Ndio shida ipo hapo, hata hawa ilemela tunaowasifia wamefeli kwa hili, yaani recreational Parks zetu tunawaza beach tu, kusingekuwa na ziwa ingekuwa je?
Kila eneo wazi tunawaza kupima viwanja watu wajenge basi kwisha.
Ilemela wangeweza tenga hata eneo kwa ajili ya CBD yao hakuna mtu kujenga unless ni ghorofa 10 kwenda juu, makampuni au mashirika au watu binafsi wakija kujenga maghorofa wanakuta viwanja vipo sio mpaka ulipe watu fidia.
Kuwe na recreational parks kila kata.
Kumiliki gari sasa hivi sio Big deal wanapopima viwanja wakumbuke kupima barabara ziwe kubwa na ziwe na njia za train, tram, brt nk baadae mji utakuwa mkubwa huu usafiri wa vipanya na mabasi hautafaa tutahitaji treni, wawaite trc wsone ni wapi panafaa kupita reli ili wslinde hayo maeneo.
Mfano inahitajika inayotoka nyegezi au buhongwa ije stendi ya Nyamhongolo mpaka airport.
Hii treni inaweza kuwa leta mjini kati watu wa pembezoni kwa kuunganisha na hii sgr inayojengwa sasa.
Maeneo mengine kama ni mazuri kwa kilimo si lazima vipimwe viwanja kisa mji unapanuka tutakosa sehemu za kulima baadae, watu wakajenge hata Magu huko tulinde baadhi ya maeneo kwa kilimo.