''Mwanangu, babako amekufa''

Asante sana dear,maneno yako yamenifariji sana.Nimekata mawasiliano naye,na kumzika rasmi.sitopanndikiza chuki yoyote kwa mtoto,ila akikuwa na kumuulizia daddy yake,jibu ni hilo kuwa,he dead a long time ago.
Ni uamuzi mzuri ila atakapokua huyo mtoto na kama baba yake atakuwepo, usimdanganye, uje umwambie ukweli, ukimdanganya utakuwa bado unapandikiza mbegu ya chuki na moyoni itakusuta kwa kumdanganya.
 
Una lugha yenye ukakasi lakini,ubarikiwe kama hujawahi tenda dhambi yeyote.
 


Naogopa kuchangia kwa sababu ya huo mstari wa mwisho uliouandika "Kama ni wewe mwanamke mwenzangu utafanyeje?

wanawake njooni mumshauri mwenzenu hapa
 
Bora umemuua mapema, me mwenzio nilichelewa kumuua hadi mtoto akamjua baba yake, sasa mtoto anamfufua kila mara......
 

Miss you.. Long time didn't see you here .. Good to see you... Thanks..
 
Ila wanaume bwana, wakati mwingine tunajitafutia malaana bila sababu. Sawa, humpendi mama watoto na hutaki kuwa na mahusiano nae, basi hata mtoto wako kweli? Hivi ulifikiri mwisho wa kustarehe na mwanamke ni nini kama sio mtoto?

Aahhhhha , well said .. Thanks..
 
Jamaa alichofanya sio vizuri kabisa hiyo ni damu yake anapaswa kuihudumia hata kama uwezo wake ni mdogo, dhambi na laana vitamhukum tu, mifano iko wazi watanisamehe lakini angalia marehem kanumba au diamond baba zao wakoje, kihistoria watoto wa kiume wana maoenzi sana na mama zao na wakike ni baba. Anajenga ukuta badala ya daraja muda utafika atasema
 
Asante sana dear,maneno yako yamenifariji sana.Nimekata mawasiliano naye,na kumzika rasmi.sitopanndikiza chuki yoyote kwa mtoto,ila akikuwa na kumuulizia daddy yake,jibu ni hilo kuwa,he dead a long time ago.
Dear I know now uko angry .. To me I do still is wrong to tell your own child a lie.. Remember lies always come with back fire and bite big time .. You will regret one day after telling your own son his Dad is dead .. So don't do that please.. Thanks..
 

Hawara sawa, hampendi sawa, hata damu yake???
Hakuna excuse kwenye majukumu ya mtoto wake. Huyo jamaa ni kiazi tena kile cha chipsi
 
Sitisha mawasoliano naye lea mwanao hayo mengine yatajipanga yenyewe....hata usipomwambia lolote anaweza kukuwa akijikuta yupo nawe na asitake kumfahamu huyo anayeitwa baba
 
Huyo ni mumeo au mzazi mwenzako? Na je mlikubaliana kuzaa? Na ni kwanini mnaishi sehemu tofauti?
 
Kama una uwezo wa kumlea mtoto wee mlee peke yako tu ila usifiche Baba yake ni yupi.
 
Hii ni mbaya sana
 

Mlee mwanao kwa Upendo wa dhati mpendwa wangu. Mwanaume ambaye hampendi mtoto wake wa damu.... Hakuthamini pia nawe hata kwa chembe. Mpendwa..... Yaliyotokea yametokea. Mpende mwanao, ujitahidi kumlea mwanao katika maadili mema. Usiache kumkumbuka katika maombi kila wakati.

Toa sadaka kwa Mungu kwa ajili ya mwanao..... Mtamkie Baraka kila siku mwanao.... Make him/her your best friend. Mungu ndiye anayefahamu future ya mwanao. Baba wa huyo mtoto asikusumbue kichwa. Future ya mwanao ipo mikononi mwa Mungu. Mtumaini Mungu katika yote katika maisha yako na ya mwanao. Mungu ndio msaada wako pekee. Mshukuru Mungu kwa huyo mtoto na pia mtangulize Mungu katika yote kuhusiana na mwanao. He will make a way always.
 
Hii issue ya wanawake kuamua kushika mimba ili kumkoleza mtu aoe ndio inawatokeaga puani namna hii.


Jamaa hajakuweka moyoni. ..lea mwanao acha kumjaza matakataka kichwani. ...ukimwambia uongo atakuchukia zaidi.

Mtoto mwenyewe wa kiume..hapo kuwa mpole.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…