifikiria zaidi ya kukiona runingani kwenye sinema za Sultani Tamba. Mbele yake kulikuwa na bwawa la maji na hakuona mwisho wake.
“Nitakuwa naota!” Aliwaza huku akigeuka na kutazama nyuma yake, mlango ulikuwepo na chumba alichotaka kilikuwepo lakini rent vilikuwa zimezungukwa na maji, ni kama alikuwa katikati ya kisiwa.
“Ni nini hiki kinanitokea?” Alijiuliza huku akipiga hatua na kurejea ndani ya chumba cha mateso, akaurudishia mlango lakini hakutaka ujifunge. Akasimama katikati ya chumba na kufikiria cha kufanya lakini kila alichojaribu kuwaza hakuona kama kutakuwa na msaada kwake, kila kitu kilikuwa kigumu kwake kukabiliana nacho kwa wakati huo.
 
kufikiria cha kufanya lakini kila alichojaribu kuwaza hakuona kama kutakuwa na msaada kwake, kila kitu kilikuwa kigumu kwake kukabiliana nacho kwa wakati huo.
“Hapa si mahali pa kukaa...” Aliwaza na kurejea kuufungua mlango, lakini bado alikuwa katikati ya maji mengi ambayo hakujua yalitokea wapi na mwisho wake ulikuwa wapi. Vipo vifungo vingi lakini kile kilikuwa ni kifungo ambacho kilimuondolea utimamu wa mawazo yake kwa sababu kila kitu alichofikiria hakuona kama kitaweza kumsaidia. Hakuwa na namna zaidi ya kurejea ndani na kukaa juu ya meza huku akisubiri hatima yake. Alizidiwa ujanja na Daudi Nyuso.
“Wakati huu nimekutana na wapinzani wajanja kuliko nidhaniavyo..” Aliwaza huku akizungusha macho yake kwenye chumba kikubwa ambacho hakikuwa na samani ya ziada zaidi na meza aliyokuwa ameikalia.

**********
Wakati hayo yakiendelea kumkuta Zuki Gadu nchini Uganda, nchini Tanzania pia kulikuwa na jambo lingine linaendelea kwenye nyumba moja iliyokuwa maeneo ya Mbezi mwisho. Montana alikuwa anatoka bafuni akiwa amejifunga mtandio mwepesi uliorichora umbo lake kama lilivyo, uzuri wake uliongezeka mara dufu. Alitoka kuoga kwenye bafu la ndani ya nyumba aliyokuwa akiishi Malima Bilali na mwenyeji wake alikuwa amekaa sebuleni akiwa na pensi laini ambayo ilionesha namna ambavyo maungo yake yalikuwa yametutuka mithili ya Kobra aliyeguswa mkiani. Kwa wakati huo hakuna alichokuwa anaelewa zaidi ya kumtazama Montana aliyekuwa akijifuta maji mwilini mwake kwa namna ya kutikisa mwili na kuifanya milima yake miwili iliyojifungasha nyuma kucheza kwa namna ya kuvutia. Khanga iliyokuwa mwilini mwa Montana ikaanguka chini na kuliacha umbo lake kama alivyozaliwa, alimgeukia Malima bila kujali alikuwa mtupu, akayalegeza macho yake kwa namna ya kuonesha alikuwa na uhitaji mkubwa na mwili wa Malima. Malima hakutaka kuonekana mnyonge, aliinuka na kuivua nguo iliyokuwa imesalia mwilini mwake na kubaki kama alivyotoka tumboni mwa *****. Malima alijikesha kama mgonjwa wa akili aliyeona sindano yenye dawa, alikuwa haelewi yaendeleayo Duniani zaidi ya kile alichotarajia kukifanya kwa Montana ambae alikuwa akimfahamu kwa jina la Marry Mariam.
“Mmmh.. mh. Subiri kwanza mpenzi. Mali yako hii utakula hadi usaze.” Montana alilalamika kimahaba huku akiizuia mikono ya Malima isiuguse mwili wake, Malima akaishia kugugumia mithili ya gegedu.
“kuna kitu nilikuuliza lakini hukunijibu mpenzi...” Montana alisema huku akiyagusa maungo ya Malima.
“Ki...ki..kitu gani dear.” Malima alisema huku akiweka jaribio la pili la kuugusa mwili wa Montana na asifanikiwe.
“Ni nani mwenye ile pikipiki niliyokutajia namba zake? Waliiniibia wale bwana..” Montana alilalama kwa sauti ya kuzigusa hisia za Malima ambae alitamani kukataa kutoa ushirikiano na wakati huohuo alitamani kutoa ushirikiano ili asilikose umbo tata la mwanamke Montana.
“Dadie hawezi kuwa mwizi bwana...” Malima alijibu kwa sauti ndogo lakini ilipenya vema sikioni kwa Montana.
“Dadie ni nani mpenzi.. rafiki yako mmh..” Montana alisema huku akiongeza utundu kwenye mwili wa Malima ambae alikuwa amechagua kuganda na kufanyiwa lolote kwa kuwa yeye hakuruhusiwa kuugusa mwili wa mwanamke aliyekuwa mbele yake mtupu. Kuanzia wakati huo Malima hakujibu wala kusema lolote zaidi ya kugugumia kwa raha za kuguswa hapa na pale, kila alichoafanyiwa na kuulizwa alitia ugumu kujibu.
“Haonekani kutaka kujibu.” Montana aliwaza huku akimtazama mwenyeji wake namna alivyokuwa ameyafumba macho yake kwa raha za kuchezewa viungo vyake vilivyokuwa imara wakati huo.
“Ngoja nikuoneshe..” Alijisemea huku akimsukuma Malima.
“Kwani vipi mpenzi..” Malima alilalamika huku akijizuia kuikwaa meza yake ya kioo.
“Utanijibu maswali yangu kwa kheri ama kwa shari, Dadie ni nani na wewe ni nani?” Montana aliuliza akiwa na tabasamu usoni mwake lakini sauti yake haikusadiki tabasamu lake.
“Kwani una agenda gani mpenzi, ona nilivyo, tafadhali nisaidie kwanza halafu nitakujibu maswali yako yote.” Malima alitaka kucheza na mawazo ya Montana lakini ni kwa kuwa hakujua ni kiumbe gani aliyekuwa mbele yake.
“pengine hujanielewa, utanijibu kwa kheri ama kwa shari.” Montana alisisitiza lakini cha ajabu hakuwa akihangaika kuusitiri mwili wake, alibaki kama alivyo huku bustani yake yenye rutuba ya kutosha ikiwa ni ufuniko pekee kwenye tonkito yake ambayo hakujali kuusitiri hata kwa kuyabana mapaja yake.
“ Unamaanisha nini?” Malima aliuliza huku nae akili ikianza kumkaa sawa, alianza kuhisi kuna kitu hakikuwa sawa lakini shaka yake aliipata akiwa nje ya muda, wakati akifikiria cha kufanya alishangaa akirukiwa kwa pigo moja mujarabu lililotua vema kifuani mwake na kumsomba hadi chini, akataka kuwahi kuinuka lakini mbele yake alisimama mwanamke akiwa mtupu na hakumpa nafasi, alimshushia makonde mazito sehemu mbalimbali za mwili wake. Malima alishangaa akishindwa kujitetea mbele ya kiumbe aliyemchukulia kama kahaba anaowatongoza siku moja na kukubaliwa kwa visenti alivyonavyo, mwanamke aliyekuwa mbele yake hakuwa kwenye kundi hilo alilohisi na badala yake ikabidi amweke kwenye kundi la wanawake wenye kujua nini wanafanya na kujilaumu yeye kwa kuokota kila mwanamke bila kujiridhisha ni mwanamke wa aina gani.
“Shida nini?” Malima aliuliza huku akijaribu kuyazuia makonde mazito yaliyokuwa yakianguka mwilini mwake.
Montana hakumpa nafasi ya kujitetea, alimpiga maeneo muhimu ambayo yalikuwa yanadhoofisha nguvu za Malima. Alimshushia kipigo hadi alipohakikisha Malima amelegea na yupo tayari kufanyiwa lolote. Akaachana nae na kuufuata mkoba wake, akaufungua na kuchukua kudu akaenda kumfunga mikono na miguu kisha akamwinua na kumkalisha kwenye sofa na yeye akakaa mbele yake na kujiachia kama vile hakuwa mtupu mbele ya Malima.
“Unajua kutongoza eeh! Njoo unifanye utakavyo basi..” Montana aliongea kinafiki huku akimringishia. Malima alibaki akiwa amekodoa macho na asijue alitaka nini kwenye mwili wa Montana.
“Sasa utanambia wewe ni nani na Dadie ni nani au niingie awamu ya pili ya kipigo.” Montana alimpa machaguo.
“Huna cha kunifanya mwanamke kahaba kama wewe.” Malima alijitutumua lakini aliishia kuliona tabasamu safi usoni mwa Montana.
“Ngoja nikuoneshe kwamba mi nikahaba kweli.” Montana alisema na kuinuka, akaufuata mkoba wake na kuingiza mkono na alipoutoa ulikuwa na jiwe la mzani lenye uzito wa gramu 500, na lilikuwa na kamba nyembamba. Akapiga hatua kumfuata Malima aliyekuwa amekaa kwenye kochi na asijue kitu gani kilifuata, alishangaa akatandikwa kofi zito lililomuagusha chini kama mzigo na kwa kuwa alikuwa amefungwa mikono kwa nyuma na miguu ilifunganishwa pamoja, alijikuta akidondoka mzima mzima bila ubishi. Montana aliinama na kuzishika tunguri mbili zilizokuwa zimekimbilia ndani kwa dhahama ya vipigo na hofu iliyokuwa mwilini mwa mmiliki wake. Malima alifurukuta lakini hakuweza, alikuwa mtupu na miguu na mikono yake ikiwa imefungwa na kwa namna alivyoanguka kwa kujipinda, tunguri zake zilibaki nyuma na ndizo zilishikwa na kufungwa jiwe la mzani kisha akainuliwa na kukalishwa kwenye kiti na si sofa kama ilivyokuwa awali. Jiwe likazivuta tunguri kuelekea chini. Mwanzo alijikaza lakini dakika moja mbele alianza kuhangaika, maumivu yalikuwa makali kiasi kwamba alijikuta akipiga kelele kama mtoto mdogo aliyepokonywa ziwa ingali hajashiba.
“Mi si kahaba? Haya njoo uniwekee utakacho kinguni wa kigeni wewe...!” Montana alisema huku akijiachia kihasarahasara mbele ya Malima ambae alikuwa ameiva kwa maumivu, macho yalikuwa mekundu na mishipa ilimtutumuka.
 
“Mi si kahaba? Haya njoo uniwekee utakacho kinguni wa kigeni wewe...!” Montana alisema huku akijiachia kihasarahasara mbele ya Malima ambae alikuwa ameiva kwa maumivu, macho yalikuwa mekundu na mishipa ilimtutumuka.
“Unataka nini wewe?” Malima aliuliza.
“Nambie Dadie ni nani na nampataje.” Montana alisema huku akimtazama na kumcheka.
“Mi sijui bwana!” Malima alitia ugumu.
“Janaume zima unapiga kelele kama mtoto?” Montana alimkejeli.
“Nenda kuzimu mbwa wewe...” Malima alitukana kwa hasira.
“Kuzimu! Hah! Unadhani nimetoka wapi?” Montana alimuuliza kwa dhihaka.
“Unakatwa na shetani mwanamke wewe...” Malima aliendelea kubwabwaja.
“Shetani ni bwana angu wa usichana, unashangaa mi kukatwa nae? Au nimuite aje?” Montana alimjibu tena huku akirejea kwenye mkoba wake na kurejea akiwa na sindano ya kushonea nguo, akamfuata Malima na kukishika kichwa chake na kuiweka sindano kwenye sikio lake la kushoto na kuanza kuichoma ngoma ya sikio. Eh bwana eh.. Malima alipiga kelele kubwa kiasi kwamba hadi majirani walisikia, hicho sicho alichikitaka Montana, akaachana na zoezi lake na kuifuata radio, akaiwasha na kuongeza sauti kubwa na alipohakikisha hata ikipigwa kelele ya namna gani hakuna atakaesikia huko nje, akarejea kuendelea na zoezi lake. Muda wote hakujali kama alikuwa mtupu na Malima nae alikuwa mtupu.
“Sasa utanambia habari za Dadie au nibadili zoezi?” Alimuuliza huku akihakikisha sindano inazidi kuzama sikioni licha ya damu nyingi kuanza kutoka, tunguri nazo zilizidi kuzidiwa uzito na jiwe la mzani ambalo lilizidi kutaka kushuka chini na kamba ikazikaza vema sana kiasi zikaanza kuwa nyekundu kama panzi aliyechomwa na moto wa njiti ya kiberiti.
“Niache tafadhali... Nitasema...” Malima alisalimu na kurudisha majeshi.
“Haya unazo dakika mbili tu!” Montana alimwambia huku akienda kupunguza sauti ya radio na kusimama mbele yake bila kujali.
“Unanichelewesha paka mwizi wewe..” Montana alifoka huku akimshushia kofi zito lilitua kwenye lile sikio lililokuwa likitibiwa kwa sindano isiyo rasmi.
“Dadie ni... ni.. rafiki yangu anaishi Juck hotel..” Malima alibwabwaja.
“Ni mgeni hapa nchini?” Aliulizwa.
“Ndiyo..!” Alijibu.
“Anatokea wapi?”
“Ni mtu wa nchini Mali..”
“Aliletwa na nani?”
“Na..na... Aagh.. niue bwana..” Malima alitia ugumu.
“Nakuua kweli unadhani natania...” Montana alisema na kurejea kwenye mkoba wake na alipotoa mkono alikuwa ameshika mkasi mdogo wa kufanyia oparesheni.
“Unataka kunifanya nini we shetani wa kike..! Eh!” Malima alitatarika kwa maumivu huku woga nao ukiwa sehemu ya mtatariko wake.
“Nataka kukuua..si umesema nikuue? Njoja nikuue kweli ili nikukutanishe na mume wangu shetani...” Montana alimwambia huku akiishikashika shingo ya Malima.
“Niache... Nasema niache...!” Malima alisema kwa woga mkubwa kwa kuwa alishabashiri ni kitu gani kitafuata kwenye shingo yake.
“Bosi wako na huyo Dadie ni nani?” Aliulizwa.
“Ni Zibuabanda! Zibuabanda! Ni yeye nasema kweli kabisa.” Alijibu huku akiwa ameshindwa kuvumilia, akalimwaga kojo mbele ya kiumbe aliyekuwa akimuona kahaba muda mfupi uliopita.
“Umeamini mi ni demu wa shetani eeh! Kwa kojo hilo umeamini kweli mi nakatwa na shetani..” Montana alimdhihaki.
“Nisamehe..!” Malima aliomba.
“Zibuabanda anaishi wapi?” Alimuuliza.
“Anaishi hapohapo Juck hotel..”
“Na yeye ni mtu wa huko Mali?”
“Hapana! Yeye ni mtu wa Congo...”
“Na wewe ni mtu wa Congo?”
“Ndiyo!”
“Upo hapa unafanya nini? Na kwa muda gani?”
“Kwa miaka nane... Mi ni... Aahg... Niu...” Malima alitaka kutia ugumu lakini akawahiwa.
“Nikuue!” Montana akamuwahi na kuuweka mkasi shingoni na kumkata kidogo kiasi damu zikaanza kutoka kwa fujo.
“Haya utanambia au nimalizie kazi yangu hapo shingoni?” Montana alimkata mkwara mbuzi.
“Mi ni jasusi wa Rwanda..” Malima alijibu huku akilia kama mtoto.
“Jasusi? Jasusi wa Rwanda? Kwenu Congo lakini wewe ni jasusi wa Rwanda..”
“Ndiyo!”
“Unajasusi nini hapa kwetu?”
“Taarifa zote za kibiashara!”
“Good! Unamtu ambae huwa unaripoti kwake?”
“Ndiyo.. Ila yupo Kenya.”
“Huwa unawasiliana nae vipi?”
“Huwa anakuja mwenyewe kila mwisho wa mwezi.”
“Kwenye simu yako umehifadhi namba yake kwa jina gani?”
“Mrembo matata..”
“Mrembo! Ni mwanamke?”
“Mwanaume..”
“Turudi kwa Zibuabanda.. yupo hapa nchini kwa sababu gani?”
“Kulipa kisasi.”
“kwa nani?”
“Kwa Zuki Gadu..”
“Sawa..” Montana alisema na kurejesha sindano na mkasi kwenye mkoba, akalifungua jiwe kwenye kende za Malima na kulirejesha kwenye mkoba wake kisha akamfuata Malima, akambeba kama karatasi na kumweka begani kisha akaelekea nae mafuni na wote walikuwa watupu. Kituo cha kwanza kilikuwa ni kwenye jakuzi lililokuwa bafuni, akambwaga Malima bila kujali angelimuumiza au la, kisha akamwacha na kujitazama kwenye kioo, akaziona sehemu zilizoguswa na damu iliyokuwa ikimtoka Malima. Akafungua bomba la mvua na kuanza kuoga sehemu mbalimbali za mwili wake, wakati wote huo hakuwa amefanya lolote kwa Malima ambae alibaki kuwa shuhuda wa mwanamke mrembo akijimwagia maji, mwanamke ambae kama ungelisimuliwa unyama wake ungelikataa katakata na pengine ungeliigeuza Dunia kuthibitisha ubishi wako. Alipomaliza kuoga alifunga bomba la mvua na kumgeukia Malima ambae alikuwa amejikunyata kwenye jakuzi na asijue hatima yake, mikono na miguu yake ilifungwa, kende zake zilikuwa kwenye maumivu makali, sikio na shingo navyo bado vilikuwa kwenye maumivu na havikuacha kutoa damu.
“Ukionana na shetani mwambie nimemkumbuka sana.. mh!” Montana alimwambia huku akifungulia maji yaliyoanza kujaa taratibu kwenye jakuzi, akatoka na kumuacha Malima akipambana kujitoa kwenye jakuzi baada ya kugundua ni kitu gani kingelifuata kwake. Montana alienda kuvaa nguo zake kabla ya kutoka na kumwacha Malima akiwa katikati ya uzima na kifo, maji yalikuwa yamejaa kwenye jakuzi na kuanza kumnyima
 
Ukiona hivyo ujue kwenye ukoo wetu Kuna ka uhusiano na yule sungura wa sitaki mbichi hizi
 
Huyu jamaa nimemtumia hela mpaka leo ananizungusha tu ushahidi ninao akibisha naweka humu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom