Mwanaume asiyejielewa

Mwanaume asiyejielewa

Jamani mahusiano maximum three months, ikizidi songa huku kwa singles club ujiepushie hasara na maumivu!
 
Habari za jioni,

Naomba ushauri wa jinsi ya kumchukulia mwanaume mwenye tabia hizi katika mahusiano.

1. Hayuko tayari kukuoa
2. Hayuko tayari kukutambulisha popote
3. Hayuko tayari kukusaidia kwa lolote
4. Anataka umpe hela ya chakula
5. Anataka umpe vipodozi kama mafuta perfume
6. Anataka atumie gari yako
7. Anataka umtoe outing
8. Anataka aishi nyumbani kwako
9. Anataka umpe chakula
10. Anataka atumie kila kitu chako

Yote hayo ni kwa kisingizio cha siku mambo yake yakikaa sawa atakuoa.

Si bora akakae kwao ajipange mambo yake yakiwa sawa ndio arudi kwa bi dada?

Au nyie mna maoni gani?

Najaribu kumsaidia mtu hapa.
Wewe umemwambiaje ??
 
Hakuna mwanaume wa hivyo Duniani, mtoa mada acha kutulisha matango pori.
 
Sasa kama upo nae mueleze laivu au unamuogopa??
 
Habari za jioni,

Naomba ushauri wa jinsi ya kumchukulia mwanaume mwenye tabia hizi katika mahusiano.

1. Hayuko tayari kukuoa
2. Hayuko tayari kukutambulisha popote
3. Hayuko tayari kukusaidia kwa lolote
4. Anataka umpe hela ya chakula
5. Anataka umpe vipodozi kama mafuta perfume
6. Anataka atumie gari yako
7. Anataka umtoe outing
8. Anataka aishi nyumbani kwako
9. Anataka umpe chakula
10. Anataka atumie kila kitu chako

Yote hayo ni kwa kisingizio cha siku mambo yake yakikaa sawa atakuoa.

Si bora akakae kwao ajipange mambo yake yakiwa sawa ndio arudi kwa bi dada?

Au nyie mna maoni gani?

Najaribu kumsaidia mtu hapa.
......nafikiri akiwa na hayo matatu ya kwanza sidhani kama anakuwa na sifa ya kuitwa mpenzi au mume mtarajiwa....huyo ni msela wako anakupaa kampani....
 
Kumbe anataka lakini bado hujamfanyia hivyo na tayari ushaleta uzi je ungemfanyia si ungeweka bango???.... Me nadhani pia hamna mwanaume ambae hapendi kufanyiwa hivyo vitu ni kwa sababu tu wanawake hujihisi hawastahili kuwafanyia wanaume wao hivyo..... Hiyo kuhusu kutambulishwa sijui na nini hiyo mwanaume yeyote hawezi kuifanya ikiwa yupo broke maana hata ndugu, jamaa na marafiki watajua kaolewa..... Wewe kama unampenda jamaa na Mungu kakubariki una kipato kizuri basi mtengeneze jamaa awe na uwezo ambao utampa confidence ya kukutambulisha instead of kuleta nyuzi za kumsengenya.
 
Mbona nyie mnavypendaga vya dezo hatulalamiki ila sisi tukipenda vya dezo mnalialia
 
Hapa Wakushauriwa Ni huyo kijana

Ushaur Ni kwamba
Akuvumilie TU kipind iki kigumu Hana KAZI unavomhudumia uku unamsimanga


Ila mambo yake yakikaa sawa
Namsihi akupige chini haraka,akaoe mwanamke asie na roho ya ubinafsi Kama Wewe.

Yani ale bureee weee akipata asepe, mbona sio poa kabisa
 
Hapa Wakushauriwa Ni huyo kijana

Ushaur Ni kwamba
Akuvumilie TU kipind iki kigumu Hana KAZI unavomhudumia uku unamsimanga


Ila mambo yake yakikaa sawa
Namsihi akupige chini haraka,akaoe mwanamke asie na roho ya ubinafsi Kama Wewe.
Mkuu, mwanamke asiye mbinafsi anapatikana wapi ?
 
He's not looking for a wife he's looking for help 😂

 
Back
Top Bottom