Kambi ya Fisi
JF-Expert Member
- Feb 3, 2018
- 13,589
- 22,159
Awali ya yote niweke wazi kuhusu hili bandiko kwamba ninapotumia neno mwanamke mbaya simaanishi wanawake wote ni wabaya. Ni kweli kuna wanawake wabaya kitabia, lakini pia kuna wanawake wema hivyo tusiwachukulie wanawake wote kuwa ni wabaya.
Sasa tuendelee....
Kwa mujibu wa Biblia mwanamke ametumika sana kuangusha wanaume, na hadi hii leo maanguko mengi ya wanaume husababishwa na wanawake.
Anguko lq kwanza la mwanaume lililosababishwa na mwanamke lilifanyika pale bustanini Eden, yaani kwa anguko hilo wanaume wote tunakula kwa jasho. Baada ya hapo yalifuata maanguko mengi tu.
Samsoni aliua maelfu ya wafilisti peke yake, lakini alikuja kudodoshwa na mwanamke.
Mfalme Daudi alikuwa na upako aliua Simba na Dubu na alimuua pia yule Goliath mfilisti, lakini alikuja kuangukia kwa mwanamke tena mke wa mtu. Nk
Mwanamke mbaya atakufanya uwe mkate (Mithali 6:26)
Amewaua mashujaa - ni njia kuu ya kuzimu ( Mithali 7:27-27)
Tukiachana na hao waliotajwa katika Biblia bila shaka katika eneo lako unakoishi unawajua baadhi ya wanaume walioangushwa na wanawake.
Ukiwa kama mwanaume jitahidi usiangushwe kama hao uwajuao.
Ubarikiwe.
Sasa tuendelee....
Kwa mujibu wa Biblia mwanamke ametumika sana kuangusha wanaume, na hadi hii leo maanguko mengi ya wanaume husababishwa na wanawake.
Anguko lq kwanza la mwanaume lililosababishwa na mwanamke lilifanyika pale bustanini Eden, yaani kwa anguko hilo wanaume wote tunakula kwa jasho. Baada ya hapo yalifuata maanguko mengi tu.
Samsoni aliua maelfu ya wafilisti peke yake, lakini alikuja kudodoshwa na mwanamke.
Mfalme Daudi alikuwa na upako aliua Simba na Dubu na alimuua pia yule Goliath mfilisti, lakini alikuja kuangukia kwa mwanamke tena mke wa mtu. Nk
Mwanamke mbaya atakufanya uwe mkate (Mithali 6:26)
Amewaua mashujaa - ni njia kuu ya kuzimu ( Mithali 7:27-27)
Tukiachana na hao waliotajwa katika Biblia bila shaka katika eneo lako unakoishi unawajua baadhi ya wanaume walioangushwa na wanawake.
Ukiwa kama mwanaume jitahidi usiangushwe kama hao uwajuao.
Ubarikiwe.