Mwanamke!

Jpinduzi

Senior Member
Feb 26, 2011
136
68
Wajibu na majukumu ya mwanamke ni kama ya mwanamume, na suala lake ni kama la mume yaani suala la haki, ujumbe na marejeo. Isitoshe, mustakbali wa kazi yoyote ni dini kwa njia moja au nyengine mwanamke naye ana kazi yake.Kuna kazi zingine ambazo hakuna awezaye kuzisimamia na kuzitekeleza ila yeye, kwa maana hiyo, huwezi kupata harakati zozote zenye kufaulu ila mwanamke atakuwa na fungu lake kubwa humo. Kunahaja ya kuweka picha bora zaidi kwa mwanamke; vipi anapaswa awe, nini wajibu na majukumu yake.
 
Uko sawa but na hao wanawake wana-differ kwa mengi. Target yako ni kundi gani, na vigezo vya categorization ni vipi

Kwa mfano wanawake wajane;wako.....wazee, vijana, waajiriwa, retired, wailiosoma, wa vijijini, wa mjini, wakristo , waislamu, wenye watoto na ambao hawakujaaliwa kuzaa wote hao ni wanawake wajane.............

Nasubiri muendelezo wa mada....wajibu na majukumu yao yatabaki sawa?????
 
Wajibu na majukumu ya mwanamke ni kama ya mwanamume, na suala lake ni kama la mume yaani suala la haki, ujumbe na marejeo. Isitoshe, mustakbali wa kazi yoyote ni dini kwa njia moja au nyengine mwanamke naye ana kazi yake.Kuna kazi zingine ambazo hakuna awezaye kuzisimamia na kuzitekeleza ila yeye, kwa maana hiyo, huwezi kupata harakati zozote zenye kufaulu ila mwanamke atakuwa na fungu lake kubwa humo. Kunahaja ya kuweka picha bora zaidi kwa mwanamke; vipi anapaswa awe, nini wajibu na majukumu yake.

ukiacha suala zima la kuzaa, mwanamke wa leo ana majukumu sawa tu na mwanaume. ila hapa ilibidiufafanue zaidi, majukumu ya mwanamke akiwa kama mke? mama? muajiriwa? mjasiriamali? au ? sifa, wajibu na majukumu hutufautiana kutoka kwa kila kundi, sifa, wajibu na majukumu ya mwanamke awapo changudoa ni wazi yatatofautiana sana na mwanamke awapo mke wa mtu, mama wa nyumbani majukumu yake hutofautiana na anaeajiriwa au anaejiajiri n.k nk.
 
Back
Top Bottom