Huyu binti ana nini? Hebu nisaidieni jamani

Kichuchunge

JF-Expert Member
Dec 2, 2020
338
891
Nina mwanangu wa kike mwenye umri kama wa miaka 12 hivi. Ana matatizo mawili ambayo nimeshindwa kupata ufumbuzi wake ndio maana nikaamua kuleta huu uzi hapa ili muweze kunishauri.

Tatizo la kwanza ni kwamba binti huyo anakojoa sana kitandani kwa hivi sasa licha ya umri huo alionao. Mwanzoni wakati alipokuwa mdogo hakuwa hivyo ila kadri anavyozidi kukua tatizo linaongezeka. Huu unaweza kuwa ni ugonjwa? Na kama ni ugonjwa tiba yake ni nini?

Tatizo la pili ni kwamba kwa kuwa binti ni kikojozi, basi amekuwa akiamshwa mara kwa mara usiku ili ajisaidie ingawa hiyo haijasaidia. Hata hivyo anapoamshwa, anakuwa kama mtu mlevi au aliyepoteza kumbukumbu.

Anaweza akazunguka nyumba nzima na kufungua milango yote akitafuta choo kilipo. Akishindwa anatoka hadi nje na ikishindikana kabisa atazunguka hadi anajikojolea.

Anakuwa kama yuko ndotoni hivi. Hii pia inaweza kuwa nini? Naombeni msaada wenu.
 
Mpeleke akapimwe Gouts, kiwango cha Cholesterol, Kisukari na pia kiwango cha madini mwilini hasa Calcium.
Pia waweza kuwa unampa kidonge kimoja cha dawa ya Atovastartin (10mg) kabla ya kulala uone kama itamsaidia.
Kumbuka si vyema kutumia dawa bila vipimo vya daktari.
 
Hii ya kuamshwa na kuwa kama mlevi na kutembea tembea hovyo hata mdogo wangu wa kike alikuwa nayo,alikuwa akikosa kopo la kukojolea anaweza kojoa hata kwenye kiatu au sufuria,nae slikojoa sana kitandani ila baadae aliacha

Ni utoto tu ataacha,ingawaje kuna dawa za kienyeji pia,zitafute
 
Hii ya kuamshwa na kuwa kama mlevi na kutembea tembea hovyo hata mdogo wangu wa kike alikuwa nayo,alikuwa akikosa kopo la kukojolea anaweza kojoa hata kwenye kiatu au sufuria,nae slikojoa sana kitandani ila baadae aliacha

Ni utoto tu ataacha,ingawaje kuna dawa za kienyeji pia,zitafute
Ajaribu ndevu za mahiindi nasikia zinatibu kikojozi
 
Nina mwanangu wa kike mwenye umri kama wa miaka 12 hivi. Ana matatizo mawili ambayo nimeshindwa kupata ufumbuzi wake ndio maana nikaamua kuleta huu uzi hapa ili muweze kunishauri...
1. Mpeleke hosp kitendo cha Afya ya Njia ya mkojo watamtibu vzr na atakua ok.

2. Mjengee saikolojia ya kujiamini. Angalia michezo anayocheza kila siku, anatumia vinywaji/vyakula gani hasa na rafiki zake, muhoji huota nini.

3. Hakikisha analala mapema akiwa amekojoa, then usiku aamshwe akakojoe.

4. Asinywe maji wala kimiminika kingine usiku. Mpen dry food (japo yaezapelekea constipation japo inasaidia).

5. Msimchape na mnapomkaripia mtumie lugha isiyoudhi.

She gonna be ok, ni stage tu!
 
Mpeleke akapimwe Gouts, kiwango cha Cholesterol, Kisukari na pia kiwango cha madini mwilini hasa Calcium.
Pia waweza kuwa unampa kidonge kimoja cha dawa ya Atovastartin (10mg) kabla ya kulala uone kama itamsaidia.
Kumbuka si vyema kutumia dawa bila vipimo vya daktari.
Atorvastatin na matatizo ya mkojo wapi na wapi? hii ni dawa inayotumika ku-lower Cholesterol na triglyceride kwenye damu.

Nipe shule zaidi, MOA ya Atorvastatin 10mg ni ipi kwa issues za mkojo?
 
1. Mpeleke hosp kitendo cha Afya ya Njia ya mkojo watamtibu vzr na atakua ok.
2. Mjengee saikolojia ya kujiamini. Angalia michezo anayocheza kila siku, anatumia vinywaji/vyakula gani hasa na rafiki zake, muhoji huota nini...
Nakupinga hapo kwenye namba 4.
 
Mkuu mm sio MD bt saikolojia naijua kidogo. Ukikojozi hutofautiana kati ya mtoto na mtoto, Kuna wanaokojoa Hadi Miaka 18, wengine zaidi ya hapo. Nakumbuka nikiwa lasaba Miaka hiyo Kuna majamaa yalikuwa yanakuja na mikojo shule.

Huyo mtoto Hana shida yoyote,atakuwa sawa isipokuwa tu kisaikolojia iwapo mtakuwa hamna busara.

Msimfanye aone kama hilo ni tatizo lisilotatulika.
 
Nina mwanangu wa kike mwenye umri kama wa miaka 12 hivi. Ana matatizo mawili ambayo nimeshindwa kupata ufumbuzi wake ndio maana nikaamua kuleta huu uzi hapa ili muweze kunishauri.

Tatizo la kwanza ni kwamba binti huyo anakojoa sana kitandani kwa hivi sasa licha ya umri huo alionao. Mwanzoni wakati alipokuwa mdogo hakuwa hivyo ila kadri anavyozidi kukua tatizo linaongezeka. Huu unaweza kuwa ni ugonjwa? Na kama ni ugonjwa tiba yake ni nini?

Tatizo la pili ni kwamba kwa kuwa binti ni kikojozi, basi amekuwa akiamshwa mara kwa mara usiku ili ajisaidie ingawa hiyo haijasaidia. Hata hivyo anapoamshwa, anakuwa kama mtu mlevi au aliyepoteza kumbukumbu.

Anaweza akazunguka nyumba nzima na kufungua milango yote akitafuta choo kilipo. Akishindwa anatoka hadi nje na ikishindikana kabisa atazunguka hadi anajikojolea.

Anakuwa kama yuko ndotoni hivi. Hii pia inaweza kuwa nini? Naombeni msaada wenu.
Inatamkwa.....spinkta masos.......
 
Huo ugonjwa unatambulika kama Enuresis. Fika kwa wataalamu apate tiba na ushauri. NB: Mimi ni daktari wa binadamu (MD) I could give you more hints lakini ethics zinanikataza.
 
Mpeleke akapimwe Gouts, kiwango cha Cholesterol, Kisukari na pia kiwango cha madini mwilini hasa Calcium.
Pia waweza kuwa unampa kidonge kimoja cha dawa ya Atovastartin (10mg) kabla ya kulala uone kama itamsaidia.
Kumbuka si vyema kutumia dawa bila vipimo vya daktari.
We mwana wee, unataka kufanya nini tena, aiseee! Mshauri mwenzako aende hospitali akapate ushauri sahihi, aisee. Mbona watanzania mnapenda kuuana hivi.
 
Hiyo hali ni tatizo la kitaalamu katika afya. Madaktari wa magonjwa ya akili wanao uwezo wa kulikabili na kulitatua kwa 100%. Kuna jamaa kadhaa walikuwa na ndugu wenye shida kama hizo, walipowacheki wataalamu wa Afya ya akili tatizo liliisha na kuwa historia.

Ondoa wasiwasi na kuwa mvumilivu.
 
Nina mwanangu wa kike mwenye umri kama wa miaka 12 hivi. Ana matatizo mawili ambayo nimeshindwa kupata ufumbuzi wake ndio maana nikaamua kuleta huu uzi hapa ili muweze kunishauri.

Tatizo la kwanza ni kwamba binti huyo anakojoa sana kitandani kwa hivi sasa licha ya umri huo alionao. Mwanzoni wakati alipokuwa mdogo hakuwa hivyo ila kadri anavyozidi kukua tatizo linaongezeka. Huu unaweza kuwa ni ugonjwa? Na kama ni ugonjwa tiba yake ni nini?

Tatizo la pili ni kwamba kwa kuwa binti ni kikojozi, basi amekuwa akiamshwa mara kwa mara usiku ili ajisaidie ingawa hiyo haijasaidia. Hata hivyo anapoamshwa, anakuwa kama mtu mlevi au aliyepoteza kumbukumbu.

Anaweza akazunguka nyumba nzima na kufungua milango yote akitafuta choo kilipo. Akishindwa anatoka hadi nje na ikishindikana kabisa atazunguka hadi anajikojolea.

Anakuwa kama yuko ndotoni hivi. Hii pia inaweza kuwa nini? Naombeni msaada wenu.
Nenda maduka ya dawa za kisunna waambie tatizo la binti yako kwa uwezo wa Allah atapona ndani ya muda mfupi tatizo dogo sana hilo.

Wengine nasikia wanatumia ndevu za mahindi kutibu hilo tatizo.
 
Back
Top Bottom