Mwanangu ana Sickle Cell, tiba yake nini?

Wakuu Salaam,

Niende moja kwa moja kwenye mada, nina binti yangu wa miaka minne. Hivi majuzi amebainika kuwa na sickle cell kusema kweli nimechanganyikiwa sababu nasikia ni ugonjwa usio na tiba.

Naomba kujua yafuatayo;
1. Ni kweli ugonjwa huu hauna tiba?
2. Kama si kweli, tiba yake ni ipi?
3. Kama hauna tiba nini hatima yake?

Nimenyongea kwa kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
Bro Pole sana.
Sina chochote cha kusema kuhusu huu ugonjwa ila kama mzazi naelewa unachopitia mana ni njia ambayo nimepita na ninaipita mpaka sasa

Mungu akupe nguvu. Imani yangu utapata suluhu tu siku moja
 
Asante mkuu, umetaja dalili zote vyema kinachonishangaza mama yake na mimi hatuna historia ya kiukoo kuwako kwa ugonjwa huu. Kwa sababu yeye ndiye aliyempeleka hospitali nikamuuliza mbona wote kwetu haupo akasema eti sisi ni carrier.

Mbaya zaidi sijaviona vipimo kwa macho, hata nikimdai document za majibu anadai hakupewa.

Mpaka napata mashaka. Ila dalili ni hizo

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole brother, siku hizi damu za wazazi hupimwa ili kujua kama ni carriers kabla ya kuzaa ili wapate njia za kumlinda mtoto asipate shida hiyo.

Nakusihi, nenda hospital utapata muongozo sahihi zaidi.
 
Atumie mlonge kwenye chakula. Kijiko Kimoja cha chai kwenye chai asubuhi, mchana achanganye kwenye mboga au juice na jioni pia. Itachukua muda ila atapona. Huu ni ushuhuda kwa watoto wa kaka yangu walikuwa nayo toka udogoni ila sasa hivi na boarding wanasoma.
Ni kweli, nimeshudia pia.
Itapona. Mungu ni mwema
 
Pole.

Naona huku juu umeshapata ushauri wa kuweza kusaidia.

Hilo la DNA isiwe kipaumbele sana, mtoto ameshazaliwa kwako ni wako hasa kipindi hiki cha ugonjwa usianze kuweka maulizo akilini mwako.

Zamani walikuwa wakisema baada ya miaka saba huo ugonjwa unapungua nguvu.

Pia tafuta waombaji, hata akiwa anatumia dawa na maombi yawepo, Mungu anapenda watoto, atamponya.
 
Kuna jamaa nimesoma naye o level na uni, alikuwa na shida hii. Hadi sasa yupo hai na ana mke na mtoto mmoja. Alikua akitumia mronge miaka yake yote. Na nadhani ndio uliomsaidia, maana familia yao ilikua ni duni kumudu hayo masuala ya kubadili damu.
 
Asante mkuu, umetaja dalili zote vyema kinachonishangaza mama yake na mimi hatuna historia ya kiukoo kuwako kwa ugonjwa huu. Kwa sababu yeye ndiye aliyempeleka hospitali nikamuuliza mbona wote kwetu haupo akasema eti sisi ni carrier.

Mbaya zaidi sijaviona vipimo kwa macho, hata nikimdai document za majibu anadai hakupewa.

Mpaka napata mashaka. Ila dalili ni hizo

Sent using Jamii Forums mobile app
Usikute Mtoto wa mchepuko, documents zimechakachuliwa
 
Asante mkuu, umetaja dalili zote vyema kinachonishangaza mama yake na mimi hatuna historia ya kiukoo kuwako kwa ugonjwa huu. Kwa sababu yeye ndiye aliyempeleka hospitali nikamuuliza mbona wote kwetu haupo akasema eti sisi ni carrier.

Mbaya zaidi sijaviona vipimo kwa macho, hata nikimdai document za majibu anadai hakupewa.

Mpaka napata mashaka. Ila dalili ni hizo

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana usimtirie mashaka mkeo Kwa lolote

Nina Binti pia anaumwa, historia nilivyouliza waliniambia hawana,lakini baada ya miaka miwili mbele niligundua Kuna ndugu wa babu ya baba inasadikika walikuwa wanakufa sana

Kuuliza kiundani walikuwa na changamoto zinazofanana na sickle cell..

Maana yangu vinaweza pita vizazi hata 4 au zaidi visioneshe dalili zozote ya kuumwa ila wakawa carrier TU

Kuhusu majibu hata mm mke alipewa kikaratasi Cha kawaida TU ambacho hakikua na details za kutosha, lakini Haina maana Kuna fraud yoyote
 
Wakuu Salaam,

Niende moja kwa moja kwenye mada, nina binti yangu wa miaka minne. Hivi majuzi amebainika kuwa na sickle cell kusema kweli nimechanganyikiwa sababu nasikia ni ugonjwa usio na tiba.

Naomba kujua yafuatayo;
1. Ni kweli ugonjwa huu hauna tiba?
2. Kama si kweli, tiba yake ni ipi?
3. Kama hauna tiba nini hatima yake?

Nimenyongea kwa kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana mkuu. Fuata maelekezo ya wataalam na funguka kama hapa. Mbona mtafanikiwa tiba na kulea mtoto. All the best
 
Pole sana mkuu wapo wengi wanao zaliwa na huu ugonjwa ila Kwa case mbili nilizo ziona nilijifunza haya. Ina takiwa uwazi wa family nzima kuelewa hususani ni mgonjwa mwenyewe anatakiwa kupewa elimu juu ya vyakula vyenye kipaombele Kwake na Hali halisi ya ugonjwa. Maana ukicheza vibaya mtu kuvuka 20s ni msala sikutishi ila na kumbuka chuoni tulimzika dada mmoja alikua kwenye 21 hivi. Lakini ukiaangalia Kwa undani unakuta family ndio ilikuwa haijielewi mtu anaumwa sickle cell hafu anasoma boarding from one Hadi chuo sasa hiyo special care angeitowa wapi. Hapo ni mboga majani na matunda Kwa wingi na mkinge sana na malaria hapa hata hizo homa atazisikilizia kwenye bomba
 
Pole.

Naona huku juu umeshapata ushauri wa kuweza kusaidia.

Hilo la DNA isiwe kipaumbele sana, mtoto ameshazaliwa kwako ni wako hasa kipindi hiki cha ugonjwa usianze kuweka maulizo akilini mwako.

Zamani walikuwa wakisema baada ya miaka saba huo ugonjwa unapungua nguvu.

Pia tafuta waombaji, hata akiwa anatumia dawa na maombi yawepo, Mungu anapenda watoto, atamponya.
Akifanikisha kuvuka 20s ndio huwa unaishiwa nguvu kabisa
 
Back
Top Bottom