mwamajinja mapunga
JF-Expert Member
- Dec 23, 2014
- 1,074
- 607
Katika uzinduzi wa kampeni za CHADEMA/UKAWA uliofanyika tar. 5/9/2015 Kyela mjini maeneo ya viwanja vya mchaga Kyela wenyewe huviita viwanja vya SUGU... Ambapo Wananchi wa Kyela walimpokea shujaa wao na tegemeo kijana makini ndg Abraham Mwanyamaki kwa nderemo na vifijo, shamra shamra za ngoma, madereva wa bodaboda wanaomuunga mkono na wananchi wengi walio na wasio na vyama.....mgombea aliambatana na ndg. JOSEPH MBILINYI (MB) A.K.A SUGU AU RAIS WA MBEYA, pIA NA MWANDISHI MAHIRI WA GAZETI LA MWANAHALISI NDG SAED KUBENEA... ambapo mheshimiwa Sugu alimnanga mwakyembe kwa unafiki, uzandiki na mambo ya kutunga kwa wananchi, pia alisikitika kuona kyela vumbi linatimka kila mahali ni aibu kwa mbunge,,,,akafuatia saed kubenea ambaye alitoa nyaraka ambazo ziliandikwa na dr. mwakyembe kwa jeshi la polisi kuwa anafuatiliwa na watu wanataka kumuua, akaongeza kuwa dr. mwakyembe hana legacy ya kuongelea RICHMOND Hata kidogo na akasisitiza kuita press conference kuongea kilicho moyoni na na kusema uongo wa dr. mwakyembe alichokisema ni uongo kwa kuwahadaa watz, pia akagusia mabehewa feki ya mwakyembe, n.k