iArmaniAdamson
JF-Expert Member
- Jun 15, 2015
- 944
- 287
1. Kwa hiyo la kuongeza kata huko Kyela ni demokrasia safi?
2. Na hu ugaidi uliotokea Tume imeuona au kuugundua baada ya kutangaza matokeo kwa siku 3? Huo ugaidi kama ulionekana siku ya uchaguzi na kuripotiwa na hao waangalizi au wawakilishi wa vyama vilivyoonewa, kwa nini tume iliendelea na mchakato wa kutangaza matokeo?
3. Nitajie ugaidi huo na jinsi ulivyomwathiri Mzanzibari katika kupiga kura ya Zanzibar pekee na si kura ya Muungano. Au ndiyo ile tumesikia ya kupika nyama ya kuku na kitimoto pamoja halafu unamkaribisha msabato au muislam na kumwambia achambue nyama ya kuku ale aachane na nyama ya kitimoto kwenye sahani moja?
ningependa uchukue nafasi usome tamko la UVCCM walilolitoa asubuhi hii kuhusu mchakato wa uchaguzi Zanzibar, pia chukua muda usome tamko la kuvunja uchaguzi uliotolewa na ZEC. Utapata picha kamili ya nini kilikuwa kinaendelea uchaguzi wa Zanzibar, tangu awamu za awali za kutafuta mzabuni wa kuchapisha karatasi za kura, watu kupiga, kuzuiwa kupiga kura, kujidhihirisha u CUF ndani ya tume, wahesabu kura kujidhihirisha kuwa ni wana CUF. process nzima ilikuwa imepenyezwa na watu wa ndani ya CUF...