Mwenye taarifa za TAPELI hili tuwasiliane

16/ 06/ 2013
tapeli latafutwa na polisi
tapeli mmoja anayejiita phinias aloyce anatafutwa na polisi kwa tuhuma za kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu hapa kahama.


mwezi mei, 2013 mtu huyo alipitia shule kadhaa hapa kahama na kuwaibia baadhi ya walimu kwa kuwadanganya akidai anatoka kampuni ya nokia ltd na kufanya promosheni ya kuuza simu na vizuia mionzi kwa bei nafuu sana.


aliandikisha majina ya watu na kukusanya fedha kwa ahadi angeleta bidhaa baada ya wiki moja lakini mpaka sasa ameshindwa kutekeleza ahadi aliyotoa.


tapeli huyo ni mwongeaji sana, mnene, mweusi sana, ana kitambi, ana sura ya duara pia anaonekana ni mtu wa heshima kupitia mavazi anayovaa.

tapeli huyo anatafutwa na polisi kwa jalada na: Khm/rb/3445/2013.


yeyote anayemfahamu tapeli huyo atoe taarifa kwenye kituo cha polisi.

wananchi tushirikiane ili kuwanasa matapeli wengi waliopo hapa kahama.


pia unaweza kutoa taarifa za tapeli huyo kupitia namba zifuatazo:


0755 831576 au 0784 821973
 
Jamaa alichukua pesa za advance kwa baadhi ya watu lakini mpaka leo hajaonekana pia simu zake zote amezima.
 
Jamaa alichukua pesa za advance kwa baadhi ya watu lakini hadi leo hajaonekana pia amezima simu zake zote
 
Subiri zamu yako ifike au yawafike ndugu zako wa karibu ndo utajua kuwa 'ajali haina kinga'
 
Jamaa kachukua pesa za advance kwa baadhi ya watu akalala 'mbele' , hadi leo hajaonekana, pia simu zake zote amezima.
 
Wengine tuna nia ya kusaidia kama tungepata taarifa zinazoeleweka.Sasa umeweka jina tu hata picha hakuna,unadhani ataendelea kutumia jina hilo kila mahali atakapoenda.?
Sifa ulizoziainisha hapo zipo so General.Watu wengi mtaani wapo hivyo.Tuambie kitu cha tofauti tumkamate huyu mshenzi.
 
nadhan watanzia tunamambo mengine tunajitakia ktk dunia ya sasa ya counterfeit kila kona njia pekee ya kua salama ni kununua vitu kwa authorized dealers hasa electronic gadgets na vifaa vya umeme!!!
 
Back
Top Bottom