RALC255
New Member
- May 11, 2025
- 4
- 4
Presumption of Death katika Sheria ya Ndoa na Mirathi
➡️ Je, mtu anapotea bila mawasiliano kwa miaka mitano mfululizo… je, bado ni mume/mke wako halali?
➡️ Je, bado atahesabika yupo hai? unaweza kufungua mirathi bila cheti cha kifo chake?
➡️ Au kuolewa tena bila talaka?
Hili si swali la kufikirika pekee. Ni tatizo halisi linalowakumba watu wengi nchini, hasa wake au waume waliotelekezwa kwa ukimya bila talaka, bila maelezo, bila msiba. Sheria ya Tanzania inalizungumzia vipi jambo hili?
🔍 Presumption of Death: Nini Maana Yake?
Presumption of death ni tamko la kisheria linalomruhusu mtu kutangazwa kuwa amefariki ikiwa hajasikika kabisa kwa miaka mitano mfululizo, na hakuna aliye na mawasiliano naye ambaye angetarajiwa kuwa nayo kama angekuwa hai.
Sheria inayotumika ni:
Kifungu cha 161(1) cha Sheria ya Ndoa (Law of Marriage Act, Cap 29 RE 2019)
“A person shall be presumed dead if he has not been heard of for a period of five years by those who might be expected to have heard of him if he were alive.”
Kwa kifupi, kimya cha miaka 5 kinaweza kuwa kifo cha kisheria.
🧾 Kesi ya Msingi (Temeke, 2022): Salum Omary Hamad
Katika kesi ya Misc. Civil Application No. 36 of 2022, Mahakama Kuu Temeke ilimsikiliza Fatma Kitwana Ally ambaye mume wake alipotea mwaka 2017, hakusikika tena, na hakuacha ujumbe. Aliishi naye kwa ndoa halali na walikuwa na watoto wanne.
Alitaka kutangazwa kuwa mume wake amefariki ili aweze kufungua mirathi na kutumia mali alizoziacha kama:
➡️ Je, bado atahesabika yupo hai? unaweza kufungua mirathi bila cheti cha kifo chake?
➡️ Au kuolewa tena bila talaka?
Hili si swali la kufikirika pekee. Ni tatizo halisi linalowakumba watu wengi nchini, hasa wake au waume waliotelekezwa kwa ukimya bila talaka, bila maelezo, bila msiba. Sheria ya Tanzania inalizungumzia vipi jambo hili?
🔍 Presumption of Death: Nini Maana Yake?
Presumption of death ni tamko la kisheria linalomruhusu mtu kutangazwa kuwa amefariki ikiwa hajasikika kabisa kwa miaka mitano mfululizo, na hakuna aliye na mawasiliano naye ambaye angetarajiwa kuwa nayo kama angekuwa hai.
Sheria inayotumika ni:
Kifungu cha 161(1) cha Sheria ya Ndoa (Law of Marriage Act, Cap 29 RE 2019)
“A person shall be presumed dead if he has not been heard of for a period of five years by those who might be expected to have heard of him if he were alive.”
Kwa kifupi, kimya cha miaka 5 kinaweza kuwa kifo cha kisheria.
🧾 Kesi ya Msingi (Temeke, 2022): Salum Omary Hamad
Katika kesi ya Misc. Civil Application No. 36 of 2022, Mahakama Kuu Temeke ilimsikiliza Fatma Kitwana Ally ambaye mume wake alipotea mwaka 2017, hakusikika tena, na hakuacha ujumbe. Aliishi naye kwa ndoa halali na walikuwa na watoto wanne.
Alitaka kutangazwa kuwa mume wake amefariki ili aweze kufungua mirathi na kutumia mali alizoziacha kama:
- Viwanja vya makazi
- Akaunti za benki
- Mashamba
Mahakama ilikubaliana naye, na ikamtangaza mumewe kuwa amefariki kisheria.
Lakini pia katika shauri hilo, Mahakama Kuu Temeke ilieleza wazi kuwa:
“Disappearance for a minimum of five years is sufficient for a court to make such a declaration (presumption of death).” — Mugeta, J.
Lakini pia katika shauri hilo, Mahakama Kuu Temeke ilieleza wazi kuwa:
“Disappearance for a minimum of five years is sufficient for a court to make such a declaration (presumption of death).” — Mugeta, J.
Mahakama ilisema pia:
“It is time we enact a law akin to the Presumption of Death Act, 2013 of the United Kingdom to take care of the affair of missing persons.”
Hii inaonyesha ukubwa wa tatizo na umuhimu wa kufuatilia haki yako kisheria.
Lakini si kila mtu aliyepotea kwa miaka 5+ atahesabika amefariki. Mahakama huangalia mambo kama:
✅ Alikuwa akipatikana kirahisi awali?
✅ Familia ilichukua juhudi gani kumtafuta?
✅ Imetolewa taarifa polisi au magazetini?
Kwa wanawake waliotelekezwa na waume waliopotea, hii ni njia pekee ya kuendelea na maisha kwa heshima ya kisheria:
Hii inaonyesha ukubwa wa tatizo na umuhimu wa kufuatilia haki yako kisheria.
Lakini si kila mtu aliyepotea kwa miaka 5+ atahesabika amefariki. Mahakama huangalia mambo kama:
✅ Alikuwa akipatikana kirahisi awali?
✅ Familia ilichukua juhudi gani kumtafuta?
✅ Imetolewa taarifa polisi au magazetini?
Kwa wanawake waliotelekezwa na waume waliopotea, hii ni njia pekee ya kuendelea na maisha kwa heshima ya kisheria:
- Kuolewa tena kihalali
- Kurithi mali
- Kuwasomesha watoto kwa kutumia mali ya baba yao
❓Je, Wewe Upo Kwenye Hali Hii?
Unaishi kwenye ndoa ambayo mume au mke alitoweka miaka mingi iliyopita?
Umeshindwa kuendelea na maisha kwa sababu huna cheti cha kifo?
Umeshindwa kugusa na kutumia mali zilizokuwa kwa jina lake?
Basi huenda Presumption of Death ni njia yako ya kisheria ya kupata suluhisho.
Unaishi kwenye ndoa ambayo mume au mke alitoweka miaka mingi iliyopita?
Umeshindwa kuendelea na maisha kwa sababu huna cheti cha kifo?
Umeshindwa kugusa na kutumia mali zilizokuwa kwa jina lake?
Basi huenda Presumption of Death ni njia yako ya kisheria ya kupata suluhisho.
IMEANDALIWA NA
Robik Attorneys & Legal Consultants (RALC)
Near Ubungo Plaza, Dar Es Salaam
🌐 www.ralc.co.tz | Instagram ralc255
Email. info@ralc.co.tz | Phone. +255 683 505 715
Near Ubungo Plaza, Dar Es Salaam
🌐 www.ralc.co.tz | Instagram ralc255
Email. info@ralc.co.tz | Phone. +255 683 505 715
Angalizo Muhimu (Disclaimer):
Maelezo yaliyomo kwenye uzi huu yametolewa kwa madhumuni ya elimu ya jumla tu na hayawezi kuchukuliwa kama ushauri wa kisheria wa moja kwa moja. Robik Attorneys & Legal Consultants haitawajibika kwa matumizi yoyote ya taarifa hizi bila kupata ushauri rasmi wa kisheria.