kwani mzee wa kaya hajafunguka tu kuhusu ugeni huo?
Nikiteuliwa kuwa boss kazini nitakwenda kumtembelea rais,kama icc ilivyo fanya.
Eeh, huyu jamaa sidhani kama kasomea sheria kweli, maana hata kutoa argument hajui-Kwa hiyo moja kati ya majukumu yake ni kutembelea nchi na kusalimia mara tu baada ya kuteuliwa!?
Hata mimi nadhani hii mahakama ni mtambo mwingine wa ku-process rushwa.Hii mahakama ya sijui ICC ama ICTR ni kupoteza muda na pesa za walipa kodi tu. Hakuna jipya hapo Arusha zaidi ya kuchezea pesa za watu na muda
....Gazeti hili lilipomtafuta Jaji Werema kuzungumzia ujio wa Bensouda alisema kuwa Mwendesha Mashtaka huyo alikuwa mgeni wa Rais Kikwete, hivyo hawezi kueleza kilichozungumzwa.
Alikuwa mgeni wa Rais, lakini kubwa nililolisikia ni kwamba alikuja kusalimia kwa sababu tangu alipoteuliwa hakuwahi kuja Tanzania, alisema Werema.
Kama ilivyokuwa kwa Werema, naye Feleshi alikwepa kuzungumzia ujio huo wa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa ICC, huku akisema jambo hilo linaweza kutolewa ufafanuzi na Ikulu.......
source: mwananchi gazeti
Alikuwa mgeni wa Rais, lakini kubwa nililolisikia ni kwamba alikuja kusalimia kwa sababu tangu alipoteuliwa hakuwahi kuja Tanzania, alisema Werema.