View attachment 502106
View attachment 502107
Upendo ni muhimu katika mahusiano, lakini mwanaume kuwa na fedha hufanya mapenzi kuwa na mvuto zaidi. Mwanaume ni lazima awe na fedha kwa ajili ya kumnunulia mpenzi wake zawadi mara kwa mara siyo leo amemnunulia mpenzi wake kijizawadi ndiyo asubiri mwakani, lakini pia kumtoa mpenzi wake out au kuwa na mitoko ya mara kwa mara ni muhimu achilia mbali kuwa na kawaida ya kumtumia mpenzi wake fedha za matumizi mbalimbali na pia muda wa maongezi kwenye simu yake yote haya ni muhimu kwa mwanaume kumhudumia mpenzi wake.
Mambo haya yanatakiwa kufanywa na mwanaume bila kusubiri kuombwa na mwanamke maana si kila mwanamke anajua kuomba omba lazima mwanaume ajue wajibu wake wa kumhudumia mpenzi wake badala ya kusubiri mpaka aombwe. Kila mwanamke anapenda kuwa na mwanaume atakayemudu kumhudumia kwa kila kitu hapo ndipo mapenzi yanapokolea na mwanamke kujitoa kwa mwenzi wake na kuhakikisha anampa raha wakati wote.
Huu ujumbe hauna maana ya kuwananga na kuwatweza wanaume wasio na fedha, la hasha, najua kutokuwa na fedha ni suala la muda tu lakini pale utakapojaaliwa hata kidogo jitoe kwa kumpa mwenzi wako fedha na kumnunulia vijizawadi vidogo vidogo na yeye anaiona hali yako atakuheshimu.
Kuna ile mijanadume ambayo ina fedha lakini mibahili ka nini, hiyo ndiyo uzi huu unawahusu sana. Jamanieeee Wanaume msiwe wabahili kuwahudumia wapenzi wenu kwani ubahili utawafanya kila mwanamke awakimbie na mwisho wa siku utaishia kuitwa shemeji
Kwa wanawake wenzangu. Kamwe tena naomba kusisitiza, Kamwe usijitie kiherehere kumhudumia mwanaume, kumbuka fedha zako zikiisha atakutosa na kutafuta mwanamke mwingine.
Ni ushauri wangu wa bure
CC:
charminglady,
Nifah,
Miss Natafuta,
snowhite,
BADILI TABIA,
gfsonwin,
King'asti,
Super women 2,