Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,067
- 994
đź“ŚKituo cha Afya Kinyerezi
🗒️15/5/2024
Mwenyekiti Uwt Mkoa Dar es salaam Mwajabu Rajabu Mbwambo ameungana na Shirika lisilo la kiserikali TAHECO linalojishughulisha na masuala ya Afya na Mazingira chini ya mkurugenzi wake Shabani Maliyatabu na baadhi ya viongozi wa serikali za mitaa, chama na Jumuiya zake. Na kutoa mahitaji kwa mama wajawazito, waliojifungua , watoto wachanga, vifaa vya usafi katika kituo hicho na kupanda miti katika maadhimisho ya siku ya familia dunia.
Mwenyekiti Mwajabu alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo. Alimpongeza Raisi Dr Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha huduma za afya katika mkoa wa Dar es salaam wilaya ya Ilala. Kituo hicho kimepanda hadhi kutoka zahanati na kuwa kituo cha afya. Na kuwa Jengo la Wazazi, na upasuaji. Na huduma zingine.Toka kupanda kuwa kituo cha afya ndani ya miezi miwili wanawake waliojifungua wanakadiriwa kuwa zaidi 100.
Mwenyekiti amepongeza shirika hilo.kwa kuunga mkono Juhudi za Rais Dr Samia na kutoa mahitaji kwa walengwa. Kwa kuwa bado ni kituo kipya mashirika mengine yana hamasishwa kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali.
Uwt imara
Jeshi la mama
Kazi iendele
Uchaguzi Serikali za mitaa 2024