mgt software
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 13,793
- 7,165
umejenga? kama umejenga chukua chumba mojawapo umwekee house girl mwakikishie asijihusishe naye kabisa kama anafanya kazi hapo safi kama mkeo ana kazi hapo majanga mpeleke boding.
utawajua wanaotegeshea ndoa.
Anyway peleka mtoto boading, akifunga shule akae kwako week siku zilizobaki mpeleke kwa dada yako. Kwan wew hauna mama?
Mpeleke boarding school, likizo aje tu nyumbani kwako, hii inapunguza muda wa yeye kumlea..uskubali mwanao kukataliwa, hii pia itasababisha utengano na watotot wenzie ulonao.
Mtoto wangu wa kwanza ana miaka 8 nilimpata nikiwa mwaka 2 chuo ambapo kutokana na mamake kutokuwa mvumilivu kunisubiria nimalize kusoma aliamua kuolewa na kumuacha nyumbani kwao mtoto, nilipohitimu chuo na baada ya kupata kazi niliamua kumtafuta mwenza wa kuoa ambapo kabla ya yote nilimwambia ukweli kuwa nina mtoto na yeye akakubali atamlea lakini mara baada ya ndoa akanigeuka hataki kumuona mtoto huyo na kule anakokaa mtoto wanataka nimchukue.
Nimetumia kila njia imeshindikana msimamo wake ni hataki kumlea mtoto wa mwanamke mwingine, nifanyeje hapa wakuu maana nikilazimisha (uwezo huo ninao) anaweza kuwa anamtesa mtoto kipindi sipo akamsababishia matatizo ikitegemea huwa nasafiri mara kwa mara na sikai nyumbani sana na kuvunja ndoa siwezi maana ni ya kanisani na tayari tuna watoto
wengine wawili.
Ushauri wakuu
na akiwa likizo mtafutie tuition mda wa kukaa hom uwe mdogo sn.
Bibie utatumia kinywaji gani?Kama ulimwambia hata kabla ya ndoa na akaridhia, basi itakua alitafuta tu njia ya kukupata, lakini hana mapenzi ya dhati na wewe na ana roho mbaya, kumbuka mtoto ni damu yako na lazima uoneshe kuwa unaipenda damu yako tena kwa dhati na hauko tayari kuona mtoto wako ananyanyasika wakati baba yake yupo hai na una uwezo wa kulea, simama na umtete mwanao weka mikakati na uisimamie, zen mlete mtoto hapo home.
Ukiendekeza mapenzi unayopata kwa mkeo atakushawishi vibaya juu ya mwanao, mtetee mwanao, ajisikie ana baba la sivyo ataishi kwa manyanyaso. Mama yake tu hana time naye unadhani ataenda wapi akapate upendo kama sio kwako.
Nb; Na nyie wanaume pia acheni kuwakataa watoto waliozaliwa na wake zenu kabla ya kuwaoa, ukute hata huyo mama mtoto ana tamani kuishi na mwanae lakini mumewe huko amekataa.
Mpe option hii, mtoto aje nyumbani au yeye aondoke....achague moja hapo....then msikilizie atajibu nini...mwanaume lazima uwe na msimamo kaka.
Muambie mkeo unahama hapo ukatafute nyumba ukae na mwanao. Yeye mtakuwa mnatembeleana kama mtu na bf wake. gfsonwin, namaanisha hapo sio utani. Hivi wewe kama mtu kakukuta na mwanao na mnaoana anajua huyo ni mwanao. Then anakuambia simtaki huyu mtoto ungefanyaje? I would have done exactly that
Bibie utatumia kinywaji gani?