Mwanaume mmoja nchini Nigeria amjeruhi vibaya mkewe baada ya vipimo vya DNA kuonesha kuwa watoto wao watatu sio wa mwanamme huyo

Hizo ndo zile mimba zakwenda kwa mganga ili upate mtoto au za madaktari uchwara kila siku kuuzia wamama dawa za kushika mimba, mara dawa za mapacha. Unameza dawa kumbe unameza na usivyovijua
 
Hio sio point, ndoa ni kitu Muhimu sana, ata iweje haupaswi kumsaliti mwanaume kumuingizia laana ndani, kama mwanamke angeona kuwa mumewe ana tatizo kwa nn asingedai waachane kama hafurahii hio life, kumzalishia ni zaidi ya unyama

Sent using Jamii Forums mobile app
Mpendwa sijafurahishwa na usaliti bali nimeshangaa hata mbegu moja asiwe nayo kati ya hao watatu
 
kama vile ambavyo wapo wanaume wana watoto nje ya ndoa vile vile wapo wanawake. uwe me au ke kama huwezi samehe ukalea achaneni kwa amani.
 
Hata mimi ningekuwa huyo mwamba ningechukua maamuzi magumu saana hattrick?

watoto wa tatu wote sio wako...***** naua kabisa nyambafff!!
 
So kama mwanaume huna nguvu za kiume mkeo afe mgumba?
Vitu vingine wanaume tunatakiwa kushukuru kwa msaada na aibu wanazotufichia kina mama
Ni vyema wakapime atoe ridhaa mwenyewe.
Wapo wengine wapo tayari akuache huru na asitake tena kuoa kuliko kuchukua maamuzi mwenyewe hatari namna hiyo.
Hapo utakuta jamaa alikuwa anahela kwa hiyo akataka kuwakuzia watoto wake kwa hela za jamaa ili baadae amuue abaki na mali, watoto na baba mzazi. Hii sio poa.
Ni dhulma kwa jamaa na jamii yake pia iliyomuhangaikia kusomesha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanamke mmoja huko Nigeria amechakazwa vibaya na MTU anayedhaniwa kuwa ni Mme wake baadaya kutokea hali yenye utata dhidi ya watoto wao. Mwanaume huyo tajiri na mfanyabiashara alikuwa na mpango wa kuhamisha family yake kutoka Benin kwenda Canada ndipo ubalozi wa NCHI hiyo
View attachment 1364291


Ulipohitaji Vipimo vya DNA kwa watoto wake hao watatu kwa kuhofia kuwa huenda alikuwa akitaka kusafirisha watu wasiokuwa na uhusiano naye kinyume cha sheria (human trafficking). Vipimo vilikuja na majibu kuwa bwana huyo siyo baba halali wa watoto wote watatu hivyo ufanyike
View attachment 1364293


Utaratibu mwingine wa kupata Visa na taratibu zingine za kisheria ili aruhusiwe kuingia Canada. Alirudi nyumbani kumhoji mke wake juu ya baba halali wa watoto hao na kwanini amekuwa msaliti kwa kiwango cha hatari kiasi hicho lakini hakupata majibu ya kueleweka Jamaa akaamua amuue

View attachment 1364295


Kabisa lakini watu wakawahi kuokoa uhai wa mwadada huyo huku meno manne yakiwa yameng'olewa kwa ngumi nzito nzito alizosukumiwa. Bado taarifa zaidi hazijatolewa kuhusu kukamatwa kwa mwanaume huyo lakini hali ya mwanamke ambaye ni msaliti ndiyo hiyo katika picha.
Huyo mke Ashukuru Mungu gunia la mkaa halikuwemo ndani, jinga kabisa Canada 🇨🇦 ndo hivyo tena. Wanawake mna nini hasa?
 
Back
Top Bottom