Mwanamke ninayeishi nae amenibadilikia Tabia

Mwanamke ninayeishi nae amenibadilikia Tabia

Twende kwenye mada naomba ushauri wa uhakika.

Miaka minne iliyopita nilibahatika kuwa na mahusiano na mwanamke mmoja ila hatukufanikiwa kudumu mara baada ya mimi kuzuia mahusiano hayo Pasi na sababu ya msingi.

Mwaka Juzi mimi niliforce kurudia tena na huyo binti na kweli alikubali tukawa kwa serious relationship ikaja kutokea amepata ujauzito na nikamwambia azae na ikawa hivyo.

Baada ya kujifungua kwa sasa tunamwaka mmoja ila changamoto kwenye mahusiano yetu ni kama ifuatavyo.

Mwenzangu kununa muda wote.

Hakubali kumaliza jambo hata liwe dogo.

Ana kinyongo hali inayopelekea kunyimwa tendo la ndoa hata kwa mwezi.

Sio mtu ambaye mnaweza mkaa mkapanga mipango ya maisha.

Hana inferiority complex na wala hajiongezi kwa kidogo.

Kiukweli Tabia nyingi hakunionyesha tulivyokuwa kwa mahusiano ya kawaida ila ndo ananionyesha sasa.

Kiukweli Nimetokea kumchukia sana ,nimekuwa mtu wa kumchit na simjali tena.

Kiukweli natamani kumwacha ila namuonea huruma mtoto mdogo niliyezaa nae.

Namalizia sio kwamba sina madhaifu ninayo tena makubwa sana.

USHAURI wenu wakuu?
Weka madhaifu yako ambayo ni makubwa sana ili tuone Sababu za wewe kulea mtoto si wako.
 
Nimesoma sijaona mahali kama umemuoa, au walau kutambulishana kwa wazazi... Pengine anaona hujamuheshimisha inavyotakiwa
 
Ulilazimisha, makosa ni yako pambana na hali yako
 
Bil

Mimi ukininunia au kuniletea kisirani nakutimua muda huo huo
Mkuu utatimua wangapi Kwa staili hyo ?😁
Najua unajua wanawake tabia zao

Maana unakuta mwngne kaamka asubuhh kanuna tuu ,mwngne anakuwa mnyonge ukimuuliza hakuna sababu ya msingi Yaan miyeyusho tuu lkn ndo hvyo tunaishi nao Kwa akili mingi
 
Mkuu utatimua wangapi Kwa staili hyo ?[emoji16]
Najua unajua wanawake tabia zao

Maana unakuta mwngne kaamka asubuhh kanuna tuu ,mwngne anakuwa mnyonge ukimuuliza hakuna sababu ya msingi Yaan miyeyusho tuu lkn ndo hvyo tunaishi nao Kwa akili mingi
Mimi ananuna mwaka mzima
 
Back
Top Bottom