Inaitwa Decceleration lane kama unatoka barabara kuu kuingia pembeni. Acceleration lane ni ile unapotoka pembeni kuingia njia kuu.Inaitwa "Acceleration lane". Kwenye hii barabara ya Mwenge -Tegeta nadhani nimeziona mbili tu, pale junction ya Africana na inapoishia barabara kule Tegeta.
Kosa liliopo ni kuwa hakuna service road ambayo mtu unatakiwa uchepuke unapokaribia njia ya kuingi nyumbani si upite mbele ukageuze!Nimekuelewa sana ndugu. Na Sio kilometa 3 tu unaweza kwenda hadi kilometa tano na kwako unapaona pale lakini lazima uzunguke ndio uweze kuingia mtaa wako. Sasa wa tz Kila kona mtu anataka aingie apendavyo yeye. Watu wanashindwa kutofautishga high ways na barabara za mitaani. Serikali itilie mkazo watu wakasome udereva na sheria za barabarani
Hahhahaaaa.....swali zuriwaziri alikuwa nani?
Joniwaziri alikuwa nani?
Uturn kweli ni pale unapogeuza kuelekea mwenge,we umetoa mfano kama unashuka kwenda rainbow, mfano huo huo unatokea lugalo ila unataka kwenda pale NBC tawi la mbezi beach utafanyaje kama sio ku uturn?? Na alama hio ya uturn ndo zimekuwa crossed, Je mtu akageukie wapi
Kama unataka kwenda NBC, unapaswa kuingia njia ya kwenda rainbow, geuza petrol station ya Puma (zamani Bp) alafu rudi tena barabara ya kuelekea mwenge.
Mmekatazwa kupiga u turn sababu barabara ni ndogo sana...gari ikiwa kubwa kidogo inaweza kushindwa ku negotiate ile kona
Watanzania bana, kila mtu ni mtaalamu wa kila kitu. Si ajabu mleta uzi unaweza kuwa mtaalamu wa linguistics lkn unakosoa design na construction ya barabara!!!Kwa kweli inasikitisha sana kuhusu mtaalamu aliye chora na kupitisha ramani ya barabara inayoanzia mwenge mpaka Tegeta. Wengi wa watumiaji tunapata taabu sana tunapotaka kuingia barabara za pembezoni.
Mara nyingi tumejikuta tukiwa katika hatari ya kugongwa kwa nyuma ya magari yetu kwa ukosefu wa maeneo ya kuwapisha wenzetu wanaotakiwa kwenda moja kwa moja.
Mfano mzuri ni pale Tangi Bovu kama unatoka mjini na unataka kuingia upande wa kulia yaani Ally Sykes road au anayetoka barabara hiyo na kutaka kuelekea Tegeta wote hao wanakuwa katika hatari ya kupata ajali.
Tunaomba mamlaka husika kabla ya kuipokea barabara hii watoe ushauri na maagizo ya kufanyiwa marekebisho sehemu zote hizo ili ionekane tuna wataalamu wanaojenga barabara za karne hii.
Ahh yess ile service road pale...Pale unatakiwa upige L turn yaani ukipiga kona kulia hakikisha umetoka mpaka service road iliyopo nje tu ya ofisi ya Tanesco Mbezi Beach/Imalaseko supermarket ya zamani then ndiyo upinde tena kuelekea Mwenge ukiwa Service road utaendelea mbele mpaka ufike NBC Bank