masopakyindi
Platinum Member
- Jul 5, 2011
- 17,882
- 13,172
Majuzi katika ziara ya Makamu wa Rais Phillipo Mpango huko Mbeya, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya aliorodhesha miradi mingi ambayo serikali iliahidi lakini haijatekelezwa kwa miaka mingi.
Kuna miradi iliahidiwa na Rais Mwinyi na Jakaya Kikwete wakati wa kampeni za urais, lakini utekelezaji ni sifuri.
AHADI NI DENI.
Marais wakati wa kampeni wanaomba kura na kuahidi hewa. Huo ni utapeli wa kisiasa. Wananchi wa Mbeya tunasimama na Mwenyekiti wa CCM Mbeya kuwa Serikali itekeleze ahadi zake. Kinyume cha hivyo wananchi wanakosa imani na serikali.
Katika hili majibu ya Makamu wa Rais Phillipo Mpango yanamuweka Rais Samia katika nafasi ngumu.
Tunataka utekelezaji wa ahadi, hasa za barabara, nothing less.