Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema ajiuzulu

tunataka pesa kwanza harafu kesi itafata kujiuzuru aondoke na pesa yetu hapana
 
Nchi hii hakuna aliye Msaafi kiasi cha kumnyooshea mwenzake kidole,wakiletwa FBI hapa wawachunguze mmoja baada ya mwingine hakuna ambaye atapona woote wenye Mali watakwenda jela, Nchi hii kila Kiongozi ana Madhambi yake japo wapo wajanja wanajua kujificha, Lakini kila Wizara hapa Tz kuna Wajanja hupiga pesa hususani zile pesa za Kasima ambazo hubaki baada ya wizara kumaliza matumizi yake ya mwaka, hizo pesa ndizo huliwa kiulaini kisha kuundiwa sababu feki za kijanja janja, Lakini huko Kafulila hafiki kwani hakuna Masilahi binafsi ya Vitalu vya Gesi, Rostam kauza hisa zako Voda kwa Dola milion 300 hakulipa kodi, Mkono amekuwa akilipwa mapesa kibao lakini halipi Kodi lakini Zito rafiki yake hapazi Sauti, Nchi hii kuna Vioja vingi lakini wanachagua na kuacha vingi vikiendelea na kupita bila swali kama ilivyokuwa kwa Rostam. Wapi mwigulu upo wapi? Kodi ya hizo dola milion za mauzo ya hisa za Voda ipo wapi?
 
Changa la macho hilo. Hakuna kujiuzulu. Taarifa tulizo nazo ni kwamba huyo mwizi Werema utumishi wake wa umma unakoma tarehe 27/12/2014. sasa hapo kajiuzulu kitu gani?? huo ni mpango wamepanga ili kuwafumba mambo watanzania kuwa kawajibika. Ikumbukwe kuwa mzee wa tezi dume na familia yake naye kahusika kwenye hizo pesa kwanini yeye naye asijiuzulu?? au washikaji zake wa Ikulu waliohusishwa na uchotwaji wa hizo pesa. Huyu mzee wa tezi dume hafai kabisa, kazi kuchecheka tu kama mlevi wa chang'aa. Haguswi kabisa na matatizo mengi yanayowakabili watanzania. Yeye anajali tumbo lake na familia yake. Asipochukuwa hatua asishangae Tanzania inakuwa kama Syria au Iraq. Kwa mambo haya haya ya ubaguzi, sasa hivi kuna matabaka Tanzania. (Tabaka la wenye nacho ambao baadhi yao ni hao mafisadi na tabaka la walio wengi wasio kuwa nacho). Na wote tunajua hao mafisadi hizo pesa ni jasho letu ambalo wamepora kwa kutumia madaraka tulio wapa. Na hilikundi la wengi wanaolia usiku na mchana bila kujua hatima ya taabu zinazosababishwa na hawa mafisadi zitaisha lini, Watakapo amua kuchukuwa hatua, hiyo amani mnayotudanganya kama watoto tutaisahau. Kwa mtindo huu
 
Ndio uwajibikaji wa kiwango cha juuu kabisa bongoland

Baada ya siku kadhaa tunasahau na kuendelea na gurudumu la maisha
 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amejiuzulu nafasi yake hiyo kuanzia leo, Jumanne, Desemba 16, 2014 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amekubali ombi hilo la kujiuzulu.

Katika barua yake kwa Mhe. Rais Kikwete, Jaji Werema amesema kuwa ameomba kujiuzulu kwa sababu ushauri wake kuhusiana na suala ya Akaunti ya Tegeta Escrow hakueleweka na umechafua hali ya hewa.

Mhe. Rais Kikwete amemshukuru Jaji Werema kwa utumishi wake ulioongozwa na uaminifu na uadilifu.

Akamatwe ashtakwe The Hague kwa kosa la uhaini na kumwita Kafulila tumbili. Bado Tibaijuka, Pinda, Muongo, Maswi, Masele, Lukuvi na Wasira
 
Wahisani wanataka kuona hatua stahiki zinachukuliwa dhidi ya wahusika....sasa mtu kajiuzuru kwa hiari yake hyo sivyo tutakavyo...afikishwe mahakamani akajibu tuhuma za kusababisha upotevu wa mabilion ya pesa za umma...

Wapi Waziri wa Viwanda na biashara , wapi Gavana wa BOT, wapi Waziri wa Fedha, wapi mwigulu? Wapi Mhongo? Japo yeye anakomaliwa na Mengi baada ya kumnyima Vitalu vya Gesi.
 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amejiuzulu nafasi yake hiyo kuanzia leo, Jumanne, Desemba 16, 2014 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amekubali ombi hilo la kujiuzulu.

Katika barua yake kwa Mhe. Rais Kikwete, Jaji Werema amesema kuwa ameomba kujiuzulu kwa sababu ushauri wake kuhusiana na suala ya Akaunti ya Tegeta Escrow hakueleweka na umechafua hali ya hewa.

Mhe. Rais Kikwete amemshukuru Jaji Werema kwa utumishi wake ulioongozwa na uaminifu na uadilifu.
Hapo ndiyo mujue rais anawaelewa vizuri wezi wa ESCROW, "ulioongozwa na uaminifu na uadilifu" hizi ni porojo, mwizi na tumbili amekuwaje mwadilifu au ni kinyume chake yaani ufisadi,ila ukiwa fisadi ccm wanakukumbatia.
 
Ni Aibu kwa serikali hii kukaa na wahujumu uchumi hadi wanapata nafasi ya kujihudhuru!.Kwani mpaka wao wanajibaini kuwa walifanya makosa! na serikali yenye madaraka kamili, inakaa kimya???.
Kweli hii mnatutendea haki wananchi!? Inamaana hamtaki kuwawajibisha kwasababu gani ya msingi?Ukiangalia walio jiudhuru kwa kashifa ya kukwapua mali za umma ni wengi na hakuna yeyote aliye chukuliwa hatua yoyote!. Hila kama kungekuwa na mtu aliyewajibishwa kwa ufujaji wa mali ya umma, nidhahiri watu wangeogopa, ndiyo maana watendaji wa serikali wanaweza kuchukua rushwa kubwa wakijua anaweza akajiudhuru na ikawa poa!. Sasa wabunge pelekeni mswaada bungeni kwa yeyeote atakayepatika na hatia ya kukwapua mali ya Umma akae maabusu kwa miaka 3 then ndiyo kesi yake itajwe na asiwe na dhamana.

tumekusikia,tutakufikia..
 
Unaweza kusema viongozi tulionao hawapo kuwatumikia wananchi bali kujinufaisha wao wenyewe, ikitokea mmoja wao kashtukiwa na umma na kujiuzuru, wenzao humsifia na kumshukuru kwa utumishi bora na uadilifu.....Hapa, najisikia vibaya sana. iweje mtu aliyesababisha hasara kubwa kama kwenye mchezo wa ESCROW, anapojiuzuru anasifiwa kwa uadilifu? ni uadilifu upi hapo unaozungumzwa? kwanini hatujifunzi kwa wenzetu kusema ukweli, kama kaharibu aambiwe ukweli. nilitegemea kwa mtu kama AG anapojiuzuru, unakubali ila pia unamwambia anataka kuwajibika kwa matendo yake, na hii nizidi ya kuvua cheo pekee bali vyombo vingine vimchukulie hatua zaidi. kwa maoni yangu kusifiana wakati mtu katuingizia hasara, ni utamaduni usiofaa kabisa. tatizo letu tunaoneana aibu mno, au labda katika madili hayo wamepiga wote, sasa inakuwa vigumu kuwajibishana. THIS IS MY CONCLUSION, "YANAMWISHO HAYA"
 
Hakuniconvince katika UDPP wake....he is not BOLD

MKUU SASA UNACHANGANYA MAMBO
DPP=Director of Public Prosecutions
AG =Attorney General
Hawa ni watu wawili na Werema was the latter

Whenever we are not sure of something, either dont comment or ask
 
Back
Top Bottom