Mwanakijiji, huu ni UDINI pia...

Mwanakijiji, huu ni UDINI pia...

Status
Not open for further replies.
The Boss!
Naelewa unachomaanisha na kwa kweli jambo hili lazima lichukuliwe kwa sura ya taifa zaidi. Lakini pia nimemwelewa Mwanakijiji. Tofauti ya kifikra pengine inakuja kwa kuwa hukumsoma Mwanakijiji kwa kutafuta kumwelewa pengine ulisoma ukitaka umjibu ndipo mgongano unapotokea ingawa nyote mna lengo moja la kutaka kujenga Tanzania iliyo moja bila kujali tofauti zetu za kiimani.

Jambo ni moja, Pengo au jumuia ya kikristo ni lazima watoe kauli. Ni kauli ambayo inaweza kutupatia dira mpya ya maisha ya uvumilivu na kuheshimu imani za watu wengine (hususani kwa waumini wao). Kubwa ni kwamba kauli ya pengo/jumuia ya kikristo haiwezi ke-replace kauli ama kazi ya serikali. By the way kauli sio lazima iwe kauli hasi, yaweza kuwa kauli chanya ya kuwaomba waumini wao wasiwe controlled na jazba za kutaka kulipiza kisasi!

Kwa hiyo kauli za viongozi wa kidini ni muhimu sana katika migogoro iliyojijenga katika tofauti za kidini. Hakuna namna ya Pengo ama viongozi wengine kukwepa kulizungumzia jambo kama hili.

Mungu Ibariki Tanzania!
 
Watuw engi wanafikiri -kwa kusoma vibaya theolojia - Yesu alikuwa anapenda watu wadhulumiwe au wafanywe duni. Mgongano wake na watawala wa zama zake (viongozi wa serikali na wale wa kidini) ulitokana na yeye kutovumilia dhulma. Au ukandamizaji. Jinsi ambavyo aliwtetea maskini (mama mjane) na hata matajiri (Zakayo) kulitokana na yeye kutambua kuwa wote ni wana wa Mungu.

Lakini kuna vitu ambavyo hakuweza kuvivumilia kwa kuitisha vikao, kutoa matamko ya kubembeleza. Mojawapo ni ni lile la kuingia Hekaluni. Alipokuta watu wamegeuza hekalu kuwa soko hakuitisha kikao, wala kuhubiri.. alifanya hivyo huku akiwatimua watu hekaluni na hivyo kuwaudhi watawala na kuchochea hasira dhidi yake.

Askofu Mkuu Pengo NI LAZIMA atoe kauli iliyo wazi dhidi ya utawala wa CCM na jinsi walivyofikisha taifa hapa. Haya ya kuremburiana na watawala na kujifunika kitanda kimoja nao ndio yamelifikisha taifa hapa.
 
Wao ni binaadamu
wanaweza kuwa 'carried out' na emotions na hasira na uchungu
mwisho wakasema 'kuweni na tahadhari na waislam wote'
we unaonaje hapo?
fair?

Mkuu unataka kusema kuwa hao Polisi unaowalilia kuwa wao Sio Binaadam na hawana Dini na hawawezi kuwa Carried out na Emotions
 
Watuw engi wanafikiri -kwa kusoma vibaya theolojia - Yesu alikuwa anapenda watu wadhulumiwe au wafanywe duni. Mgongano wake na watawala wa zama zake (viongozi wa serikali na wale wa kidini) ulitokana na yeye kutovumilia dhulma. Au ukandamizaji. Jinsi ambavyo aliwtetea maskini (mama mjane) na hata matajiri (Zakayo) kulitokana na yeye kutambua kuwa wote ni wana wa Mungu.Lakini kuna vitu ambavyo hakuweza kuvivumilia kwa kuitisha vikao, kutoa matamko ya kubembeleza. Mojawapo ni ni lile la kuingia Hekaluni. Alipokuta watu wamegeuza hekalu kuwa soko hakuitisha kikao, wala kuhubiri.. alifanya hivyo huku akiwatimua watu hekaluni na hivyo kuwaudhi watawala na kuchochea hasira dhidi yake. Askofu Mkuu Pengo NI LAZIMA atoe kauli iliyo wazi dhidi ya utawala wa CCM na jinsi walivyofikisha taifa hapa. Haya ya kuremburiana na watawala na kujifunika kitanda kimoja nao ndio yamelifikisha taifa hapa.
Ndoo maanake!!
 
Pengo anastahili kutoa kauli nzito kwa serikali AU kujiuzulu. kwa sababu: Haya matukio yametokea mengi lakini hakuna mtuhumiwa aliyekamatwa Waislam hawataki amani iliyopo wanataka ipotee hivyo watakayoyafanya ni makubwa zaidi
 
Inachosha kwakweli mambo ambavyo yamekuwa yakiachwa. Mungu wa Israel aliyewashindia vita ndiye tunayemuabudu; ninaamini atalishindia kwa njia yoyote anayotaka (hayuko limited) kanisa lake linalodhulumiwa. Ninaamini atanena kwa njia za watumishi wake (Pengo akiwemo) na kutupa directives za jinsi ya kushinda dhulma (vita) hii kama alivyomuinua Daudi mbele ya Goliath!
 
The Boss,

Sheikh Ilunga anatoa mafundisho ya kulipa visasi kwa kuua makafir, askofu na mapadre, in the name of Islam. CD zinasambazwa nchi nzima, in the name of Islam. A padre was shot, he naturally becomes a suspect and so does Islam.

Hakuna taasisi iliyo-denounce mafundisho yake na sijaona wewe ukipinga kile anachofundisha zaidi ya kufumbia macho. Hivyo, indirectly, kuhalalisha anachofundisha. Je, huo ni Uislam? If not, mbona hamsemi lolote juu ya mafundisho yake ya "kiislam"?
 
Huo sio udini, na sio hatari ndio maana The Boss hajauongelea. Ila maoni ya Mwanakijiji ni UDINI na ni hatari sana!
The Boss,

Sheikh Ilunga anatoa mafundisho ya kulipa visasi kwa kuua makafir, askofu na mapadre, in the name of Islam. CD zinasambazwa nchi nzima, in the name of Islam. A padre was shot, he naturally becomes a suspect and so does Islam.

Hakuna taasisi iliyo-denounce mafundisho yake na sijaona wewe ukipinga kile anachofundisha zaidi ya kufumbia macho. Hivyo, indirectly, kuhalalisha anachofundisha. Je, huo ni Uislam? If not, mbona hamsemi lolote juu ya mafundisho yake ya "kiislam"?
 
Last edited by a moderator:
Wana JF nilikuwa sujawahi kumsikia wala simjui huyu Sheikh! Niko Rwanda kikazi Lakini nimebaki Mdomo wazi kusikia vitu Kama hivi. Hivi kweli huyu ni mtanzania? Sidhani na wala siamini kuwa huyu ni mtanzania! Nina marafiki wengi sana waislaam bara na huko Zanzibar ambako Nina rafiki ambaye ni ndugu kwa jinsi tunavyothaminiana na kuheshimiana including ndugu na wazazi wetu. Haya siyo maneno ya uchochezi ya kiongozi wa dini ila ni uhalifu ambao hauhitaji kupewa hata sekunde! Ni lazima akamatwe mara moja na kushitakiwa. Huyu si mtanzania, kwa hili naapa kabisa kuwa si mtanzania maana sioni ule moyo wa kitanzania hata chembe tu!

Ni mtanganyika c mtanzania.
 
Hizo ndiyo fikra za Mwakijiji zipo wazi katika jamii ya Kiislam.
 
TWO wrongs do not make it right...

wakuwa held responsible ni serikali.....na sio kila mtu akimbilie kwa viongozi wa dini yake
unapinga nini,na unafanya nini?

The Boss huoni huu ni wakati muafaka wa wanaodaiwa kuwa wachochezi kutoka dini ya Kiislam kama Ilunga, kupiga kelele na kulaani tendo hili lililofanywa huko Zanzibar? Maana wachochezi wote utawasikia wakisema Allah Akbar. Nenda Mzalendo.net uone comments zao.
 
Last edited by a moderator:
Ni mtihani mkubwa sana haya mambo yanatokea... Ni mtihani kwa Waislamu na Wakristo pia. I can understand Mwanakijiji ingawa sikubaliani naye; najaribu kufikiria katika nafasi yake ningekuwa na msimamo na mawazo gani... Najikuta siwezi pata jibu sababu circumstances zake na zangu ni tofauti... Na hali pia circumstances za tukio na matukio ni lazima yapeleke wengi huko na kuwafanya wawe wenye hasira, hasa kwa Imani ya Wakristo.

Boss I support you na uliyosema... I can understand the frustration for I am so frustrated right now na sielewi ni nani nimwelekezee. Sad.

Huu mtihani mkubwa ila naamini wahuni wamevamia jambo wanalotaka kwa kivuli cha udini.
 
Hizo ndiyo fikra za Mwakijiji zipo wazi katika jamii ya Kiislam.

Naamini kabisa wanaofanya fujo ni wahuni wanaojificha kwenye shuka la udini...tusikimbilie jumla jumla kusema haya mambo yanayoendelea ni mambo yanayoungwa mkono moja kwa moja na dini fulani.Ila viongozi wa dini wasimung'unye maneno kuhusu tabia mbaya zinazoendelea...
 
Kaka yangu ni Mmissionari; alivyoenda kwa mara ya kwanza Afrika kaskazini ambapo 98% ni waislamu nilikosa amani kabisa ni miaka zaidi ya 10 yuko huko na sasa ninaamini yuko salama kuliko angekuwa wa jimbo na kupelekwa Zanzibar kwa utumishi wake.

Mungu aipumzishe Roho ya Fr. Mushi karibu na kiti cha enzi kwani ni Mfia dini maana pamoja na kujua hatari ya kuhudumia Zanzibar bado aliendelea na utume wake!
 
Hapo (kwenye red) ni sahihi, lakini kuna namna ya uteteaji ambayo inahatarisha amani. Kuna wakati vurugu zilitokea Dar, makanisa yakachomwa moto na mali kwibwa, viongozi wa dini wahanga wakatoa tamko kuwa waumini wao wawe wavumilivu na wawe wenye kusamehe. Lakini kwa tukio lililotokea nchi jirani, 'viongozi' wa dini nyingine hapa nchini wametoa tamko kuwa waumini wa nchi hii washike bunduki na silaha nyinginezo waue viongozi wa dini yoyote (isiyo yao) hata kama haijulikani mauaji yamefanywa na nani. Huu ndio utaifa unaotaka kuona ambapo mmoja ana haki ya kusema na kufanya chochote cha kumkandamiza mwenzake? Hii amani tunayoichezea kuna siku tutaijutia. Na sina uhakika wote tunaohamasishwa kuchinja (watu, si ng'ombe wala mbuzi) kama tunaelewa madhara ya uchinjaji huo.

Ningependa kuona Tanzania yenye amani na heshima bila kujali dini, kabila wala rangi ya mtu. matumaini ya kuiona Tanzania ya namna hiyo siku za usoni yameanza kupungua kwa kasi!
Mungu na atusaidie kuondokana na upofu uliotupata, tuone mbele, japo mita moja tu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom