Mwanamke lazima Abadili Dini na Imani Ili ifanane na yako ndipo umuoe.

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
MWANAMKE LAZIMA ABADILI DINI NA IMANI ILI IFANANE NA YAKO NDIPO UMUOE.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Moja ya ishara za awali Kwa Mwanamke anayekupenda na anayeweza kuwa Mkeo ni kukuamini, na kuamini Kwa kile ukifanyacho na kile unachokiamini. Kwa Mwanamke Hisia na Imani vinaenda sambamba. Mwanamke akishakuwa na hisia za upendo na wewe hapo moja Kwa moja atakuwa na Imani na wewe. Atakuamini. Kila unachomwambia Mwanamke anakiamini. Weka akilini hiyo.

Mwanamke akikupenda, atapenda unayoyapenda. Mtazamo wake utabadilika utakuwa Sawa na wako. Ndio maana ni rahisi kumbadilisha Mwanamke hata kama alikuwa ni kahaba lakini akishakupenda atauacha ukahaba wake. Ishu hapo ni hivi, Kwenye Moyo WA Mwanamke kuna Hisia na Imani. Wakati Sisi wanaume Imani Ipo kwenye Ubongo. Yaani hatuwezi kuamini Jambo bila kulitafakari Kutumia ubongo Akili.
Wakati Wanawake hawawezi kukuamini Jambo pasipo kuwa na hisia nalo, yaani kulipenda.

Sasa ili Mwanamke apende Jambo kuna michakato kadha wa kadha. Na yote lazima itimize imagination zake.

Ukiona umemtongoza Mwanamke mkaingia kwenye mahusiano alafu mpaka mnamaliza miezi sita hajataka Kubadili Imani na dini, jua huyo hujamkamata, yaani hujauteka moyo wake. Huyo hakufai. Hakuna mahali mtaenda.

Tena akikuambia wewe ndio umfuate ndio kabisa. Sisi Watibeli na wataalamu WA hayo mambo tunajua kuwa huyo Mwanamke Hakupendi, lakini pia atakupelekesha tuu.
Kingine ni lazima utashindwa kwenye ishu ya malezi. Yaani Watoto lazima wakushinde Kwa sababu tayari ulimshindwa Mama Yao.

Kubaniwa papuchi na kupewa chakula cha Usiku Kwa vipimo litakuwa ni Jambo la kawaida kwako na hautakuwa na chakufanya. Kiufupi utakuwa Dume-jike ambalo limeoa.

Asije akakudanganya MTU kuwa ndoa ya MKE na Mume WA Imani tofauti zinadumu au zinakuwa na Amani, hakuna kitu kama hicho.

Kingine cha muhimu zaidi ni kuwaz kamwe usimwambie Mwanamke abadili dini ili UMUOE. Hilo ni kosa la kiufundi. Mwanamke akishakupenda hatasubiri umwambie abadili Dini. Atabadili mwenyewe tuu Kwa mapenzi na uelewa wake kuhusu dini yako.

Kama hataki Kubadili dini yake Kwa hiyari jua huyo moyo wake haukupendi. Na kamwe hatakutii wala kukusikiliza Ila wewe ndiye utamtii na kumsikiliza. Atakupelekesha vile atakavyo.

Kesi nyingi za wanaowasiliana na Mimi nyingi zipo Kwa wanandoa ambao ni Aidha Mume alibadili dini na kufuata dini ya MKE. Au kila MTU alibaki na Dini yake wakafunga ndoa za bomani(serikalini).
Au mwanaume alitumia nguvu kumbadilisha Mwanamke Imani na Dini.

Elewa kuwa, kwenye mapenzi sio lazima uwe na MTU Fulani hasa kama hakupendi.
Elewa kuwa , mapenzi hayalazimishwi.
Elewa kuwa, kila mtu anauhuru wa Kutumia mwili wake. Hivyo usimpangie mkeo au mumeo matumizi ya mwili wake. Bali jipangie mwenyewe. Kama anakupenda basi ataji-commit kwako na sio wewe umlazimishe aji-commit kwako. Ila unaweza kujipangia kuwa huwezi ishi na Mwanamke au Mwanaume aliyeamua kuutumia mwili wake kufanya uasherati na uzinzi.
Hivyo katika mkataba wenu wa mahusiano ya ndoa, uwepo sheria iliyosainiwa au kukubaliana kuwa Kila MTU anauhuru wa Kutumia mwili wake atakavyo pasipo kuingiliwa na mwingine lakini Mimi(unaweza kuwa MKE au Mume) hutoweza kuishi na mtu mchafu (mzinzi na muasherati) hivyo Talaka itatoka ili kumpa MKE/mume Uhuru wa kuutumia mwili wake katika uchafu kadiri ya atakavyo.
Na hakutakuwa na Mijadala wala usuluhishi Kwa sababu ni Jambo lililojulikana mapema.

Hakutakuwa na hiyo nafasi ya kumshauri, kumfundisha mtu mzima aliyeko kwenye ndoa namna ya kuutumia mwili wake. Ila kila litakalofanyika litahesabika kama uamuzi wa Makusudi uliodhamiriwa na Mhusika.

Msamaha WA pekee utatolewa Baada ya Talaka kukabidhiwa. Kila MTU aishi Maisha yake lakini tukiwa tumesameheana. Hizo ni Kanuni za Watibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Dini ni kifungo kilicho letwa kuja kutugawa waafrika hadi inakuwa ngumu mtu kubadili kifungo hichi.

Inashangaza sana mwafrika kwa mwafrika wanashindwa kuoana kwa sababu ya dini za kuletwa na wakoloni.

We tend to glorify our differences more than those aspects that unifies us.
 
Dini ni kifungo kilicho letwa kuja kutugawa waafrika hadi inakuwa ngumu mtu kubadili kifungo hichi.

Inashangaza sana mwafrika kwa mwafrika wanashindwa kuoana kwa sababu ya dini za kuletwa na wakoloni.

We tend to glorify our differences more than those aspects that unifies us.

Dini zilikuwepo Kabla ya Ukoloni.
Kabla ya Ukoloni au kuja dini ngeni, Waafrika waliooana Kwa dini za makabila Yao.
Kabila moja halikuruhusiwa kuoa kabila jingine.

Yaani Mpare kuoa Msukuma Hilo lisingewezekana Kwa dini za mababu.

Hatuwezi kuwa unified ikiwa hatufanani. Sisi hatulingani, hatupo Sawa.
Ni Watu wajinga wenye Upeo mdogo wanaofikiri Sisi binadamu tupo Sawa.

Hizo aspects ambazo tunafanana hazitufanyi tuwe kitu kimoja hasa Kwa ishu nyeti kama kuanzisha kizazi na Familia.
 
Ni kweli sana

Mtoto wa mama mkwe aliponikamata sawasawa niliswitch kutoka RC kwenda KKKT chap bila kuombwa, na niko vizuri kuzidi na yeye mwenyewe mzawa, hisia na imani vinaenda pamoja ni ngumu kumuombea mtu ambae hamko imani moja hamuongei lugha moja

Ila PM na mkewe wamewezaje kuishi hivyo mpaka kufikia level hiyo na bado kila mmoja akiwa na dini yake na jamaa hajaongeza mke mwingine wala
 
Ni kweli sana

Mtoto wa mama mkwe aliponikamata sawasawa niliswitch kutoka RC kwenda KKKT chap bila kuombwa, na niko vizuri kuzidi na yeye mwenyewe mzawa, hisia na imani vinaenda pamoja ni ngumu kumuombea mtu ambae hamko imani moja hamuongei lugha moja

Ila PM na mkewe wamewezaje kuishi hivyo mpaka kufikia level hiyo na bado kila mmoja akiwa na dini yake na jamaa hajaongeza mke mwingine wala
Nadhani mwanamke kaamua kujishusha utii by nature
 
Ni kweli sana

Mtoto wa mama mkwe aliponikamata sawasawa niliswitch kutoka RC kwenda KKKT chap bila kuombwa, na niko vizuri kuzidi na yeye mwenyewe mzawa, hisia na imani vinaenda pamoja ni ngumu kumuombea mtu ambae hamko imani moja hamuongei lugha moja

Ila PM na mkewe wamewezaje kuishi hivyo mpaka kufikia level hiyo na bado kila mmoja akiwa na dini yake na jamaa hajaongeza mke mwingine wala
Hapo hukubadili dini,ulibadili dhehebu.
 
Dini ni kifungo kilicho letwa kuja kutugawa waafrika hadi inakuwa ngumu mtu kubadili kifungo hichi.

Inashangaza sana mwafrika kwa mwafrika wanashindwa kuoana kwa sababu ya dini za kuletwa na wakoloni.

We tend to glorify our differences more than those aspects that unifies us.
Inashangaza sana
 
Ni kweli sana

Mtoto wa mama mkwe aliponikamata sawasawa niliswitch kutoka RC kwenda KKKT chap bila kuombwa, na niko vizuri kuzidi na yeye mwenyewe mzawa, hisia na imani vinaenda pamoja ni ngumu kumuombea mtu ambae hamko imani moja hamuongei lugha moja

Ila PM na mkewe wamewezaje kuishi hivyo mpaka kufikia level hiyo na bado kila mmoja akiwa na dini yake na jamaa hajaongeza mke mwingine wala

Iko hivyo.
Mwanamke akishika dini anaishika zaidi na kujitoa kuliko mwanaume. Hasa akiwa amehamia. Na akilea Watoto anakuwa Bora zaidi kuliko Baba kwenye mafunzo ya Dini.
Mwanamke akikupenda alafu akahama Imani yake Kwa hiyari yake hata siku moja huwezi mwambie Aende Kanisani au msikitini Ila yeye ndiye atakuwa namba moja.

Na MKE akianza ushirikina na Uchawi kazi Ipo. Yaani Kwa kifupi Mwanamke ni kiumbe mwenye uwezo wa kukuza kitu kidogo kiwe kikubwa.

Pia katika malezi ni rahisi kuwaweka Sawa Watoto kimaadili hasa pale wanapokengeuka.
 
Nadhani mwanamke kaamua kujishusha utii by nature

Mwanamke akikupenda atafanya chochote kwaajili yako.
Ila ukim- Disappoint upendo wake ukafa, nakuhakikishia utamuona shetani tuu.

UTI Kwa Mwanamke upo Kwa mwanaume anayempenda. Na automatically atakupenda Kwa jinsi ulivyo na Hali uliyonayo.
Hiyo unayosikia Wanawake wanapenda Pesa ni Uongo mkubwa.
Wanawake wanapenda Pesa pale wanapowapoteza wanaume waliowapenda Kwa mioyo Yao yote.

Kingine, Wanaume wengi tunatumia nguvu kubwa kulazimisha Mapenzi Kwa Wanawake Wakati wao hisia zao hazipo kwetu. Mwisho wa siku ndio kina kuja kutuumiza.

Mila na desturi za kiafrika ambazo nyingi zilikuwa za kijinga na zenye lengo la kumfanya Mwanamke mtumwa zimeathiri Kwa sehemu kubwa Akili za Wanawake.

Kina kisa cha kuolewa na Kaburi nilikiangalia TBC ONE Juzi. Nitakiandika hapa
 
Dini ni kifungo kilicho letwa kuja kutugawa waafrika hadi inakuwa ngumu mtu kubadili kifungo hichi.

Inashangaza sana mwafrika kwa mwafrika wanashindwa kuoana kwa sababu ya dini za kuletwa na wakoloni.

We tend to glorify our differences more than those aspects that unifies us.
Exactly mkuu umeusema ukweli ambao wengi wanaogopa, dini zetu za asili na mizimu yetu ndio msingi wa imani ,haya madini yaliyoletwa na merikebu ni uongo at its best, na pia mke ana mamlaka ya kuamua imani yake, tuachane na utamaduni wa utawala wa kidume,after all wengi wa akina mama wame prove wana uwezo wa kuishi, wanaume endeleeni kuwa sperm donors
 
MWANAMKE LAZIMA ABADILI DINI NA IMANI ILI IFANANE NA YAKO NDIPO UMUOE.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Moja ya ishara za awali Kwa Mwanamke anayekupenda na anayeweza kuwa Mkeo ni kukuamini, na kuamini Kwa kile ukifanyacho na kile unachokiamini. Kwa Mwanamke Hisia na Imani vinaenda sambamba. Mwanamke akishakuwa na hisia za upendo na wewe hapo moja Kwa moja atakuwa na Imani na wewe. Atakuamini. Kila unachomwambia Mwanamke anakiamini. Weka akilini hiyo.

Mwanamke akikupenda, atapenda unayoyapenda. Mtazamo wake utabadilika utakuwa Sawa na wako. Ndio maana ni rahisi kumbadilisha Mwanamke hata kama alikuwa ni kahaba lakini akishakupenda atauacha ukahaba wake. Ishu hapo ni hivi, Kwenye Moyo WA Mwanamke kuna Hisia na Imani. Wakati Sisi wanaume Imani Ipo kwenye Ubongo. Yaani hatuwezi kuamini Jambo bila kulitafakari Kutumia ubongo Akili.
Wakati Wanawake hawawezi kukuamini Jambo pasipo kuwa na hisia nalo, yaani kulipenda.

Sasa ili Mwanamke apende Jambo kuna michakato kadha wa kadha. Na yote lazima itimize imagination zake.

Ukiona umemtongoza Mwanamke mkaingia kwenye mahusiano alafu mpaka mnamaliza miezi sita hajataka Kubadili Imani na dini, jua huyo hujamkamata, yaani hujauteka moyo wake. Huyo hakufai. Hakuna mahali mtaenda.

Tena akikuambia wewe ndio umfuate ndio kabisa. Sisi Watibeli na wataalamu WA hayo mambo tunajua kuwa huyo Mwanamke Hakupendi, lakini pia atakupelekesha tuu.
Kingine ni lazima utashindwa kwenye ishu ya malezi. Yaani Watoto lazima wakushinde Kwa sababu tayari ulimshindwa Mama Yao.

Kubaniwa papuchi na kupewa chakula cha Usiku Kwa vipimo litakuwa ni Jambo la kawaida kwako na hautakuwa na chakufanya. Kiufupi utakuwa Dume-jike ambalo limeoa.

Asije akakudanganya MTU kuwa ndoa ya MKE na Mume WA Imani tofauti zinadumu au zinakuwa na Amani, hakuna kitu kama hicho.

Kingine cha muhimu zaidi ni kuwaz kamwe usimwambie Mwanamke abadili dini ili UMUOE. Hilo ni kosa la kiufundi. Mwanamke akishakupenda hatasubiri umwambie abadili Dini. Atabadili mwenyewe tuu Kwa mapenzi na uelewa wake kuhusu dini yako.

Kama hataki Kubadili dini yake Kwa hiyari jua huyo moyo wake haukupendi. Na kamwe hatakutii wala kukusikiliza Ila wewe ndiye utamtii na kumsikiliza. Atakupelekesha vile atakavyo.

Kesi nyingi za wanaowasiliana na Mimi nyingi zipo Kwa wanandoa ambao ni Aidha Mume alibadili dini na kufuata dini ya MKE. Au kila MTU alibaki na Dini yake wakafunga ndoa za bomani(serikalini).
Au mwanaume alitumia nguvu kumbadilisha Mwanamke Imani na Dini.

Elewa kuwa, kwenye mapenzi sio lazima uwe na MTU Fulani hasa kama hakupendi.
Elewa kuwa , mapenzi hayalazimishwi.
Elewa kuwa, kila mtu anauhuru wa Kutumia mwili wake. Hivyo usimpangie mkeo au mumeo matumizi ya mwili wake. Bali jipangie mwenyewe. Kama anakupenda basi ataji-commit kwako na sio wewe umlazimishe aji-commit kwako. Ila unaweza kujipangia kuwa huwezi ishi na Mwanamke au Mwanaume aliyeamua kuutumia mwili wake kufanya uasherati na uzinzi.
Hivyo katika mkataba wenu wa mahusiano ya ndoa, uwepo sheria iliyosainiwa au kukubaliana kuwa Kila MTU anauhuru wa Kutumia mwili wake atakavyo pasipo kuingiliwa na mwingine lakini Mimi(unaweza kuwa MKE au Mume) hutoweza kuishi na mtu mchafu (mzinzi na muasherati) hivyo Talaka itatoka ili kumpa MKE/mume Uhuru wa kuutumia mwili wake katika uchafu kadiri ya atakavyo.
Na hakutakuwa na Mijadala wala usuluhishi Kwa sababu ni Jambo lililojulikana mapema.

Hakutakuwa na hiyo nafasi ya kumshauri, kumfundisha mtu mzima aliyeko kwenye ndoa namna ya kuutumia mwili wake. Ila kila litakalofanyika litahesabika kama uamuzi wa Makusudi uliodhamiriwa na Mhusika.

Msamaha WA pekee utatolewa Baada ya Talaka kukabidhiwa. Kila MTU aishi Maisha yake lakini tukiwa tumesameheana. Hizo ni Kanuni za Watibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Ndoa zinahitaji maximum flexibility, with reservations. Ukiweka misingi isiyokuwa flexible, huwezi ishi na mke au Mume, maana kiuhalisia tunayajua haya maisha yetu.
 
Ndoa zinahitaji maximum flexibility, with reservations. Ukiweka misingi isiyokuwa flexible, huwezi ishi na mke au Mume, maana kiuhalisia tunayajua haya maisha yetu.
Ndoa zinahitaji maximum flexibility, with reservations. Ukiweka misingi isiyokuwa flexible, huwezi ishi na mke au Mume, maana kiuhalisia tunayajua haya maisha yetu.
Ni kweli.
Ila upendo na Imani hauhitaji Flexibility
 
Sijasoma ndani nimesoma heading ila kwenye heading yakaja maswali yafuatayo....

Hivi aliyesema maisha yana formula (yaani constant unayoweza kuhamisha kutoka kwa huyu kwenda kwa yule ni nani) yaani sababu y = mx + c; kwahio wewe / mtu yoyote ni kupachika hizo variables basi unapata jibu ambalo ni sawa kwa wote ?

Nadhani ukijua kwamba maisha sio black or white na kuna variables kibao; pia kinachofanyika kwako sio lazima kifanyike kwa mwingine utaona kwamba maisha ni simple sana wala hayahitaji complications (to each his / her own); Yaani Maisha yako ni wewe ndio unayajua zaidi kuliko third party yoyote....
 
Sijasoma ndani nimesoma heading ila kwenye heading yakaja maswali yafuatayo....

Hivi aliyesema maisha yana formula (yaani constant unayoweza kuhamisha kutoka kwa huyu kwenda kwa yule ni nani) yaani sababu y = mx + c; kwahio wewe / mtu yoyote ni kupachika hizo variables basi unapata jibu ambalo ni sawa kwa wote ?

Nadhani ukijua kwamba maisha sio black or white na kuna variables kibao; pia kinachofanyika kwako sio lazima kifanyike kwa mwingine utaona kwamba maisha ni simple sana wala hayahitaji complications (to each his / her own); Yaani Maisha yako ni wewe ndio unayajua zaidi kuliko third party yoyote....

Tunazungumzia Mapenzi na mahusiano ya Ndoa. Wewe unazungumzia MAISHA.
Ni vitu viwili tofauti.

Maisha ni neno la Jumla ambalo ndani yake kuna mambo mengi.
Alafu Mapenzi na ndoa ni neno mahususi.

Ni Sawa useme Matunda alafu useme Embe.

Maisha hayana Kanuni Kwa sababu ni neno la Jumla lakini vitu vilivyomo ndani ya Maisha ambavyo ni mahususi (specific) vina Kanuni na formula.

Siasa zina Kanuni zake,
Uchumi unakanuni zake
Dini zinakanuni zake
Akili na tabia ya Mwanadamu inakanuni zake.
Mapenzi na ndoa vinakanuni zake.

Maisha hayana Kanuni Kwa sababu yanahusu muunganiko wa specifications zote za yanayomzunguka Mwanadamu.
 
Back
Top Bottom