Mwanasiasa anapohudhuria msiba wenye kamera lengo lake ni moja tu, ambalo ni kujiimarisha kisiasa, vivyo hivyo kwa mwanamuziki.

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,716
36,184
Akifa kiongozi au Kiongozi mstaafu ni sawa tu na kifo cha mwanakijiji wa kule Nanjirinji Kilwa. Akifa msanii ni sawa tu na kifo cha raia wa Tandale aliyekufa kwa typhoid ambayo alishindwa kujigharamia dawa. Wote ni watu, wote ni past . Hawawezi kufanya lolote tena. Ni void na ubatili.

Hivyo kwanini watu kaarufu kama wasanii na wanasiasa hupenda kuhudhuria misiba ya watu maarufu?

Je, wanalipa fadhila au kujiandalia mazishi yao?

Hilo kundi la wanasiasa na wasanii mtaji wao mkubwa ni watu hivyo hujipenyeza kila penye camera kuhakikisha watu wanaendelea kuwaunga mkono.

Mbona matajiri, wafanyabishara hawana mpango na misiba ya camera?

Ni kwasababu haina impact kwenye biashara zao.

Mwisho: Wasanii na wanasiasa acheni unafiki na uzandiki.
 
Back
Top Bottom