Mwanamke ni chanzo cha anguko la mwanaume

Kambi ya Fisi

JF-Expert Member
Feb 3, 2018
13,589
22,159
Awali ya yote niweke wazi kuhusu hili bandiko kwamba ninapotumia neno mwanamke mbaya simaanishi wanawake wote ni wabaya. Ni kweli kuna wanawake wabaya kitabia, lakini pia kuna wanawake wema hivyo tusiwachukulie wanawake wote kuwa ni wabaya.

Sasa tuendelee....
Kwa mujibu wa Biblia mwanamke ametumika sana kuangusha wanaume, na hadi hii leo maanguko mengi ya wanaume husababishwa na wanawake.

Anguko lq kwanza la mwanaume lililosababishwa na mwanamke lilifanyika pale bustanini Eden, yaani kwa anguko hilo wanaume wote tunakula kwa jasho. Baada ya hapo yalifuata maanguko mengi tu.

Samsoni aliua maelfu ya wafilisti peke yake, lakini alikuja kudodoshwa na mwanamke.

Mfalme Daudi alikuwa na upako aliua Simba na Dubu na alimuua pia yule Goliath mfilisti, lakini alikuja kuangukia kwa mwanamke tena mke wa mtu. Nk

Mwanamke mbaya atakufanya uwe mkate (Mithali 6:26)
Amewaua mashujaa - ni njia kuu ya kuzimu ( Mithali 7:27-27)


Tukiachana na hao waliotajwa katika Biblia bila shaka katika eneo lako unakoishi unawajua baadhi ya wanaume walioangushwa na wanawake.

Ukiwa kama mwanaume jitahidi usiangushwe kama hao uwajuao.

Ubarikiwe.
 
Upo sahihi 40%

Kiufupi mwanaume huwa anajiangusha yeye mwenyewe na sio mwanamke, pale anapoanza kuamini kuwa amesimama na kuanza kutoa attention yake kwa cheapest women.

Ili mwanaume usiangushwe na mwanamke ni kuhakikisha hata ukimkuta uchi mwanamke unampita bila kugeuka.

Kitu kinachoanguka huwa ni kile ambacho hakijasimama vizuri.

Kubali kutikiswa Ila usikubali kutikisika wewe Kama wewe.
 
Wote hawa hawajaangushwa na wanawake ni wao wenyewe walichangia anguko lao

Adamu alipaswa kumwongoza mke ila yeye akamsikiliza Hawa yalipowakuta ya kuwakuta akabaki kumlaumu Mungu.

Samsoni alikuwa mnadhiri hivyo hakupaswa kabisa kujihusisha na wanawake

Daudi alianza na tamaa, kumpiga jicho mke wa mtu akiwa anaoga mwisho wa siku akamla akamtia mimba
 
Back
Top Bottom