Mwanza barabara kikwazo (Ilemela imekithiri)

Mwanza barabara kikwazo (Ilemela imekithiri)

Nafikiri si vizuri kusema huo ni msaada wakati serikali inalipa, pili Kama uko mza nakushauri uende ofisi husika uwaulize nafikiri huko utapata majibu.
Kipaumbele sio barabara tu za lami kumbuka kuna barabara za vumbi nyingi ambazo pia hutumia pesa nyingi kuzi maintain, kama tunahisi tunaibiwa hao tuliowapa dhamana ya pesa zetu leo hii wangekuwa matajiri sana...
 
Ilemela ndio hakuna kitu kabisa, heri Nyamagana kama ni mbunge basi Mabula Kijana is far better than Mrs Mabula
Mabula kijana ndo kituko
Mi niko Nyamagana...barabara za mitaa ambazo ndo daizi yake kabisa ziko hoi.mnooo....hebu nenda kajionee barabara inayopita lango la stendi mpya na kushuka kwa Masai...imegeuka na kuwa mto...
Mabula kijana ndo hapana kabisa aiseee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mabula kijana ndo kituko
Mi niko Nyamagana...barabara za mitaa ambazo ndo daizi yake kabisa ziko hoi.mnooo....hebu nenda kajionee barabara inayopita lango la stendi mpya na kushuka kwa Masai...imegeuka na kuwa mto...
Mabula kijana ndo hapana kabisa aiseee

Sent using Jamii Forums mobile app
Stendi mpya ipi?
 
Wakuu hata kama sio kwa pesa za ndani ni pesa za wafadhili Ilemela kwa mwaka ulioisha imejenga Km 12 za barabara kwa kiwango cha lami. Sabasaba-Buswelu, Mjimwema-Big bite, Nera-Kigoto/ Mwaloni.

"Hatua hii imetokana na usimamizi mzuri wa miradi ya TSCP ambapo wafadhili wamekuwa wakiridhika na kuendelea kutoa fedha kila mwaka. Mpango ujao ni kujenga kwa kiwango cha lami barabara za Kahama – Kabusungu – Kayenze, Mbogamboga – Nyamadoke – Nyamhongolo, Buswelu – Cocacola na Pasiansi – Lumala – Kiseke. Tayari maandiko ya miradi hiyo yanaendelea kufanyiwa kazi na mradi wa TSCP."

Sipo kusifia kila kitu, ila ni bora kidogo kuliko kukosa kabisa, Tujiandae kwa miradi ijayo barabara za Kahama – Kabusungu – Kayenze, Mbogamboga – Nyamadoke – Nyamhongolo, Buswelu – Cocacola na Pasiansi – Lumala – Kiseke.

http://www.ilemelamc.go.tz/storage/app/uploads/public/5d7/8b0/f04/5d78b0f046dc6745412498.pdf

ILEMELA ni yetu, tushirikiane kuijenga.
Ilemela iko vizuri mno...vituko viko Nyamagana...hakuna kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
fafanua mkuu baada ya kumegwa kutoka jiji 2010/2011, ilemela imejenga barabara ipi kwa lami ukiacha ile ya ufadhili wa WB, kiseke Buswelu, na Ile ya Buswelu-Veta,

Manispaa gani mitaa kama vijiji; give us a break aiseee

Ilemela iko vizuri mno...vituko viko Nyamagana...hakuna kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Manispaa gani hata kujenga barabara kilomita 3 kila mwaka wa fedha haijengi? KODI ZETUTUNAZIDAI, tumedai risiti ila tunaona tunajaza dashboards zetu na risiti za EFD wakati maendeleo kama barabara ni vumbi na sampo zinakufa tu, tungejenga kilomita 3x10years tungekuwa na kilomita 30 zetu, wafadhili 12Km , jumla 42KM hata mfadhili anakuwa na adabu
 
Mlipopewa IMC mlipaswa kuandikia Serikali KUU ilete pesa za Barabara IMC, za kama kilomita 100 hivi kisha mkazigawa kwenye barabara zenu za mitaa, kusema hii ni manispaa yaani kuiunda hata serikali kuu inapaswa kuwa imejiandaa, manispaa huku mitaa ni vijiji. HAIWEZEKANI. kilomita 100 za lami, bi bei gani? kilomita moja ni 300-1000 millionTZS au?
 
hadhi ipande ama iundwe kwa uwepo wa huduma, na anayepandisha awe amejiandaa sio kuita tu jiji au manispaa wakati tope tupu wakati wa mvua, au vumbi tupu wakati wa kiangazi najua afya maji umeme usafiri-nauli, mawasiliano-airtimes, barabara 40TZS per litre of fuel tunalipia wananchi directly. sasa kodi zetu zinaenda wapi? ndio nauliza tunalipa kodi za kulipana posho?
 
fafanua mkuu baada ya kumegwa kutoka jiji 2010/2011, ilemela imejenga barabara ipi kwa lami ukiacha ile ya ufadhili wa WB, kiseke Buswelu, na Ile ya Buswelu-Veta,

Manispaa gani mitaa kama vijiji; give us a break aiseee
Hivi zile za kiloleli,maduka tisa,mjimwema si ni za ilemela na zenyewe.... Sababu niliondoka hiyo miaka ya 2010-11 hazikuwepo ila nilivyorudi nikazikuta.
 
Kipaumbele ni Hospital ya Wilaya iliyopo Kabusungu na kuunganisha Kayenze na Halmashauri kwa njia ya lami.

Na hii ya AIRPORT-TX-IGOMBE kwenye huo mpango mbona haimo au kwenye mipango mingine tofauti na ufadhili wa world Bank imewekwa?
 
Sisi tulio huku milimani tunatumia vizuri resource ya mawe, nyie subirini lami tu😆😆😆😆
 
Mlipopewa IMC mlipaswa kuandikia Serikali KUU ilete pesa za Barabara IMC, za
Hivi zile za kiloleli,maduka tisa,mjimwema si ni za ilemela na zenyewe.... Sababu niliondoka hiyo miaka ya 2010-11 hazikuwepo ila nilivyorudi nikazikuta.
Huko kote ni ilemela, hata mecco, buzuruga, maeneo yote ya kirumba, mwaloni, bwiru, malaika, airport hiyo yote ni ilemela,
Mkuu hata hivyo tumetoka mbali, hadi mkapa a naingia madarakani 1995 kulikuwa na lami mza mjini to kona ya bwiru, barabara ya machemba na barabara chache sana pale mjini kati jumla zilikuwa hazifiki hata 10km.
But sasa hivi ukichukua ilemela na nyamagana kuna zaidi ya 100km,
Barabara zote zilizotajwa ziko pembezoni mwa mji,
 
Cuba na Fidel Castro walitufunza mapema sana kuwa cha muhimu kukuza uchumi ni kufungua nchi na maeneo yake kwa lami, najua kuna ni mahitaji mengi japo mengine yote ya muhimu tunalipia wananchi wenyeewe tofauti na kodi, kama umeme. maji afya (elimu serikali kuu inaleta pesa zake), sasa baada ya hayo mahitaji muhimu, pesa zinaenda wapi kiasi tusijenge bararbara za lami kwa pesa zetu za ndani, out 45Bilions yaa tunakosa hata lami km 10? why?

Lile jadwari halioneshi pesa imetumika kwenye maeneo yapi, ni makisio mapato na matumizi in jumlajula, je matumizi ni jumla ya nini? POSHO, MAFUTA YA GARI, VIYOYOZI-Umeme tuuu?

Njua ujenzi wa vituo vya afya, hospitali za wilaya au zahanati JPM(mungu ampe maisha marefu) anatoa pesa serikali KUU, hii yetu inatumia.


Naona wameangalia kipaumbele kwa sababu inaenda Hospital ya wilaya
 
IJUMAA KUU, Mfufuka afufuke na barabara za ILEMELA/NYAMAGANA
 
Kesho saa tatu kamili Usiku Mbunge wa Jimbo la Ilemela Bi. Angeline Mabulla atakuwa ITV kuongelea suala la maendeleo jimboni, Changamoto, mipango na mafanikio. Tumsikilize ndio tuhukumu. Asanteni.
 
Back
Top Bottom