Mwenye Anointing Water kutoka kwa TB Joshua

Mwenye Anointing Water kutoka kwa TB Joshua

Majaribu2013

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
952
Reaction score
1,050
Wadau humu ndani,

Kuna mtu ana maji haya ya baraka toka SCOAN kwa TB Joshua anisaidie kidogo tu? Kuna jambo zito limetanda mbele yangu.

Nakuomba kama unayo unisaidie. Asante.
 
jamani, kwa nini usiamini katika sala zako, maji yaliyoguswa na mtu yanakusaidia nini?jamani hebu lets grow our faith in God and our prayers, tusitegemee hivi vitu vya duniani, mtegemee Mungu wako, piga goti chini, omba

alafu haya majina mnayojipa, kama lako Majaribu2013 sasa si mwaka huo ulikuwa na majaribu sana na yanaendelea, jamaniii
 
$ 80,but mjue Yesu first maji is nothing without faith.Watu wengi upenda vya Mungu lakini awampendi Mungu.Uwezi chezea Yanga ukalipwa Simba hata ukiogea anointing water pipa zima.Bila kumpa Yesu maisha yako hakika utapata shida,Yesu yupo kwa ajili ya watu wenye shida kama wewe.

Umejuaje huyo anayeuliza hamjui Yesu?
 
Tubu na uungame dhambi zako, kiri kwa kinywa chako. Funga hata kwa siku 3, ndani ya huo mfungo wako jitahidi uamke saa 8-9 usiku usali kwa dhati kwa Mungu ninayemwabudu utapata majibu. Muhimu ni dhamira ya dhati na kuamini. Imani yako itakuponya maji ya nini ili hali Mungu wetu anaponya bure. Barikiwa.
 
Umejuaje huyo anayeuliza hamjui Yesu?

Kwa kupata shida na kuulizia anoiting water inaonesha anamjua Yesu kwa jina tu au anamjua lakini afati maandiko yake kwa kweli yake.Maana Bibilia inasema Sisi tukikaa ndani yake na Neno likakaa ndani yetu tutaomba chochote na kitakuwa.
 
Tubu na uungame dhambi zako, kiri kwa kinywa chako. Funga hata kwa siku 3, ndani ya huo mfungo wako jitahidi uamke saa 8-9 usiku usali kwa dhati kwa Mungu ninayemwabudu utapata majibu. Muhimu ni dhamira ya dhati na kuamini. Imani yako itakuponya maji ya nini ili hali Mungu wetu anaponya bure. Barikiwa.

Mgosi saa ntuhu nawakaua hawa wantungwa nkielewa kwa kwei
 
$ 80,but mjue Yesu first maji is nothing without faith.Watu wengi upenda vya Mungu lakini awampendi Mungu.Uwezi chezea Yanga ukalipwa Simba hata ukiogea anointing water pipa zima.Bila kumpa Yesu maisha yako hakika utapata shida,Yesu yupo kwa ajili ya watu wenye shida kama wewe.

mmm kumbe ufalme wa Mungu unauzwa gali...sisi tusio Na pesa inakuwaje....80*24000=192000/-
 
Tubu na uungame dhambi zako, kili kwa kinywa chako. Funga hata kwa siku 3 ndani ya huo mfungo wako jitahidi uamke saa 8-9 usiku usali kwa dhati kwa mungu ninayemwabudu majibu utapata. Muhimu ni dhamira ya dhati na kuamini. Imani yako itakuponya maji ya nini ili hali mungu wetu anaponya bure. Barikiwa

Acheni kujidai mnajua sana kuliko wengine! Shida ya wabongo tunajiona tunajua mno kuliko wengine. Ona kama wewe waajabu kabisa eti amka saa 8-9 omba. Pooorsheratu. Kama hujui masuala ya viwango vya rohoni nyamaza tu.
 
Kwa kupata shida na kuulizia anoiting water inaonesha anamjua Yesu kwa jina tu au anamjua lakini afati maandiko yake kwa kweli yake.Maana Bibilia inasema Sisi tukikaa ndani yake na Neno likakaa ndani yetu tutaomba chochote na kitakuwa.

Tatizo mnajiona mnajua kila kitu. Aibu sana hii kwetu wabongo. Hujui hata viwango vya roho. Hujui kuwa Mungu anagawa kwa kadri ya kipawa cha mtu. Hujui hata kuwa wengine wanakarama za uponyaji, neno la maarifa, n.k unataka kila mtu awe same standard halafu unadundisha tumbo hapa kutype type ujinga wako nyooooo! Nyamaza kabisa kama hujui gospel vizuri sheratoni wewe!
 
Nenda mwenyewe BWM Tower, usitume watu pale. Nje kuna wahuni na maji yao, usiojua unaingia chaka.
 
Kama una mwamini Mungu kweli..basi omba atakusikia na atakujibu... Kumbuka mawazo ya Mungu si ya mwanadamu,,, Mungu anaweza kukujibu kwa namna ambayo yawezekana hata usigundue ukaona ni kawaida tu....

Hayo maji ya hao wanaojiita watumishi wa Mungu ni mtego tu, ukitumia ndio umejifunga, kila atakachosema wewe utaona sawa tu...
Mpendwa, Mungu alisema "Ombeni nanyi mtapewa, bisheni nanyi mtafunguliwa" hakika sikio la Mungu si zito... Omba kwa imani na hutaona tena haja ya hayo maji.
 
Back
Top Bottom