Mwandishi wa Makala

Mwandishi wa Makala

Mwandishi wa Makala – 12

Nilivuta droo yangu chini ya meza kuifungua. Nilikuwa na tabia ya kukusanya na kununua vitu mbalimbali vya kihistoria katika maduka ya vitu ya kale kila nilipokuwa kwenye safari zangu mbalimbali. Watu wengi walinishangaa kwanini nilinunua vitu vya kale, wao hupenda kununua vitu vyao kutoka kwenye maeneo yanayouza vitu vya kitalii, huku mimi nikinunua walichoona ni takataka kutoka maduka ya vitu vya kale.

Nilikumbuka kwamba katika moja ya safari zangu kadhaa mwaka mmoja na nusu nyuma, nilinunua pete mbili na vitu vingine vya kitamaduni. Nilipata bangili nzuri yenye mawe ya kijani na pete ya fedha. Kisha, pale katika lile duka la kwenye kona, nilinunua kile ambacho nilikuwa nakitafuta kwenye droo muda huo.

Ilikuwa ni pete ya dhahabu ambayo ilikuwa na jiwe la zambarau. Niliipata na kuitoa kwenye droo, nikaishika katika mkono wangu.

“Ninayo pete niliyoinunua katika duka moja la vitu vya kale nilipotembelea Musoma mwaka mmoja na nusu uliopita kabla sijapata safari ya Amboni. Lakini Musoma ni eneo tofauti na mbali kutoka ulikokuwa wewe. Sijui inaweza kufanana na pete yako?”

“Ooh Bwana mkubwa, sitaki kukutisha tena. Lakini ningependa sana kuiona, sijui unaweza kunirushi niione?”

Sikutaka kubishana naye, nilifanya kama alivyotaka, nikairusha ile pete kwenye vile vivuli juu ya sofa.

“Aisee, umeipata! Ndiyo hii!” Yule mgeni alipiga kelele.

Nilipokuwa nataka kumuuliza yule mgeni kuwa alijuaje kuwa ile ndio ilikuwa pete yake muda huohuo dirisha la studio yangu likafunguka kwa kishindo kutokana na upepo mkali. Nilikurupuka kuzinyakua karatasi zangu zilizokuwa juu ya meza kutokana na upepo uliozipeperusha na kusambaa sakafuni. Nilipoinua macho yangu kuangalia juu, Nilipigwa butwaa, nilimuona mdada mrembo kwelikweli ambaye sijapata kumuona wa mfano wake katika dunia hii.

Alikuwa mwembamba lakini akiwa na umbile lililovutia mno. Mrefu kiasi mwenye urefu wa futi tano na inchi tisa. Kwa yeyote awaye mwanaume rijali hapana shaka kama angemuona angekiri kuwa mwanadada huyo alikuwa ni moto wa kuotea mbali na hakuwa na mfano wake.

Kwa mlingano wa macho tu, mdada huyo alitoa tafsiri ya kuwa na ule uzuri usiomithilika, uzuri uwezao kumliwaza, kumpumbaza na hata kumlaza kitandani mtu yeyote aliye timamu.

Alikuwa na uchotara wa Kidigo na Kingazija uliomfanya aonekane kama ni mmoja kati ya wasichana wachache ambao walishushwa kimakosa hapa duniani kwa kuwa walikusudiwa kuumbwa malaika!

Nywele zake zilikuwa nyeusi tii zilizotumwa vema sambamba na sura yake yenye mvuto wa asilimia mia moja. Nyusi na kope zake zilikuwa ndefu zilizong’ara na kuyafanya macho yake yawe wazi nusu.

Pua yake ilikuwa ndefu kiasi, nyoofu ya wastani iliyoiacha midomo yake ijidai kwa kuhifadhi meno meupe yaliyojipanga vizuri huku yakiachia kijiuwazi kidogo kwa mbele. Alikuwa mweupe lakini si ule weupe wa mkorogo bali weupe wa asili wenye ung’avu wa kuteleza.

Uzuri wake haukuishia hapo, alikuwa na shingo nzuri iliyokaa vyema katikati ya mabega yake ya kike mazuri, nilijikuta natatamani kumkumbatia. Kifua chake kilibeba matiti ya wastani yaliyochongoka mbele na yenye hasira ya kutoboa gauni alilovaa. Tumbo lake lilikuwa flati na kiuno chake kilikuwa chembamba mithili ya dondola.

Kwa kweli alikuwa mrembo wa asili aliyekolea kiasi kwamba nilijikuta nikikubaliana na wale wanaosema kuwa wapo wasichana walioumbwa Malaika lakini wakashushwa kimakosa hapa duniani!.

“Hujambo mpenzi wangu,” mdada huyo mrembo alimsabahi mgeni wangu kwenye kiza huku akiachia tabasamu.

Muda huohuo vile vivuli katika upande wa pili wa chumba vikaanza kuhama taratibu, kisha akatokea kijana mtanashati. Katika macho yake yalionekana machozi ya mtu mwenye shukrani za pekee. Akanyoosha mikono yake na kumsogelea yule mdada mrembo ambayue muda huo alikuwa amesimama mbele ya meza yangu ya kompyuta.

Nikajikuta nikistaajabu sana huku nikimtazama yule mgeni wangu. Kumbe alikuwa ni kijana mtanashati sana na kwa kumwangalia tu niliweza kubaini kuwa alikuwa na miaka therathini na tano hivi, mrefu na mwenye umbo kakamavu lililofanana na wachezaji wa ligi ya mpira wa kikapu.

Yule kijana mtanashati alitembea kwa mbwembwe na kumsogelea yule mdada mrembo.

“Tunu?” yule kijana mtanashati aliuliza kwa mshangao. “Ni wewe Tunu wangu?”

“Ndiyo,” mdada mrembo alijibu na kuongeza. “Ni wakati muafaka sana mfalme wangu. Najua umeteseka sana kwa muda mrefu, sasa sogea na ushike mkono wangu na uniruhusu nikuongoze twende upande wa pili. Njoo mpenzi wangu na uwe nami milele.”

“Tunu wangu, malkia wangu,” yule kijana mtanashati alisema.

“Ndiyo mfalme,” mdada mrembo alijibu. “Ni wakati wa wewe kuja nyumbani.”

“Shhhh,” yule kijana mtanashati alisema huku akiweka mkono wake kwenye kiuno chembamba cha Tunu na kumtazama kwa makini usoni.

“Tunu, sasa ninathibitisha kutimiza kiapo yangu… kiapo ambacho nilikiweka kwa jina la baba yangu na nafsi ya mama yangu.”

Wakabaki kimya wakitazamana huku tabasamu likiwa limechanua kwenye nyuso zao. Chumba chote kikawa kimya. Niliendelea kuketi palepale huku nikisubiri kuona nini kitaendelea, machozi yalianza kunilenga kwenye macho yangu.

“Nakupenda Tunu,” yule kijana mtanashati alisema huku akimkazia macho yule mdada mrembo. “Malkia wangu, nakupenda sana zaidi ya maisha yenyewe.”

Baada ya kutamka maneno hayo kwa Tunu yule kijana mtanashati alianza kulia kilio cha kwikwi, mbele ya mwanamke wa maisha yake. Aliinamisha kichwa chake mbele ili kujiegesha kwenye bega la mdada mrembo.

“Nakupenda pia mfalme wangu,” mdada mrembo alisema huku akimkazia macho yule kijana mtanashati. “Sasa ni wakati wa sisi kwenda nyumbani.”

Niliendelea kuyashuhudia yote hayo nikiwa nimeketi katika kiti changu cha kuzunguka, nikawaona wakishikana vizuri kwa upendo na kuanza kuelea juu ya chumba. Walianza kuondoka taratibu na walipokaribia kwenye dirisha la studio, yule kijana mtanashati aligeuka kuniangalia. Akaachia tabasamu.

“Mheshimiwa, asante kwa ushirikiano wako, ni wakati wako sasa kuandaa hatima yako. Hapa kazi yako imekwisha!” Kijana mtanashati alisema na kuitazama ile pete aliyokuwa ameishika mkononi kwa tabasamu, kisha akawa anataka kuivaa kwenye kidole.

“Subiri kwanza,” nilipiga kelele nikijaribu kumzuia yule kijana mtanashati asiivae ile pete huku nikiinuka haraka kutoka kwenye kiti changu na kumkabili. Yule kijana mtanashati akanitazama kwa mshangao.

“Subiri kwanza,” nilipiga kelele nikijaribu kumzuia yule kijana mtanashati asiivae ile pete huku nikiinuka haraka kutoka kwenye kiti changu na kumkabili. Yule kijana mtanashati akanitazama kwa mshangao.

“Unaondokaje na pete yangu? Si umeshampata Tunu wako, nirudishie pete yangu!” Nilimwambia yule kijana mtanashati huku nikimnyang’anya ile pete. Sikujua ujasiri wa kumnyang’anya ile pete niliutoa wapi!

Yule kijana mtanashati alibadilika ghafla na kunitazama kwa macho yenye ghadhabu. Macho yake yalitoa miale kama umeme na kunipata kwenye uso wangu, nikapigwa shoti ya umeme na kuanguka kwa kishindo kikubwa huku nikipiga kisogo changu sakafuni.

Itaendelea…
 
Mwandishi wa Makala – 13

Yule kijana mtanashati alibadilika ghafla na kunitazama kwa macho yenye ghadhabu. Macho yake yalitoa miale kama umeme na kunipata kwenye uso wangu, nikapigwa shoti ya umeme na kuanguka kwa kishindo kikubwa huku nikipiga kisogo changu sakafuni.

Muda huohuo ukungu ukatanda tena ndani ya studio yangu ingawa niliniweza kuona japo kwa shida, na hapo hapo zikafuata sauti kali za vicheko vikubwa vilivyopenya vyema ndani ya ngoma ya masikio yangu. Sikuweza kuona kiumbe chochote zaidi ya zile sauti zilizoendelea kujirudia rudia, tena kwa kitisho maradufu.

Nilijikuta naogopa sana nikiwa hapo sakafuni nilipoanguka, na mara nikastukia nazabwa kibao na mtu ambaye sikumuona. Nilikodoa macho yangu kuangaza kila upande lakini sikuweza kuona kitu chochote. Mara wakajitokeza fisi wawili, jike na dume, wakawa wananitazama kwa macho makali yaliyowaka kama moto kwa ghadhabu.

Wale fisi wawili wakanisogelea na kuchutama pembeni yangu, wakawa wananiangalia kwa macho yenye uchu wa nyama kana kwamba wameona mzoga, walionekana kama walitaka kunitafuna mwili wangu mzima mzima.

Niliogopa sana na kuanza kutetemeka huku nikirudi nyuma kwa woga, hasa pale iliponijia ile picha ya awali ya mwili wangu kucharangwa na kisha kuungua na moto, na tukio la kushambuliwa na mbwa mwitu waliokuwa na hasira. Nilipotaka kurudi nyuma zaidi nilishindwa kwa kuwa nilikuwa nimefika ukingoni mwa chumba.

Wale fisi wakanisogelea tena na kuchutama pembeni yangu huku wakiendelea kunikodolea macho kwa uchu. Nikabaki nimeyakodoa macho yangu kwa hofu huku nikijaribu kuwatazama kwa makini zaidi, nilijitahidi kuwakodolea macho ili kuwafanya waogope na wasiweze kunishambulia na kunisababishia majeraha.

Wale fisi walinitazama kwa makini wakaonekana kama vile wameyasoma mawazo yangu, walitazamana kisha wakaanza kunicheka kwa sauti kubwa iliyotisha. Kutahamaki nikazabwa kofi la pili lililonifanya kuanza kuona vimulimuli mbele ya macho yangu, na hapo hapo kengele ya hatari ikalia akilini mwangu.

Nikaona nikijilegeza nitaumia, hivyo nilijivika ujasiri na kuinuka haraka pale sakafuni, lakini nikahisi kizunguzungu kilichofuatiwa na kuanguka tena sakafuni, nikaanza kuhisi fahamu zangu zinaanza kunipotea.

Sikukubali kupoteza fahamu zangu katika mazingira yale kwa hofu ya kuwapa nafasi wale fisi ya kunishambulia, nikazidi kuyakodoa macho yangu, mara nikawawaona wale fisi wakisimama huku wanaendelea kucheka sana. Walicheka, wakacheka na kuendelea kucheka kisha wakatoweka mbele ya macho yangu huku sauti za vicheko vyao zikiendelea kujirudia rudia.

Nikiwa bado nashangaa, ule ukungu mbele ya macho yangu ukatoweka na kunipa nafasi ya kuona vitu kwa urahisi zaidi japo giza bado lilikuwa limechukua nafasi yake, muda huohuo wakatokea tena yule kijana mtanashati na mdada mrembo na kusimama mbele yangu wakiniangalia kwa tabasamu ya kejeli.

Nikabaki nawatazama kwa hofu huku nikihisi kuanza kuchanganyikiwa. Kuna wakati nilihisi kama vile nilikuwa ndotoni lakini milango yangu ya fahamu ilinitanabaisha kuwa sikuwa ndotoni. Nilitamani kupiga kelele lakini nilishindwa na kubaki mdomo wazi huku nikiwakodolea macho wale watu.

Yule kijana mtanashati alinitazama kwa muda na kuitazama pete iliyokuwa imedondoka kando yangu, kisha alivuta pumzi ndefu kisha akazishusha taratibu, na kuninyooshea kidole chake cha shahada katika hali ya kunionya na kusonya.

“Usidhani umefanikiwa kuibakisha pete, nitarudi tena kuifuata pete yangu,” alisema yule kijana na kugeuka kumtazama yule binti mrembo.

Nikawaona wakishikana mikono na kupotea mbele ya macho yangu nisijue walikoelekea huku sauti za vicheko vya fisi zikiendelea kujirudia rudia kwenye masikio yangu, kisha zilianza kubadilika taratibu na kuwa kali kama kengele.

Sauti kali ya kengele iliendelea kusikika na sikujua ilitokea wapi na bado iliendelea kusikika na kugeuka kero masikioni mwangu, niliziba masikio yangu na kufinya macho kwa sekunde chache. Hatimaye nikayafumbua macho yangu taratibu nikiyatembeza mle ndani kutazama huku na kule na hapo nikakutana na mwanga mkali sana wa taa ulionifanya kuyafinya macho yangu.

Nilishtuka sana baada ya kugundua kuwa nilikuwa nimeketi juu ya kiti changu kirefu cha ngozi cha kiofisi, na juu ya meza simu yangu ya mkononi ilikuwa ikiita kwa fujo.

Nikawaza haraka nimefikaje kwenye kiti wakati nilikuwa nimeanguka chini wakati yule kijana mtanashati na binti mrembo walipoondoka! Nilipochunguza vizuri nikagundua kuwa nilikuwa nimelala usingizi ndani ya studio yangu kwa kuegemeza kichwa changu nyuma kwenye kiti. Na ile sauti ya kengele niliyokuwa nikiisikia ilikuwa ni simu yangu ya mkononi inaita.

Nikatazama vizuri na kugundua kuwa hata kompyuta yangu juu ya meza yangu ilikuwa imewashwa. Jambo hili likanifanya kutafakari sana, inamaana yale yote yaliyokuwa yanatokeoa ilikuwa ni ndoto?

Nikashangaa sana huku nikijiuliza ni nini hiki kilichokuwa kinanitokea? Je, ni ndoto kweli au labda nilikuwa niameanza kupatwa na wazimu? Mbona kila kitu ndani ya studio yangu kilikuwa sawa na hakukuwa na dalili yoyote iliyoonesha kuwa kulikuwa na mtu yeyote aliyekuja? Nilitafakari sana na sikupata jibu.

Nikiwa pale kwenye kiti sikuweza kukumbuka haraka kuwa ni wakati gani usingizi ulifanikiwa kunichukua muda mfupi tu mara baada ya kuwasha kompyuta yangu ili niandike makala kuhusu maajabu niliyoyaona kwenye safari yangu ya kutembelea mapango ya Amboni.

Hata hivyo, nilikuwa na hakika kuwa muda ule ungekuwa ni usiku wa manane kutokana na uwepo wa hali ya utulivu wa kutisha ndani na nje chumba kile.

Ile simu yangu juu ya meza mbele yangu iliendelea kuita na mara hii nikashawishika kutaka kuitazama ili nijue ni nani aliyekuwa akinipigia simu katika muda ule wa usiku wa manane. Nilitafakari kidogo lakini jibu sikulipata, hivyo nikajinyoosha huku akili yangu ikiwa imeanza kupoteza utulivu.

Usingizi ukiwa bado haujanitoka vizuri nikayafikicha macho yangu na kupiga mwayo hafifu wa uchovu huku nikiendelea kuvinyoosha viungo vyangu mwilini. Nilipoyatuliza macho yangu kutazama saa ya ukutani mle ndani haraka nikagundua kuwa ilikuwa tayari imetimia saa tisa na robo usiku.

Kitendo hicho kikaufanya moyo wangu upige kite kwa nguvu na hapo kijasho chembamba kikaanza kunitoka. Sikujua ni kwanini nilikuwa natokewa na hali ile, na bado niliendelea kujiuliza ni nani angeweza kunipigia simu muda huo.

Hofu ikiwa imeanza kuniingia moyoni nikaitazama tena ile simu juu ya meza kwa wasiwasi huku nikianza kuhisi jambo la hatari. Simu ile ilikata kabla sijaichukua kisha ikaanza kuita tena.

Sikujua kwanini nilikuwa nasita sana kuichukua, hata hivyo, sikutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata tena baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo nikaichukua kivivuvivu na kuitazama kwa makini.

Nikaliona jina la Vailet Shirima kwenye kioo cha simu yangu. Huyu alikuwa ni binti mrembo ambaye alikuwa akiishi maeneo ya jirani nilipoishi na nilitokea kumpenda sana kutoka kwenye moyo wangu, ila sikujua kwanini nilikuwa naogopa kumweleza ukweli kuwa nilimpenda.

Nilishangaa sana kwa kuwa mimi na Vailet hatukuwa na mazoea ya kupigiana simu ingawa tulipeana namba za simu, hivyo nilipoona jina lake jasho jepesi likaanza kunitoka na mapigo ya moyo wangu yakaanza kwenda mbio isivyo kawaida. Sikujua kwanini hali ile ilikuwa inanitokea!

Itaendelea…
 
Mwandishi wa Makala – 14

ILIPOISHIA...

Nikaliona jina la Vailet Shirima kwenye kioo cha simu yangu. Huyu alikuwa ni binti mrembo ambaye alikuwa akiishi maeneo ya jirani nilipoishi na nilitokea kumpenda sana kutoka kwenye moyo wangu, ila sikujua kwanini nilikuwa naogopa kumweleza ukweli kuwa nilimpenda.

Nilishangaa sana kwa kuwa mimi na Vailet hatukuwa na mazoea ya kupigiana simu ingawa tulipeana namba za simu, hivyo nilipoona jina lake jasho jepesi likaanza kunitoka na mapigo ya moyo wangu yakaanza kwenda mbio isivyo kawaida. Sikujua kwanini hali ile ilikuwa inanitokea!

Endelea…

Nikajiuliza tena na tena, Vailet anataka nini kutoka kwangu saa hizi? Hata hivyo, kabla sijaipokea ile simu ikakatika tena na tukio lile likautowesha kabisa usingizi wangu kichwani badala yake nikabaki nikiikodolea macho ile simu kama vile nimeshika bomu la kutupa kwa mkono lililokuwa limetelekezwa na magaidi wa kundi la al-Shabab ndani ya ofisi yangu na wakati wowote lilitaka kunilipukia.

Akili yangu taratibu ikazama kwenye tafakuri nzito huku nikianza kuwaza, ni vipi Vailet anipigie simu usiku ule, alikuwa na shida gani kiasi cha kupiga simu usiku wa manane!

Kitambo kirefu cha ukimya kikapita, nikaacha kumfikiria Vailet na kukumbuka kuhusu ndoto niliyoiota ya mgeni wa ajabu aliyekuja kunitembelea ndani ya studio usiku huo. Ni ndoto ya ajabu sana! Ili kujiridhisha kuwa ile ilikuwa ni ndoto tu nikatazama pale chini ilipokuwa imeanguka ile pete. Sikuoina!

Haraka sana nikavuta droo yangu na kupeleka mkono wangu kupapasa, nikagusa kiti mfano wa pete na kuitoa ile pete ya dhahabu iliyokuwa na jiwe la zambarau ambayo niliinunua kwenye duka la vitu vya kale huko Musoma.

Niliitazama kwa makini ile pete huku nikistaajabu sana, nilijiuliza kama inawezekana ilikuwa na nguvu fulani kama ile ndoto niliyoota usiku ule, muda huohuo koo langu likakauka ghafla na nywele zangu zikanisimama kichwani kwa hofu.

Nikiwa bado naitazama ile pete kwa hofu nilianza kukata tama, mara ile simu ikaanza kuita tena mle ndani. Sikutaka ile simu iendelee kuita zaidi hivyo haraka nikaipokea na kuiweka sikioni huku nikiipa akili yangu utulivu wa hali ya juu.

Sauti ya Vailet akiongea kwa wasiwasi ikasikika upande wa pili wa ile simu. Kitendo cha kuisikia sauti adimu ya mrembo yule kikanifanya nimeze funda kubwa la mate kuutuliza mtima wangu huku nikianza kuhisi jambo lisilo la kawaida.

“Max, ni wewe?” sauti ya Vailet iliuliza kwa wasiwasi.

“Ndiyo, ni mimi! Kwani kuna tatizo lolote?” nilijibu na kumtupia swali Vailet. Lakini kabla hajajibu nilimtupia swali jingine tena. “Vipi, mbona umepiga simu usiku wote huu, kuna nini?”

Vailet hakujibu badala yake aliendelea kubaki kimya. Nilihisi alikuwa analia upande wa pili wa simu ila hakutaka nijue kama analia, na pia hakuamini kama ni mimi Max, kama alivyozoea kuniita kwa kifupi, ndie nilikuwa naongea naye kwenye simu.

“Vai?” niliita kwa wasiwasi baada ya kuona kimya kimezidi.

“Max, ni wewe kweli?” Vailet aliuliza tena kwa sauti ya wasiwasi.

“Ni mimi, kwani vipi mbona sikuelewi!?” Nilishindwa kuelewa ni kwanini alikuwa akiniuliza swali lile lile usiku huo, na kwanini anipigie simu usiku wa manane kuulizia kama nilikuwa mimi kweli! Nikahisi kuna jambo lilikuwa limemchanganya Vailet na muda huo hakuwa katika hali ya kawaida.

“Nimeota ndoto mbaya sana, nimeota…” sauti ya Vailet ilikuwa imejaa wasiwasi, alionekana kama aliyekuwa analia.

“Umeota nini?” nilimuuliza Vailet huku nikikodoa macho yangu kutazama ndani ya studio yangu. Sasa akili yangu ilikuwa inafanya kazi haraka.

Vailet aliniambia kwa sauti yenye mtetemo wa hofu kuwa alikuwa ameona watu wawili wa ajabu sana ambao hajawahi kuwaona maishani mwake waliokuwa katika maumbo ya kutisha na kuchekesha sana wakiingia ndani ya nyumba yangu kwa namna ya ajabu.

Watu hao walikuwa ni mke na mume na walikuja kudai pete yao ya dhahabu yenye jiwe la zambarau ambayo walisema nilikuwa nimeiiba kutoka kwao. Mimi nikawa mbishi na sikutaka kuwapa, nikataka kukimbia lakini nilishindwa kwa sababu walikuwa wamesimama kwenye mlango wakizuia nisiweze kutoka.

Vailet aliendelea kuniambia kuwa baadaye aliniona nikichomoka kama mkizi na kukimbilia kwenye chumba kingine cha ofisi na kujificha chini ya meza lakini wale viumbe waliniona na kunikamata. Nilitaka kulia lakini nikashindwa.

Akawashuhudia wale viumbe wakinikamata kwa nguvu na kunilaza chini, wakanifunga kamba madhubuti. Kisha yule mwanaume alinijia mbele yangu akiwa kashika kisu kikali sana na yule mwanamke akiwa na chombo cha kukingia damu.

Huku akishindwa kuficha kilio chake, Vailet alisema huku akilia kilio cha kwikwi kuwa yule mwanaume alikiweka kisu chake sambamba na shingo wakati yule mwanamke akipiga vigelegele kwa furaha ya kupata mlo. Wakaanza kuhesabu kwa sauti ya pamoja: “Moja, mbili, ta…”

Kabla hawajamalizia na kutimiza azma yao Vailet akapiga kelele na kuwashtua sana wale viumbe wa ajabu. Wakataharuki na kudondosha kisu, kisha wakakimbia.

Muda huohuo Vailet akaamka kutoka usingizini huku jasho likimtoka sana, alijaribu kutafakari juu ya ndoto hiyo lakini hakupata jibu, akaamua anipigie simu kunitahadharisha kuwa kuna jambo baya linaweza kunitokea kwani siku zote amekuwa hadharau ndoto anazoota kuaznia saa saba usiku hadi saa kumi na moja alfajiri, na mara nyingi amekuwa akipata maono kupitia ndoto endapo kuna jambo baya linakuja, ndiyo maana akasukumwa kunipigia simu ule ule.

“Na nilipokuwa napiga sana simu lakini ikawa haipokelewi, hali hiyo ilizidi kunichanganya sana!” Alimaliza kusema Vailet.

“Usihofu, hiyo ni ndoto tu,” nilimtoa shaka Vailet ingawa ndani yangu nilihisi hofu kubwa. Nilifikiria sana alivyoniambia kuhusu pete ya dhahabu yenye jiwe la zambarau jambo ambalo ni kweli ninayo pete ya aina hiyo, isitoshe mimi pia nimeota ndoto kuhusu pete hiyo hiyo, na si hivyo tu, nimewaona watu wawili, Tunu na mpenzi wake ambaye hadi wakati huo nilikuwa sijamjua jina.

Niliitazama kwa makini ile pete ya dhahabu yenye jiwe la zambarau niliyokuwa nimeishika mkononi. Wasiwasi ukazidi, nikaogopa sana na kutamani nifungue kioo cha dirisha niitupe nje.

“Ni ndoto tu, chukua maji kidogo unywe utakuwa sawa,” nilimwambia Vailet huku nikihisi kutetemeka mno, mgongo wangu ukiwa umejiegemeza kwenye kiti..

“Hapana Max, hii siyo ndoto ya kawaida kama ndoto zingine. Nina uhakika lipo jambo baya linataka kukutokea. Nisingependa likutokee jambo baya, nakupenda sana Max na sipendi kukupoteza…” Vailet alisema na kuanza kulia kilio cha kwikwi.

Nilishtuka sana. Vailet hajawahi kuonesha kunijali kiasi kile na wala hajawahi kutamka kama alikuwa ananipenda, na hata pale nilipomuonesha kwa ishara kuwa nilikuwa nampenda lakini bado aliendelea kujikausha na kujifanya haelewi kinachoendelea.

“Vai, naomba nisikilize, tulia, hutakiwi kuhuzunishwa na ndoto. Inawezekana ikawa kweli au isiwe kweli ila cha msingi ni kwamba mimi ni mzima kwa sasa,” nilijitahidi kumliwaza japo ndani yangu nilikuwa natetemeka sana.

Vailet hakunijibu. Aliendela kulia kilio cha kwikwi. Mara akanyamaza na kikazuka kimya cha dakika nzima. Nikaingiwa na wasiwasi.

“Vai?” niliita kwa wasiwasi.

“Nifungulie, nipo hapa nje ya nyumba yako.” Vailet alisema kwenye simu.

Nikashtuka sana na kuitazama saa yangu. Ilikuwa saa tisa na nusu usiku. Nikalamba midomo yangu kuilainisha huku nikikunja sura yangu na kutenegeneza matuta madogo usoni.

“Kuna nini?” niliuliza huku nikishangazwa, mtoto wa kike kuja nyumbani kwangu usiku ule kisa ndoto!

“Nifungulie tafadhali, siwezi tena kulala bila kukuona, ninataka nihakikishe kama kweli ni wewe na umzima.” Alisema Vailet na kunifanya nizidi kushangaa.

Bila hata kuwaza zaidi nilijikuta nikiinuka na kuuendea mlango wa barazani, nikaufungua na kutoka hadi kwenye geti kubwa la uwa wa nyumba yangu, nikachungulia nje kupitia upenyo uliopo kwenye geti dogo, nikamuona Vailet amesimama nje ya nyumba yangu akiwa na wasiwasi.

Kwa sekunde chache nilibaki nimesimama nikiwa nimepigwa butwaa huku nikijiuliza, hivi mtoto wa kike amewezaje kutoka nyumbani kwao katika usiku wa manane na kuja nyumbani kwangu? Nilichungulia tena kuhakikisha kama ni yeye, nikamuona akiwa na hofu akitazama huku na huko. Sikujiuliza mara mbili, nikafungua geti huku nikimtazama kwa makini.

Vailet aliponiona alinirukia na kunikumbatia kwa nguvu huku akilia kwa furaha. Nilishindwa kufanya chochote nikabaki nashangaa. Jambo moja likanijia akilini mwangu: “inawezekana hii nayo ni ndoto tu kama zingine na mara tu ningeamka kutoka usingizini na kukuta kila kitu kikiwa cha kawaida.”

Nikahisi ubaridi mwepesi ukinitambaa mwilini mwangu na kuzifanya nywele zangu kusisimka. Nikabaki hoi nisijue la kufanya!

MWISHO.
 
Mwandishi wa Makala – 14

ILIPOISHIA...

Nikaliona jina la Vailet Shirima kwenye kioo cha simu yangu. Huyu alikuwa ni binti mrembo ambaye alikuwa akiishi maeneo ya jirani nilipoishi na nilitokea kumpenda sana kutoka kwenye moyo wangu, ila sikujua kwanini nilikuwa naogopa kumweleza ukweli kuwa nilimpenda.

Nilishangaa sana kwa kuwa mimi na Vailet hatukuwa na mazoea ya kupigiana simu ingawa tulipeana namba za simu, hivyo nilipoona jina lake jasho jepesi likaanza kunitoka na mapigo ya moyo wangu yakaanza kwenda mbio isivyo kawaida. Sikujua kwanini hali ile ilikuwa inanitokea!

Endelea…

Nikajiuliza tena na tena, Vailet anataka nini kutoka kwangu saa hizi? Hata hivyo, kabla sijaipokea ile simu ikakatika tena na tukio lile likautowesha kabisa usingizi wangu kichwani badala yake nikabaki nikiikodolea macho ile simu kama vile nimeshika bomu la kutupa kwa mkono lililokuwa limetelekezwa na magaidi wa kundi la al-Shabab ndani ya ofisi yangu na wakati wowote lilitaka kunilipukia.

Akili yangu taratibu ikazama kwenye tafakuri nzito huku nikianza kuwaza, ni vipi Vailet anipigie simu usiku ule, alikuwa na shida gani kiasi cha kupiga simu usiku wa manane!

Kitambo kirefu cha ukimya kikapita, nikaacha kumfikiria Vailet na kukumbuka kuhusu ndoto niliyoiota ya mgeni wa ajabu aliyekuja kunitembelea ndani ya studio usiku huo. Ni ndoto ya ajabu sana! Ili kujiridhisha kuwa ile ilikuwa ni ndoto tu nikatazama pale chini ilipokuwa imeanguka ile pete. Sikuoina!

Haraka sana nikavuta droo yangu na kupeleka mkono wangu kupapasa, nikagusa kiti mfano wa pete na kuitoa ile pete ya dhahabu iliyokuwa na jiwe la zambarau ambayo niliinunua kwenye duka la vitu vya kale huko Musoma.

Niliitazama kwa makini ile pete huku nikistaajabu sana, nilijiuliza kama inawezekana ilikuwa na nguvu fulani kama ile ndoto niliyoota usiku ule, muda huohuo koo langu likakauka ghafla na nywele zangu zikanisimama kichwani kwa hofu.

Nikiwa bado naitazama ile pete kwa hofu nilianza kukata tama, mara ile simu ikaanza kuita tena mle ndani. Sikutaka ile simu iendelee kuita zaidi hivyo haraka nikaipokea na kuiweka sikioni huku nikiipa akili yangu utulivu wa hali ya juu.

Sauti ya Vailet akiongea kwa wasiwasi ikasikika upande wa pili wa ile simu. Kitendo cha kuisikia sauti adimu ya mrembo yule kikanifanya nimeze funda kubwa la mate kuutuliza mtima wangu huku nikianza kuhisi jambo lisilo la kawaida.

“Max, ni wewe?” sauti ya Vailet iliuliza kwa wasiwasi.

“Ndiyo, ni mimi! Kwani kuna tatizo lolote?” nilijibu na kumtupia swali Vailet. Lakini kabla hajajibu nilimtupia swali jingine tena. “Vipi, mbona umepiga simu usiku wote huu, kuna nini?”

Vailet hakujibu badala yake aliendelea kubaki kimya. Nilihisi alikuwa analia upande wa pili wa simu ila hakutaka nijue kama analia, na pia hakuamini kama ni mimi Max, kama alivyozoea kuniita kwa kifupi, ndie nilikuwa naongea naye kwenye simu.

“Vai?” niliita kwa wasiwasi baada ya kuona kimya kimezidi.

“Max, ni wewe kweli?” Vailet aliuliza tena kwa sauti ya wasiwasi.

“Ni mimi, kwani vipi mbona sikuelewi!?” Nilishindwa kuelewa ni kwanini alikuwa akiniuliza swali lile lile usiku huo, na kwanini anipigie simu usiku wa manane kuulizia kama nilikuwa mimi kweli! Nikahisi kuna jambo lilikuwa limemchanganya Vailet na muda huo hakuwa katika hali ya kawaida.

“Nimeota ndoto mbaya sana, nimeota…” sauti ya Vailet ilikuwa imejaa wasiwasi, alionekana kama aliyekuwa analia.

“Umeota nini?” nilimuuliza Vailet huku nikikodoa macho yangu kutazama ndani ya studio yangu. Sasa akili yangu ilikuwa inafanya kazi haraka.

Vailet aliniambia kwa sauti yenye mtetemo wa hofu kuwa alikuwa ameona watu wawili wa ajabu sana ambao hajawahi kuwaona maishani mwake waliokuwa katika maumbo ya kutisha na kuchekesha sana wakiingia ndani ya nyumba yangu kwa namna ya ajabu.

Watu hao walikuwa ni mke na mume na walikuja kudai pete yao ya dhahabu yenye jiwe la zambarau ambayo walisema nilikuwa nimeiiba kutoka kwao. Mimi nikawa mbishi na sikutaka kuwapa, nikataka kukimbia lakini nilishindwa kwa sababu walikuwa wamesimama kwenye mlango wakizuia nisiweze kutoka.

Vailet aliendelea kuniambia kuwa baadaye aliniona nikichomoka kama mkizi na kukimbilia kwenye chumba kingine cha ofisi na kujificha chini ya meza lakini wale viumbe waliniona na kunikamata. Nilitaka kulia lakini nikashindwa.

Akawashuhudia wale viumbe wakinikamata kwa nguvu na kunilaza chini, wakanifunga kamba madhubuti. Kisha yule mwanaume alinijia mbele yangu akiwa kashika kisu kikali sana na yule mwanamke akiwa na chombo cha kukingia damu.

Huku akishindwa kuficha kilio chake, Vailet alisema huku akilia kilio cha kwikwi kuwa yule mwanaume alikiweka kisu chake sambamba na shingo wakati yule mwanamke akipiga vigelegele kwa furaha ya kupata mlo. Wakaanza kuhesabu kwa sauti ya pamoja: “Moja, mbili, ta…”

Kabla hawajamalizia na kutimiza azma yao Vailet akapiga kelele na kuwashtua sana wale viumbe wa ajabu. Wakataharuki na kudondosha kisu, kisha wakakimbia.

Muda huohuo Vailet akaamka kutoka usingizini huku jasho likimtoka sana, alijaribu kutafakari juu ya ndoto hiyo lakini hakupata jibu, akaamua anipigie simu kunitahadharisha kuwa kuna jambo baya linaweza kunitokea kwani siku zote amekuwa hadharau ndoto anazoota kuaznia saa saba usiku hadi saa kumi na moja alfajiri, na mara nyingi amekuwa akipata maono kupitia ndoto endapo kuna jambo baya linakuja, ndiyo maana akasukumwa kunipigia simu ule ule.

“Na nilipokuwa napiga sana simu lakini ikawa haipokelewi, hali hiyo ilizidi kunichanganya sana!” Alimaliza kusema Vailet.

“Usihofu, hiyo ni ndoto tu,” nilimtoa shaka Vailet ingawa ndani yangu nilihisi hofu kubwa. Nilifikiria sana alivyoniambia kuhusu pete ya dhahabu yenye jiwe la zambarau jambo ambalo ni kweli ninayo pete ya aina hiyo, isitoshe mimi pia nimeota ndoto kuhusu pete hiyo hiyo, na si hivyo tu, nimewaona watu wawili, Tunu na mpenzi wake ambaye hadi wakati huo nilikuwa sijamjua jina.

Niliitazama kwa makini ile pete ya dhahabu yenye jiwe la zambarau niliyokuwa nimeishika mkononi. Wasiwasi ukazidi, nikaogopa sana na kutamani nifungue kioo cha dirisha niitupe nje.

“Ni ndoto tu, chukua maji kidogo unywe utakuwa sawa,” nilimwambia Vailet huku nikihisi kutetemeka mno, mgongo wangu ukiwa umejiegemeza kwenye kiti..

“Hapana Max, hii siyo ndoto ya kawaida kama ndoto zingine. Nina uhakika lipo jambo baya linataka kukutokea. Nisingependa likutokee jambo baya, nakupenda sana Max na sipendi kukupoteza…” Vailet alisema na kuanza kulia kilio cha kwikwi.

Nilishtuka sana. Vailet hajawahi kuonesha kunijali kiasi kile na wala hajawahi kutamka kama alikuwa ananipenda, na hata pale nilipomuonesha kwa ishara kuwa nilikuwa nampenda lakini bado aliendelea kujikausha na kujifanya haelewi kinachoendelea.

“Vai, naomba nisikilize, tulia, hutakiwi kuhuzunishwa na ndoto. Inawezekana ikawa kweli au isiwe kweli ila cha msingi ni kwamba mimi ni mzima kwa sasa,” nilijitahidi kumliwaza japo ndani yangu nilikuwa natetemeka sana.

Vailet hakunijibu. Aliendela kulia kilio cha kwikwi. Mara akanyamaza na kikazuka kimya cha dakika nzima. Nikaingiwa na wasiwasi.

“Vai?” niliita kwa wasiwasi.

“Nifungulie, nipo hapa nje ya nyumba yako.” Vailet alisema kwenye simu.

Nikashtuka sana na kuitazama saa yangu. Ilikuwa saa tisa na nusu usiku. Nikalamba midomo yangu kuilainisha huku nikikunja sura yangu na kutenegeneza matuta madogo usoni.

“Kuna nini?” niliuliza huku nikishangazwa, mtoto wa kike kuja nyumbani kwangu usiku ule kisa ndoto!

“Nifungulie tafadhali, siwezi tena kulala bila kukuona, ninataka nihakikishe kama kweli ni wewe na umzima.” Alisema Vailet na kunifanya nizidi kushangaa.

Bila hata kuwaza zaidi nilijikuta nikiinuka na kuuendea mlango wa barazani, nikaufungua na kutoka hadi kwenye geti kubwa la uwa wa nyumba yangu, nikachungulia nje kupitia upenyo uliopo kwenye geti dogo, nikamuona Vailet amesimama nje ya nyumba yangu akiwa na wasiwasi.

Kwa sekunde chache nilibaki nimesimama nikiwa nimepigwa butwaa huku nikijiuliza, hivi mtoto wa kike amewezaje kutoka nyumbani kwao katika usiku wa manane na kuja nyumbani kwangu? Nilichungulia tena kuhakikisha kama ni yeye, nikamuona akiwa na hofu akitazama huku na huko. Sikujiuliza mara mbili, nikafungua geti huku nikimtazama kwa makini.

Vailet aliponiona alinirukia na kunikumbatia kwa nguvu huku akilia kwa furaha. Nilishindwa kufanya chochote nikabaki nashangaa. Jambo moja likanijia akilini mwangu: “inawezekana hii nayo ni ndoto tu kama zingine na mara tu ningeamka kutoka usingizini na kukuta kila kitu kikiwa cha kawaida.”

Nikahisi ubaridi mwepesi ukinitambaa mwilini mwangu na kuzifanya nywele zangu kusisimka. Nikabaki hoi nisijue la kufanya!

MWISHO.
Bishop hapa umezingua mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pamoja sana mkuu.
Sasa hao kinaTunu hawatarudi kweli kudai pete yao?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom