Mwanza: Wazazi wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Thaqaafa waandamana kudai matokeo ya watoto wao

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
FoQyh_4WcAEekFp.jpg
Wazazi wa watoto waliokuwa wanasoma katika shule ya sekondari Thaqaafa iliyopo wilayani Nyamagana jijini Mwanza wameandamana kudai matokeo ya watoto wao waliomaliza kidato cha nne 2022 kufuatia kuwepo kwa sintofahamu.

Thaqafa.jpg
Wazazi hao wamesema wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka jana katika shule hiyo walikuwa 164 matokeo ya mtihani yametoka ya wanafunzi 22 pekee wengine matokeo yao hayajulikani yalipo.

‘Hatujui Watoto wetu tunawapeleka wapi tunamlilia Rais wetu Samia Suluhu huko aliko atuangalie kwa hii shule ya Thaqafa sisi wengine ni wajane tunahangaika na Watoto wetu wa kike tunawapeleka wapi sisi Watoto hawa"

Afisa Elimu sekondari wa halmashauri ya jiji la Mwanza Allan Said amefika katika shuel hiyo na kuzungumza na wazazi wa wanafunzi hao na kuwataka kufuata taratibu zote za madai yao.

"Serikali inafanya kazi kwa kutumia makaratasi wewe ukisema mimi mtoto wangu amefutiwa utalizwa Ushahidi uko wapi nyie chukueni barua muende nazo mkaulize vizuri kuhusu hayo matokeo ya Watoto wenu."

Chanzo: EATV

====

UFAFANUZI WATOLEWA
Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Allan Said amesema “Matokeo ya Wanafunzi hao yamefutwa na chanzo ni udanganyifu wa matokeo, kuna barua mbazo zinaeleza wazi sababu ya matokeo yao kufutwa zilizoelekezwa kwa wazazi lakini wakakataa kuzipokea.

“Udanganyifu uliobainika ni katika majibu, mfano kuna maswali ambayo kila mwanafunzi alijibu tofauti, lakini baadaye wakaanza kukata na kjibu majibu ya aina moja, hiyo pekee inaonesha kulikuwa na mawasiliano na ndio maana wakafuta na kuandika majibu sawa.

“Huo ni uchunguzi wa awali, shule au uongozi wa shule wenyewe haujapata adhabu nyingine yoyote lakini kama ikibainika wamehusika kwa lolote nao watachukuliwa hatua kulingana na ukubwa wa kosa.

“Hatma ya Wanafunzi waliofutiwa mitihani wanaweza kuamua kujisajili tena wakiwa ‘private candidates’ na usajili bado unaendelea na unaisha mwezi huu wa pili (2023), akifaulu anapata haki sawa kama yule ambaye amefauu kawaida."
 
WANAANDAMANA WANAMUANDAMANIA NANI..? NANI KAWADANGANYA KULALAMIKA KUTAWAFICHIA MAKOSA YA UDANGANYIFU WA MITIHANI WA WATOTO?
 
Udanganyifu uliobainika ni katika majibu, mfano kuna maswali ambayo kila mwanafunzi alijibu tofauti, lakini baadaye wakaanza kukata na kjibu majibu ya aina moja, hiyo pekee inaonesha kulikuwa na mawasiliano na ndio maana wakafuta na kuandika majibu sawa.
Hii kauli utaipingana nayo kweli jamani. Haiwezekani majibu yakafanana ujue
 
Mamaee zao wanangu wanasoma pale sijui itakuwaje academically wapo sawa mmmmh ngoja tuone
 
Wazazi wa watoto waliokuwa wanasoma katika shule ya sekondari Thaqaafa iliyopo wilayani Nyamagana jijini Mwanza wameandamana kudai matokeo ya watoto wao waliomaliza kidato cha nne 2022 kufuatia kuwepo kwa sintofahamu.

Wazazi hao wamesema wanafunzi waliomaliza kidato cha nne mwaka jana katika shule hiyo walikuwa 164 matokeo ya mtihani yametoka ya wanafunzi 22 pekee wengine matokeo yao hayajulikani yalipo.

‘Hatujui Watoto wetu tunawapeleka wapi tunamlilia Rais wetu Samia Suluhu huko aliko atuangalie kwa hii shule ya Thaqafa sisi wengine ni wajane tunahangaika na Watoto wetu wa kike tunawapeleka wapi sisi Watoto hawa"

Afisa Elimu sekondari wa halmashauri ya jiji la Mwanza Allan Said amefika katika shuel hiyo na kuzungumza na wazazi wa wanafunzi hao na kuwataka kufuata taratibu zote za madai yao.

"Serikali inafanya kazi kwa kutumia makaratasi wewe ukisema mimi mtoto wangu amefutiwa utalizwa Ushahidi uko wapi nyie chukueni barua muende nazo mkaulize vizuri kuhusu hayo matokeo ya Watoto wenu."

Chanzo: EATV

====

UFAFANUZI WATOLEWA
Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Allan Said amesema “Matokeo ya Wanafunzi hao yamefutwa na chanzo ni udanganyifu wa matokeo, kuna barua mbazo zinaeleza wazi sababu ya matokeo yao kufutwa zilizoelekezwa kwa wazazi lakini wakakataa kuzipokea.

“Udanganyifu uliobainika ni katika majibu, mfano kuna maswali ambayo kila mwanafunzi alijibu tofauti, lakini baadaye wakaanza kukata na kjibu majibu ya aina moja, hiyo pekee inaonesha kulikuwa na mawasiliano na ndio maana wakafuta na kuandika majibu sawa.

“Huo ni uchunguzi wa awali, shule au uongozi wa shule wenyewe haujapata adhabu nyingine yoyote lakini kama ikibainika wamehusika kwa lolote nao watachukuliwa hatua kulingana na ukubwa wa kosa.

“Hatma ya Wanafunzi waliofutiwa mitihani wanaweza kuamua kujisajili tena wakiwa ‘private candidates’ na usajili bado unaendelea na unaisha mwezi huu wa pili (2023), akifaulu anapata haki sawa kama yule ambaye amefauu kawaida."
Shule yangu
Nilikuwa hapa 2010-2012 wakati huo ilikuwa ni moja ya shule bora sana kwa mwanza.
Imekutwa na nini tena. Wanafunzi waliandaliwa vizuri sana wakati huo. Mpaka ukanyage kidato cha nne ulipaswa kuwa umeivaa vizuri
 
Back
Top Bottom