Mwiba wa chuma(Zuki Gadu)

Mwiba wa chuma(Zuki Gadu)

Kudo

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2017
Posts
1,821
Reaction score
6,122
RIWAYA; MWIBA WA CHUMA.
Na; Bahati Kisarwa Mwamba.
Simu; WhatsApp 0658564341

1.

Siku kwake ilikuwa inaelekea kuisha vema. Jioni ya siku hiyo aliamua kuimalizia kwa kufanya mazoezi ya kukimbia kilomita nane. Alikimbia bila kujali waliomfahamu walikuwa wakimshangaa kwa namna ipi kwa sababu, hawakuwahi kumuona akikimbia zaidi ya kumuona akishinda mtaani kwa kujichanganya na watu mbalimbali huku akiwa amevaa kanzu, vazi ambalo liliwafanya majirani zake kumkariri hata kama alikuwa akitembea usiku mnene. Wapo waliompigia mluzi wa shangwe kwa kumuona akiwa amependeza kwenye vazi la trakisuti yenye bendera ya Tanzania.

“Leo Sheikh umeamua kupunguza mafuta?” Alisikika mama mmoja akimpazia sauti kutoka umbali mfupi na eneo alilokuwa akipita, akamjibu kwa kutabasamu na kumpungia mkono. Safari yake iliendelea kwa umbali aliohitaji, aligeuka na kuanza kurejea nyumbani kwake ambapo alipanga kuingia kwenye chumba cha mazoezi na kuzikata dakika mia moja na ishirini kama alivyokwisha zoea. Njiani alipishana na watembea kwa miguu, waendesha pikipiki, baiskeli na gari chache sana. Kuna wakati alipishana na wapasha misuli wenzake ambao kwao ilikuwa ni kawaida kukimbia kila inapofika jioni. Akiwa katikati ya safari yake kuna pikipiki moja ilimpita kwa kasi kubwa huku akiwa ameikwepa kwa sentimita chache sana, laiti kama asingelikuwa si mtu mwenye kuhisi hatari mapema pengine angeliishia kugongwa vibaya.

“Jamaa kalewa bangi tayari....” Aliwaza huku akitikisa kichwa kwa masikitiko na kuendelea kunyakua miguu kama kawaida, aliamua kumsamehe mwendesha hovyo huku akimuombea afike salama aendako.Alipokaribia njia ya kuelekea nyumbani kwake umbali wa mita mia moja kutoka barabarani, alipunguza mwendo na kuanza kukimbia taratibu ili kupooza viungo vyake kabla hajaanza kutembea kuifuata njia nyembamba iliyokuwa ikikatiza nyuma ya kuta za nyumba za majirani zake. Giza nalo lilizidi kukolea licha ya kwamba taa za majirani ziliwashwa na kuangaza kwa kiasi kikubwa kwenye njia aliyokuwa akikimbia na nusu kutembea huku akibana pumzi kidogo na kuiachia kwa namna ya kuyaandaa mapafu yake kupitisha hewa kwa kiasi kidogo baada ya kutoka kuyatumikisha kwa mbio za kasi. Hakuwa na wasiwasi kwenye njia aliyoizoea kwa zaidi ya miaka mitano tangu alipohamia kwenye nyumba yake mpya baada ya kuhama kutoka sehemu aliyokuwa akiishi zamani. Angelihofu nini ikiwa mitaa ilikuwa tulivu na hakuwahi kusikia kuna kibaka ama mwizi kaiba? Angelihofu nini ikiwa vijana wa mtaani walimfahamu na kumheshimu kuliko kawaida, ni nani ambae angeliweza kuinua hata mdomo wake kumtisha ingali kila mtu alimfahamu, kila mtu alimpenda na kulitaja jina lake la utani kwa furaha? Hakika wasiwasi wa kukatiza kwenye uchochoro wa kumfikisha kwake akili yake haikuwahi kuuwaza. Licha ya kutembea kwa kujiamini lakini kuna hali fulani ilianza kujijenga kichwani kwake, alianza kuhisi kuna hatari siku chache zijazo. Mwili na akili yake vilishirikiana kujenga picha ya matukio machache ya kubashiri ambayo hakutarajia kama yangelikuwa na matokeo mazuri.

“Na ni muda mrefu sana sijapata kazi wala kashikashi yoyote... Maisha yakiendelea hivi nina imani nitaanza kwenda msikitini au kanisani kwa kadri imani itakavyonielekeza.” Aliwaza huku akisimama katikati ya njia na kugeuka nyuma alikotoka, hakuona mtu wala kuhisi dalili ya uwepo wa mtu. Kwake wasiwasi ni akili na kila mara hutembea kwa tahadhari hata kama atakuwa hatazami nyuma lakini huyaacha masikio yake yanase kila tukio kama antena. Akaanza kuishusha zipu ya sweta lake huku akiumaliza ukuta wa nyumba ya tatu kabla ya kufika kwake. Vitendo vyote hakufanikiwa kuvimaliza, hakumaliza kona ya nyumba wala kumaliza kuishusha zipu ya sweta la trakisuti aliyovaa kabla ya macho yake hayajaona kivuli cha mtu mbele yake. Mtu yule alikuwa amekaa juu ya pikipiki yake na kuifumbata mikono yake kifuani, kichwa chake akiwa amekiziba kwa kofia ngumu ya kuendeshea pikipiki.
Alisimama ghafla huku mkono ukiganda na zipu na mguu mmoja ukishindwa kuinuka chini kuufuata mguu mwingine uliokwisha tangulia, macho hayakupepesa na ngozi yake ikajikunja kwa baridi ya ghafla iliyotowesha jasho lote alilotumikia kwa zaidi ya nusu saa. Sekunde chache baadae akili yake ilianza kufanya kazi na kumbukumbu zikarejea; mavazi na aina ya pikipiki ya yule mtu ni sawasawa na ile ambayo ilimpita dakika chache wakati akikaribia kumaliza mbio zake za ucheshimwili.

“Haiwezi kuwa bahati mbaya..” Aliwaza huku akisimama mguu pande na mikono akiishusha chini kwa namna ya kujiweka tayari kwa lolote mbele yake. Hakusogea mbele wale kurudi nyuma, alibaki akiwa amesimama na macho yake yakiwa mbele sawasawa na mwili wa mtu aliyekuwa amekaa tulivu kwenye kwenye pikipiki yake. Masikio yake nayo yalikuwa tayari kupokea mjongeo wowote kando yake.

“Safi sana...”Alijisemea mara baada ya kumuona mtu aliyekuwa kwenye pikipiki akishuka kwa namna yake, alishuhudia sarakasi safi isiyoacha kishindo wakati wa kutua chini. Macho yake yakiwa kodo kwa kiumbe aliyekuwa amesimama kando ya pikipiki yake, mwili wake ukajivunja kwa kwenda chini na mkono wake wa kulia ukazihesabu punje nne za changarawe na kuzitupia mdomoni kisha akasimama wima akiwa tayari kupokea barua ya mwaliko wa makonde. Hakutaka kuwa wa kwanza kupiga hatua kumfuata mtu ambae hakujua dhamira yake halisi ni ipi, akatulia huku umakini ukiwa juu zaidi kuliko kawaida, hakupepesa.

Alichokuwa akikisubiri ndicho na mwenzake alikuwa anasubiri lakini mwendesha pikipiki alipoona anategewa, akafanya kile ambacho alihitaji kufanya bila kupoteza muda. Kwanza akapiga hatua moja ndefu na kuiweka nyuma pikipiki yake kisha akayatazama mabega yake kwa namna ya kutaka kuona kuta mbili zilizomweka katikati, akachanua tabasamu lake kwa namna ya kudhihaki kisha akafanya kitendo ambacho mtu aliyekuwa mbele yake hakukiona vema. Alinesa na kwenda juu kisha akakanyaga ukuta uliokuwa kushoto kwake na kuutembea kwa kasi kumfuata Zuki Gadu ambae bado alikuwa anashangaa kitendo cha mwendesha pikipiki kukimbia ukutani mithili ya mjusi, alipomkaribia akajiachia na kutua chini kisha akanesa tena na kuruka juu kisha akajipinda na kuukanyaga ukuta wa upande wake wa kulia, kwa kasi ileile akapiga hatua tatu na kutua chini akiwa uso kwa uso na mbaya wake ambae alikuwa anatema punje moja ya changarawe na kubakiza tatu, akamchekea kwa dharau kisha akamtisha kama anataka kupaa tena lakini kabla hajafanya hivyo akaachia makonde matatu ya haraka haraka na yote yakajaa vema kifuani mwa Zuki Gadu ambae hakuelewa alipigwaje. Mpigaji hakuridhika na hakutaka kumpa mwanya wa kufanya lolote, akanesa na kuukanyaga ukuta kisha akafyatua teke kali lililotua vema kwenye mkono wa Zuki ambae alikuwa anajaribu kuukinga mkono wake ili kupunguza uzito wa teke hilo, lakini aliishia kuteguka mkono kwa namna teke alilopokea lilivyokuwa na ujazo mkubwa.

“Huyu jamaa mbona kama anavyuma mwilini?” Alijiuliza huku akitema kipande kingine cha changarawe na kusaliwa na vipande viwili mdomoni. Akanesa na kurudi nyuma lakini hilo likawa ni kosa ambalo hakupata muda mzuri wa kulijutia kabla ya kukutana na mateke mawili yaliyotua vema kifuani mwake kwa kupishana kwa sekunde chache, mateke hayo yalikuwa na uzito uliotosha na kumsukuma nyuma kisha kumbwaga chini kwa kishindo mithili ya mlevi aliyeanguka juu ya kaburi.
“Anapiga na haongei...!” Zuki alijisemea taratibu huku akijaribu kukabiliana na maumivu makali yaliyokuwa yaliyoanzia kifuani na kusambaa sehemu zingine za mwili. Licha ya maumivu hayo lakini alifanikiwa kujizoazoa na kusimama huku akitema punje nyingine ya changarawe na kusaliwa na punje moja pekee, macho yake yakiendelea kumshuhudia jamaa akiwa amesimama wima mbele yake bila kutaka kufanya lolote lile la ziada. Zuki Gadu aliingiwa na hofu kwa namna ambavyo adui yake alijipa utulivu mkubwa kiasi kwamba hakueleweka anakusudia kufanya nini na kwa mara ya kwanza alikiri kukutana na adui mwenye nguvu,kasi na ujuzi wa mapigano. Lakini hiyo haikuwa sababu ya yeye kushindwa kujipanga upya ili kutokuingia kwenye aibu ya kupigwa kwa mara ya kwanza kwenye maisha yake na hakutaka hilo litokee, lakini alishindwa kuelewa jambo moja muhimu kwenye maisha; siku hazifanani na hazina kurasa za kufanana kwenye maisha ya binaadamu.

Lakini angelijuaje ikiwa mara zote amekuwa mshindi kwa kila pambano aliloshiriki? Angelijua vipi ikiwa maisha yake yaliyojaa hekaheka za kila namna hayajawahi kumwingiza kwenye aibu ya kupigwa ama kushindwa kumudu jambo liloingia kwenye anga zake? Lakini hakujua... hakujua..

Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku alijiweka vema tayari kwa mpambano, akatega mtego wake ambao aliamini ni lazima adui auvae kwa namna yoyote. Akakaa mguu pande kisha akawa kama anachuchumaa na kuutanguliza mguu mmoja mbele huku akiiandaa mikono yake kufanya kile alichokusudia, akatega. Hila yake ilikuja kumshangaza hata yeye mwenyewe pale ambapo aliyemtegea alipofanya kitu ambacho hakukitarajia, jamaa alirudi nyuma hatua tatu kisha akaanza kukimbia kwa kasi ya duma, alipomkaribia aliteleza mithili ya mchezaji ashangiliae ushindi kisha akaachia mapigo matatu kwa namna ya kuvigawanya viungo vyake, ngumi ilitua vema chini ya kidevu cha Zuki Gadu huku miguu yake ikifanya kazi ya kuitengua miguu yake iliyokuwa imewekwa mkao wa mrukochura. Miguu ya kuku alipiga ukelele wa maumivu makali yalitokea sehemu tatu tofauti mwilini mwake na wakati huohuo jamaa yeye alikuwa akasimama wima nyuma yake huku akinesanesa tayari kwa kuachia pigo lingine ambalo alikuwa kalidhamiria. Akampiga kwa namna aliyoitaka yeye na taratibu Zuki Gadu akaenda chini mzimazima huku maumivu ya nyuma ya kichwa yakiwa ni makali kuliko kawaida, macho yake nayo yakaingiwa na ukungu na akashindwa kuona vema licha ya kujitahidi kadri ya uwezo wake kuona adui yake alitaka kumfanya nini. Licha ya maumivu na akili yake kuanza kushindwa kufanya kazi vema, lakini alijitahidi kujigeuza ili amuone vema.
“Hatimae leo nimepatikana!”Aliwaza huku akifanikiwa kumuona jamaa kama kivuli kilichokuwa kikimwinamia, akajaribu kurusha mikono lakini ikawa mizito, akatupa mguu lakini akagundua imekuwa mizito maradufu kwa sababu adui yake alikuwa ameikanyaga na kusimama juu yake huku akinesanesa kama vile amekosa mhimili sahihi.

“Aaggh!” Zuki aliunguruma kwa jaziba na wakati huohuo guu zito likatua kifuani na kumnyima hata pumzi ya kutatarika, akatulia huku akihema kwa taabu, alimuomba Mungu ampe angalau dakika chache za uhai ili aweze kujitetea kutoka kwenye mikono ya mtu ambae hakuwahi kudhani kama atakutana nae kwenye maisha yake, maisha ambayo amezoea kushinda kila mara. Maombi yake yalisikilizwa lakini hayakusikilizwa kwa namna aliyoitaka, akazidi kuishia nguvu na pigo la kichwa alilopigwa awali lilizidi kumchanganya kwa maumivu ambayo bado yalikuwa yakizidi kuharibu utimamu wa mwili wake, nguvu zikzidi kumkimbia na giza likazidi kufunika mboni za macho yake, hakujua kilichoendelea wala hakujua alichofanyiwa tena na adui yake ambae alikuwa akimwadhibu kwa nyodo na majivuno.

Tukutane jioni....
 
Masikio yake yalinasa sauti za vicheko vya watu kwa mbaali sana, lakini kadri muda ulivyozidi kwenda zile sauti za soga na vicheko zilizidi kuwa karibu zaidi na ngoma za masikio yake. Akatikisa vidole vya mikono yake, akajisikia, akafumbua jicho lake moja na kutazama mazingira aliyokuwepo, akawaona vijana watatu wakiwa wamekaa kando yake wakisogoa huku wakicheza karata. Akili yake ikaanza kufanya kazi taratibu huku akivuta kumbukumbu na kujaribu kubashiri ni wapi alipokuwa, jibu halikukawia...
“Nimefikaje kwangu? Hawa ni...” Alijiuliza huku akikurupuka kuinuka kwenye kochi alipolazwa na vijana watatu ambao walimuokota akiwa hoi, taabani.
“Braza... Taratibu braza uko kwako...” Kijana mmoja alisema huku akiwahi kuzuia asitumie nguvu kuinuka.
“Oh! Kumbe ni nyinyi?” Alijibaraguza huku akimzuia aliyetaka kumzuia asiinuke.
“Niko sawa.. Niko sawa.” Alisema huku akikaa na kufikicha macho yake huku akivuta na kushusha pumzi zake.
“Ni ninyi mlionifikisha hapa?” Aliwauliza.
“Ni sisi Kaka.” Mmoja alijibu huku akibwaga karata mezani na kumgeukia Zuki.
“Mlinikuta wapi? Kuna mtu mlimuona mahali mliponitoa?”
“Kuna mtu alitufuata kule kijiweni, alikuwa ni dereva wa pikipiki bila shaka kwa sababu alikuwa amevaa kofia ngumu na hakutaka kuitoa hata tulipomuomba kufanya hivyo..”
“Aliwambia ni kwa nini hataki?”
“Hatukutaka kumlazimisha, tulichohitaji kwa wakati huo ni kuwahi eneo alilotuelekeza ili kutoa usaidizi na kujua ni nani aliyelala njiani. Tulipokukuta hatukuwa na budi kukuleta hapa licha ya kwamba awali tulitaka kukupeleka hospitali..”
“Kitu gani kiliwafanya mnilete hapa badala ya hospital?”
“Aliyetuita ndiye aliyeshauri tukulete hapa.”
“Ahsanteni sana.” Zuki alisema huku akiinuka na kuelekea chumbani na kuwaacha vijana aliowafahamu wakiendelea na soga zao. Dakika tatu baadae alirejea akiwa na noti tatu za elfu kumi kumi, akawagawia wale vijana ambao walizipokea kwa bashasha.
“Ahsanteni sana ndugu zangu...usiku umekuwa mkubwa, naombeni tuzungumze kesho nikija kijiweni.” Aliwambia huku akiwapa mkono wa kheri. Jamaa hawakuwa na pingamizi, wangelipinga nini ikiwa mwenyeji wao ndiye aliyewataka waondoke? Wangelipinga nini ikiwa mifuko yao imetuna waliopata bila jasho? Waliondoka wakiwa hawajui mtu aliyewaita kusaidia ndiye aliyemshambulia ndugu yao wa hiyari.
Baada ya Zuki Gadu kubaki peke yake nyumbani kwake, maswali machache yalipita kichwani kwake kwa namna ambayo hakuweza kuelewa, alijiuliza yule mtu aliyemshambulia alikuwa ni nani na alitaka nini? Maswali yote hayakuwa na majibu wale hakuona mtu wa kuweza kuyajibu zaidi ya yule jamaa ambae alimvamia njiani na kufanikiwa kumzimisha, lakini angelimpata wapi? Likabaki swali ambalo hakuwa na jibu nalo. Mbali na hayo maswali lakini alijiuliza swali lingine ambalo hakutaka kuwauliza vijana waliokuwa ndani kwake, waliwezaje kuingia ndani ikiwa ni yeye aliyekuwa na funguo? Hapo akakumbuka kitu na haraka mikono yake ikakimbilia kwenye mifuko ya nguo alizovaa. Funguo hakuzikuta. Macho yakahamia kwenye kitasa cha mlango huku mkono wake mmoja ukisalia mfukoni baada ya kugusa kitu ambacho aliamini kwa asilimia zote hakuwa amekiweka yeye. Funguo zilikuwa zikining’inia mlangoni, mkono nao ulitoka na kipande kidogo cha karatasi na hakikuwa tupu.
‘ENTEBE PLOT 607.’ Karatasi ilikuwa na maelezo yaliyosomeka hivyo. Aliigeuza ili kujua kama kulikuwa na ziada nyingine kwenye karatasi hiyo lakini hakuonala ziada.
“Ujumbe wa nini huu? Huko Entebe kuna nini? Je, aliyeweka hii karatasi kwenye mifuko yangu ndiye huyohuyo aliyenipiga kiasi cha kupoteza fahamu?” Alijiuliza huku akiitazama karatasi kama vile hakuwa amesoma kilichoandikwa. Wakati akiwa bado anatafakari kuhusu karatasi hiyo masikio yake yakanasa sauti ya muito wa simu chumbani kwake, akainuka haraka na kwenda kuipokea. Alitarajia kuona namba au jina la mpigaji lakini vyote hakuviona, simu ilipigwa kutoka kwa mtu aliyezuia namba yake.
“Mh!” Aliguna huku akibofya kitufe cha kupokelea.
“Ujumbe umeshausoma bila shaka...” Sauti nzito upande wa pili ilizingumza kijivuni, ikaendelea..
“Kuna mtu anavuta pumzi huko Entebe, lakini kila akivuta mimi nahisi maumivu makali moyoni mwangu. Pumzi yake inanikondesha.” Alitua huku kwikwi za vilio zikisikika kutoka kwake, alikuwa analia.
“Wewe ni nani?” Zuki alimuuliza lakini ni kama alipuuzwa swali lake.
“Natuma pesa kwenye akaunti yako sasa hivi.. nitatuma pesa nyingi ambazo huhitaji kubageini. Nahitaji pumzi yake iondoke.” Jamaa aliendelea kusisitiza huku wakati huu akiangua kilio cha kwikwi mithili ya mtoto mchanga aliyeporwa nyonyo la mama yake.
“Punguza maigizo bro... Nikufahamu kwanza na pia nikwambie sihitaji kazi kwa sasa...” Zuki alifoka.
“N'nse..n’nse...! Zuki, nakujua vema sana..wewe ni Mwiba na siyo mwiba wa kijiti, ni mwiba wa chuma unachoma hadi moyo, unachoma hadi kwato za punda.” Jamaa alisema huku mara hii akiangua kicheko kikubwa kama si yeye aliyekuwa akilia sekunde chache zilizopita. Maajabu! Inawezekanaje mtu aliyekuwa akilia kwa kwikwi muda mfupi uliopita aangue kicheko mithili ya mtu aliyetekenywa na mpenziwe? Ebo!
“Sihitaji kazi yako...” Zuki alisema huku dhahiri akiwa amechukia.
“No! Kazi yangu huwa haipingwi. Naweka pesa, najua hutaweza kuvunja kanuni za kazi yako hasa ile kanuni namba nane, yaani ile ya kukutaka usivunje makubaliano punde ukishapokea pesa. Najua, najua..” Jamaa akaongea kwa kujiamini na mwisho akamalizia kwa kukohoa kikohozi kikavu, kikohozi ambacho dhahiri kililazimishwa.
“Huyu mtu wa aina gani? Mara alie, mara acheke na sasa anakoho..ni nani huyu?” Zuki alijiuliza huku akisikia upande wa pili ukikwaruza kitu kama ubao mkavu.
“Tizama ujumbe wa muamala kwenye simu yako..” Jamaa akasema na Zuki akashusha simu yake na kupangusa ili auone ujumbe huo, aliuona.
“Haiwezekani...” Zuki akasema kwa ghadhabu kubwa, aliona ujumbe uliosoma kiasi cha tsh milioni saba pekee. Alighadhabika kwa sababu aliona ni kama dharau alifanyiwa, dharau ambayo hakuwa amefikiria. Kulipwa milioni saba kwa kazi ya kuua mtu nje ya nchi? Hakika Zuki hakuwa mamluko wa bei rahisi kiasi hicho, wala hakuwahi kufanya kazi nyepesi kiasi hicho.
“Una utani na mimi?” Zuki alimuuliza.
“Utani? Tangu lini nikataniana na watu wembamba kama wewe? Yaani nitaniane na mtu hatari kama wewe kweli? Aah! Lakini ngoja nikuhakikishie sitanii...” Jamaa alisema huku akimalizia kwa kupiga uluzi na dakika moja baadae kwenye simu kukawa na mtu mwingine lakini mtu huyo hakuwa na mbwembwe kama za yule wa awali bali alikuwa kwenye ombwe la maumivu makali kuliko kawaida, sauti yake ilitoka kwa taabu sana. Licha ya sauti ya mtu huyo kutokuwa kwenye utimamu halisi, lakini haikuwa sababu ya Zuki Gadu p.a.k miguu ya kuku kushindwa kuitambua, sauti ambayo kamwe haikuwa kutoka kichwani mwake hata kama ikimuamsha katikati ya usingizi wa uhai na kifo.
“Dodi! Dodi Danga!” Zuki alijikuta akitamka huku akipiga hatua moja chumbani kwake, alitamani kukimbia na kuwahi huko alikoshikiliwa rafiki yake kipenzi, Dodi Danga.
“Heheheee! Nadhani umegundua sitanii na hiyo pesa nimekupa kwa uungwani tu lakini sikupaswa kukupa hizo pesa. Nenda uminye pumzi ya mshenzi na mimi nitamuachia salama rafikiyo kipenzi Dodi Danga. Siku sita zinakutosha..” Alisema na kukata simu bila kusubiri jibu lolote kutoka kwa Zuki Gadu ambae alibaki akiwa ameganda katikati ya chumba chake mithili ya sanamu la uswekeni, hasira ilimkaba lakini hakuwa na sehemu ya kuishusha. Mwanzo alipigwa mithili ya paka aliyekula mboga ya shughuli na sasa anaagizwa kazi ngumu kwa mbadala wa kumuokoa rafiki yake kipenzi, rafiki kama ndugu.
“Ni nani watu hawa? Lakini sauti hii si mgeni masikioni mwangu, ni nani mtu huyo?” Alijiuliza huku akirejea kuitazama simu yake ambayo haikuacha rekodi yoyote ya mtu aliyepiga kwa namba fiche.
 
Masikio yake yalinasa sauti za vicheko vya watu kwa mbaali sana, lakini kadri muda ulivyozidi kwenda zile sauti za soga na vicheko zilizidi kuwa karibu zaidi na ngoma za masikio yake. Akatikisa vidole vya mikono yake, akajisikia, akafumbua jicho lake moja na kutazama mazingira aliyokuwepo, akawaona vijana watatu wakiwa wamekaa kando yake wakisogoa huku wakicheza karata. Akili yake ikaanza kufanya kazi taratibu huku akivuta kumbukumbu na kujaribu kubashiri ni wapi alipokuwa, jibu halikukawia...
“Nimefikaje kwangu? Hawa ni...” Alijiuliza huku akikurupuka kuinuka kwenye kochi alipolazwa na vijana watatu ambao walimuokota akiwa hoi, taabani.
“Braza... Taratibu braza uko kwako...” Kijana mmoja alisema huku akiwahi kuzuia asitumie nguvu kuinuka.
“Oh! Kumbe ni nyinyi?” Alijibaraguza huku akimzuia aliyetaka kumzuia asiinuke.
“Niko sawa.. Niko sawa.” Alisema huku akikaa na kufikicha macho yake huku akivuta na kushusha pumzi zake.
“Ni ninyi mlionifikisha hapa?” Aliwauliza.
“Ni sisi Kaka.” Mmoja alijibu huku akibwaga karata mezani na kumgeukia Zuki.
“Mlinikuta wapi? Kuna mtu mlimuona mahali mliponitoa?”
“Kuna mtu alitufuata kule kijiweni, alikuwa ni dereva wa pikipiki bila shaka kwa sababu alikuwa amevaa kofia ngumu na hakutaka kuitoa hata tulipomuomba kufanya hivyo..”
“Aliwambia ni kwa nini hataki?”
“Hatukutaka kumlazimisha, tulichohitaji kwa wakati huo ni kuwahi eneo alilotuelekeza ili kutoa usaidizi na kujua ni nani aliyelala njiani. Tulipokukuta hatukuwa na budi kukuleta hapa licha ya kwamba awali tulitaka kukupeleka hospitali..”
“Kitu gani kiliwafanya mnilete hapa badala ya hospital?”
“Aliyetuita ndiye aliyeshauri tukulete hapa.”
“Ahsanteni sana.” Zuki alisema huku akiinuka na kuelekea chumbani na kuwaacha vijana aliowafahamu wakiendelea na soga zao. Dakika tatu baadae alirejea akiwa na noti tatu za elfu kumi kumi, akawagawia wale vijana ambao walizipokea kwa bashasha.
“Ahsanteni sana ndugu zangu...usiku umekuwa mkubwa, naombeni tuzungumze kesho nikija kijiweni.” Aliwambia huku akiwapa mkono wa kheri. Jamaa hawakuwa na pingamizi, wangelipinga nini ikiwa mwenyeji wao ndiye aliyewataka waondoke? Wangelipinga nini ikiwa mifuko yao imetuna waliopata bila jasho? Waliondoka wakiwa hawajui mtu aliyewaita kusaidia ndiye aliyemshambulia ndugu yao wa hiyari.
Baada ya Zuki Gadu kubaki peke yake nyumbani kwake, maswali machache yalipita kichwani kwake kwa namna ambayo hakuweza kuelewa, alijiuliza yule mtu aliyemshambulia alikuwa ni nani na alitaka nini? Maswali yote hayakuwa na majibu wale hakuona mtu wa kuweza kuyajibu zaidi ya yule jamaa ambae alimvamia njiani na kufanikiwa kumzimisha, lakini angelimpata wapi? Likabaki swali ambalo hakuwa na jibu nalo. Mbali na hayo maswali lakini alijiuliza swali lingine ambalo hakutaka kuwauliza vijana waliokuwa ndani kwake, waliwezaje kuingia ndani ikiwa ni yeye aliyekuwa na funguo? Hapo akakumbuka kitu na haraka mikono yake ikakimbilia kwenye mifuko ya nguo alizovaa. Funguo hakuzikuta. Macho yakahamia kwenye kitasa cha mlango huku mkono wake mmoja ukisalia mfukoni baada ya kugusa kitu ambacho aliamini kwa asilimia zote hakuwa amekiweka yeye. Funguo zilikuwa zikining’inia mlangoni, mkono nao ulitoka na kipande kidogo cha karatasi na hakikuwa tupu.
‘ENTEBE PLOT 607.’ Karatasi ilikuwa na maelezo yaliyosomeka hivyo. Aliigeuza ili kujua kama kulikuwa na ziada nyingine kwenye karatasi hiyo lakini hakuonala ziada.
“Ujumbe wa nini huu? Huko Entebe kuna nini? Je, aliyeweka hii karatasi kwenye mifuko yangu ndiye huyohuyo aliyenipiga kiasi cha kupoteza fahamu?” Alijiuliza huku akiitazama karatasi kama vile hakuwa amesoma kilichoandikwa. Wakati akiwa bado anatafakari kuhusu karatasi hiyo masikio yake yakanasa sauti ya muito wa simu chumbani kwake, akainuka haraka na kwenda kuipokea. Alitarajia kuona namba au jina la mpigaji lakini vyote hakuviona, simu ilipigwa kutoka kwa mtu aliyezuia namba yake.
“Mh!” Aliguna huku akibofya kitufe cha kupokelea.
“Ujumbe umeshausoma bila shaka...” Sauti nzito upande wa pili ilizingumza kijivuni, ikaendelea..
“Kuna mtu anavuta pumzi huko Entebe, lakini kila akivuta mimi nahisi maumivu makali moyoni mwangu. Pumzi yake inanikondesha.” Alitua huku kwikwi za vilio zikisikika kutoka kwake, alikuwa analia.
“Wewe ni nani?” Zuki alimuuliza lakini ni kama alipuuzwa swali lake.
“Natuma pesa kwenye akaunti yako sasa hivi.. nitatuma pesa nyingi ambazo huhitaji kubageini. Nahitaji pumzi yake iondoke.” Jamaa aliendelea kusisitiza huku wakati huu akiangua kilio cha kwikwi mithili ya mtoto mchanga aliyeporwa nyonyo la mama yake.
“Punguza maigizo bro... Nikufahamu kwanza na pia nikwambie sihitaji kazi kwa sasa...” Zuki alifoka.
“N'nse..n’nse...! Zuki, nakujua vema sana..wewe ni Mwiba na siyo mwiba wa kijiti, ni mwiba wa chuma unachoma hadi moyo, unachoma hadi kwato za punda.” Jamaa alisema huku mara hii akiangua kicheko kikubwa kama si yeye aliyekuwa akilia sekunde chache zilizopita. Maajabu! Inawezekanaje mtu aliyekuwa akilia kwa kwikwi muda mfupi uliopita aangue kicheko mithili ya mtu aliyetekenywa na mpenziwe? Ebo!
“Sihitaji kazi yako...” Zuki alisema huku dhahiri akiwa amechukia.
“No! Kazi yangu huwa haipingwi. Naweka pesa, najua hutaweza kuvunja kanuni za kazi yako hasa ile kanuni namba nane, yaani ile ya kukutaka usivunje makubaliano punde ukishapokea pesa. Najua, najua..” Jamaa akaongea kwa kujiamini na mwisho akamalizia kwa kukohoa kikohozi kikavu, kikohozi ambacho dhahiri kililazimishwa.
“Huyu mtu wa aina gani? Mara alie, mara acheke na sasa anakoho..ni nani huyu?” Zuki alijiuliza huku akisikia upande wa pili ukikwaruza kitu kama ubao mkavu.
“Tizama ujumbe wa muamala kwenye simu yako..” Jamaa akasema na Zuki akashusha simu yake na kupangusa ili auone ujumbe huo, aliuona.
“Haiwezekani...” Zuki akasema kwa ghadhabu kubwa, aliona ujumbe uliosoma kiasi cha tsh milioni saba pekee. Alighadhabika kwa sababu aliona ni kama dharau alifanyiwa, dharau ambayo hakuwa amefikiria. Kulipwa milioni saba kwa kazi ya kuua mtu nje ya nchi? Hakika Zuki hakuwa mamluko wa bei rahisi kiasi hicho, wala hakuwahi kufanya kazi nyepesi kiasi hicho.
“Una utani na mimi?” Zuki alimuuliza.
“Utani? Tangu lini nikataniana na watu wembamba kama wewe? Yaani nitaniane na mtu hatari kama wewe kweli? Aah! Lakini ngoja nikuhakikishie sitanii...” Jamaa alisema huku akimalizia kwa kupiga uluzi na dakika moja baadae kwenye simu kukawa na mtu mwingine lakini mtu huyo hakuwa na mbwembwe kama za yule wa awali bali alikuwa kwenye ombwe la maumivu makali kuliko kawaida, sauti yake ilitoka kwa taabu sana. Licha ya sauti ya mtu huyo kutokuwa kwenye utimamu halisi, lakini haikuwa sababu ya Zuki Gadu p.a.k miguu ya kuku kushindwa kuitambua, sauti ambayo kamwe haikuwa kutoka kichwani mwake hata kama ikimuamsha katikati ya usingizi wa uhai na kifo.
“Dodi! Dodi Danga!” Zuki alijikuta akitamka huku akipiga hatua moja chumbani kwake, alitamani kukimbia na kuwahi huko alikoshikiliwa rafiki yake kipenzi, Dodi Danga.
“Heheheee! Nadhani umegundua sitanii na hiyo pesa nimekupa kwa uungwani tu lakini sikupaswa kukupa hizo pesa. Nenda uminye pumzi ya mshenzi na mimi nitamuachia salama rafikiyo kipenzi Dodi Danga. Siku sita zinakutosha..” Alisema na kukata simu bila kusubiri jibu lolote kutoka kwa Zuki Gadu ambae alibaki akiwa ameganda katikati ya chumba chake mithili ya sanamu la uswekeni, hasira ilimkaba lakini hakuwa na sehemu ya kuishusha. Mwanzo alipigwa mithili ya paka aliyekula mboga ya shughuli na sasa anaagizwa kazi ngumu kwa mbadala wa kumuokoa rafiki yake kipenzi, rafiki kama ndugu.
“Ni nani watu hawa? Lakini sauti hii si mgeni masikioni mwangu, ni nani mtu huyo?” Alijiuliza huku akirejea kuitazama simu yake ambayo haikuacha rekodi yoyote ya mtu aliyepiga kwa namba fiche.
HII CHUMA NI KALI KAMA ILIVYO KIUKWELI
NATAMANI KUENDELEA KUSOMA ZAIDI NA ZAIDI
 
Tatizo la huyu mwandishi hana riwaya aliyowahi kuimaliza hivo haina haja ya kimya. Wenzako mbona tunasoma na kumaliza huna haja ya kusoma na kukoment. Maana hii ni kazi kama kazi nyingine. Hivyo SI jambo la busara kuharibu biashara ya watu. Pita kushoto

Na story zake zenyewe mbaya hazivutiii
Andikw yako upost maana hii ni kazi kama kazi anauza story zake kama unahitaji nzima nunua
 
Andikw yako upost maana hii ni kazi kama kazi anauza story zake kama unahitaji nzima nunua
Tunajua ww ndo huyo huyo mwandishi na ID zako mbili huoni uzi umedoda sababu ya riwaya zako hazina mvuto na hujawahi maliza hata moja kwenda huko
 
Huyu ni tapeli.afungiwe mimi nimemtumia pesa ili anitumie inbox hadi leo ni kimya
Hata mm pia nimemtumia pesa lkn ananizungusha tu, pesa yenyewe kaitisha mwenyewe et km uko tyr nikutumie riwaya tuma pesa leo! Toka nitume now ni wiki na hakuna kitu.
 
Hata mm pia nimemtumia pesa lkn ananizungusha tu, pesa yenyewe kaitisha mwenyewe et km uko tyr nikutumie riwaya tuma pesa leo! Toka nitume now ni wiki na hakuna kitu.
Hata mimi nimemtumia ila jamaa kakaa kimya,hajibu whatsapp sms wala nini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom