Mwenyekiti wa Kijiji afungwa Miaka 20 Jela kwa kuharibu Miundombinu ya Gesi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
1689094833296.png
Hukumu imetolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Lindi dhidi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahumbika, Hamis Bandari baada ya kumkuta na hatia ya Matumizi Mabaya ya Madaraka.

Hamisi na mwenzake Juma Kapilima, mkazi wa Liwale, walitenda kosa la kuharibu na kuuza miundombinu ya Kingo za Mabomba ya Gesi, Juni 2022 na kulisababishia hasara hiyo Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Pamoja na hukumu hiyo, Washtakiwa wote wawili wametakiwa kulipa kiasi cha Tsh. 54,710,000 kama fidia kwa TPDC kutona na uharibifu uliofanywa.

============

Mahakama ya hakimu mkazi wilaya ya Lindi imemhukumu kifungo cha miaka 20 aliyekuwa mwenyekiti wa Kijiji cha Mahumbika wilayani humo Hamis Bandari (46) kwa kosa la matumizi mabaya ya madaraka.

Hamisi amepata hukumu hiyo Pamoja na mwenzake Juma kapilima (38) ambaye ni mkazi wa wilaya ya Liwale aliyehukumiwa miaka 20 pia kwa kosa la kuharibu miundombinu ya gesi na kuisababishia hasara shirika la maendeleo ya Pertoli Tanzania (TPDC) na serikali kiasi cha shilingi milioni 119.

Imeelezwa mahakamani hapo kuwa, watu hao walitenda makosa hayo mwezi Juni 2022 baada ya kuharibu miundombinu ya mabomba ambayo yanayotumika kuweka kingo katika sehemu linapopita bomba la gesi na kisha kwenda kuyauza.

Hukumu hiyo imetolewa na hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya Lindi Maria Batulaine ambapo pia amewataka wawili hao kulipa shirika la TPDC fidia ya Shilingi Milioni 54,710,000
 
Wezi wa mabilioni na Mafisadi wanapeta mtaani ila Mtu mdogo kama Mwenyekiti wa Kijiji anafungwa miaka 20 eti Kwa kutumia madaraka vibaya Kuiba Mabomba,hii sio sawa.


My Take
Muogopeni Mungu nyie Mahakimu na Watawala,hukumu ya Haki inakuja.
 
Hiyo adhabu haiendani na huo uharibifu lakini Kuna watu wakubwa kibao wamewahi shitakiwa Kwa matumizi mabaya ya ofisi lakini hakuna hata mmja amewahi fungwa Kwa hatia ila huyu maskini ndio anapigwa nyumdo zote hizo?
Ndio maana nikasema inaudhi kweli kweli kusikia walioiba mabilioni hata kupelekwa mahakamani haitokei lakini ubadhilifu wa milioni mahakamani haraka na hukumu inatolewa haraka na Kali sana. Ila tukirudi upande mwingine nawaza huyu mwenyekiti hakujua ni kosa kisheria? Je tutetee? Kikubwa tutii Sheria hasahasa ukijijua wewe n masikini Hana wa kumtetea.
 
Bila Pesa hata sasa hivi umefungua huu uzi unaonekana unapga makelele.

Ukiwa na Pesa kila kitu ni point utachoshauri na kutamka.

nchi yetu hii bila pesa Ni chungu amani utaiona kwenye Bendera tu, Sheria za Hii nchi zinambeba Tajiri.

Ukiwa Maskini huwezi pewa nyundo zote hizo kwa kosa kama hilo,ila ndio Tanzania nchi yetu yenye Amani ya Bendera.
 
Hakimu akitoa hukumu anasemaga iwe Funzo na kwa wengine..

Yani Maskini sisi ndio wakutolewa DEMO wote mkipewa favor sheria itatumika kwa nani?

M/kiti kakosea kisheria kabisa,hoja hapa nadhani ni kwanini Maskini anahukumiwa lakini makosa makubwa zaidi ya hayo Hayatolewi hukumu sawa sawa?

M/kiti ye apambane tu,sheria imetumika na ana haki ya kukata rufaa pia nadhani.
 
Bila Pesa hata sasa hivi umefungua huu uzi unaonekana unapga makelele.

Ukiwa na Pesa kila kitu ni point utachoshauri na kutamka.

nchi yetu hii bila pesa Ni chungu amani utaiona kwenye Bendera tu, Sheria za Hii nchi zinambeba Tajiri.

Ukiwa Maskini huwezi pewa nyundo zote hizo kwa kosa kama hilo,ila ndio Tanzania nchi yetu yenye Amani ya Bendera.
Huyu karudi kuanza kufunika uzi za Bandari ....ni mmoja wa waliotumika kuwashambulia Watanzania. Subiri uone nyuzi kila baada ya dakika tano. na zote ni za kutia hasira na kejeli tu.

Nafikiri ile ID yake nyingine imefungiwa
 
Back
Top Bottom