Mwanakijiji, huu ni UDINI pia...

Mwanakijiji, huu ni UDINI pia...

Status
Not open for further replies.
Mkuu umegusa nilipokuwa napataka haya mauaji ni ya kuangalia kwa jicho mawili.Hivi na Shehe akiuwawa mawazo yetu tutayapeleka wapi?
 
Mkuu The boss viongozi wanasema tutawachukulia hatua, kwenye thread yangu nmesema watawala wawajibike, tuna hitaji kupewa taarifa ya kinachoendelea na kama taifa tunahitaji kuona mtu anawajibishwa kwa uzembe huu

Ni bora kuitisha maandamano ya waislam na wakristo pamoja kulaani haya
kuliko mtu kukimbilia kwa kiongozi wa dini yake
 
Mjj yupo marekani hana shida tukichinjana,yeye anaratibu akiwa mbali ya uwanja wa mapambano
 
Police case ni ngonjera za kupumbaza jamii.
Ina maana huoni yote yafanywayo na Police dhidi ya raia? Tumeyaona ya Iringa na tumeyaona ya Madaktari, bado unashauri watu waende police?
Acha kujaza watu hofu, Udini unazidi kukua na kushika kasi...umesahau kauli ya Wassira huko Mwanza?
Unakataza waumini wasiende kwa viongozi wao wa kidini kuomba miongozo, je ulitaka waende wapi? Kama ni serikali..unaiongelea serikali ipi? Tusikariri wajibu wa serikali bali tutambue uwezo wa serikali iliyopo.
If we are destined to vurugu, then let that one be...si kwa kushambulia walio kinyume na imani yetu, bali kwa kuwatafuta wahuni hawa wachache watumiao mwamvuli wa dini....na ni lazima viongozi watoe kauli mapema sana kuliko kusubiri hisia zigeuke kuwa imani na ukweli vichwani mwa wengi.
hapo kwenye red nafikiri ndilo jambo la muhimu na ndio na mimi ninapopingana na The Boss na wanaounga mkono hoja
 
Narudia tena hao waislamu wafanya ujinga wao huko huko ZNZ na kwa waoga Geita .. Wasithubutu kuingia A town itakula Kwao ... Nasema Hakuna rangi wataacha ona..​
 
Kwanza nani anauthibitisho kwamba haya mauaji yamefanyika kutokana na msukumo wa kidini? Au kwa vile kauwawa kiongozi wa dini?
 
Boss hudhani pia kutokaana na tension iliyopo sasa mtaani viongozi wakristo wakisimama na kutuomba tuwe wavumilivu kipindi hiki wakati serikali inafanya jitihada za kuwakamata waatuhumiwa?
 
Police case ni ngonjera za kupumbaza jamii.
Ina maana huoni yote yafanywayo na Police dhidi ya raia? Tumeyaona ya Iringa na tumeyaona ya Madaktari, bado unashauri watu waende police?
Acha kujaza watu hofu, Udini unazidi kukua na kushika kasi...umesahau kauli ya Wassira huko Mwanza?
Unakataza waumini wasiende kwa viongozi wao wa kidini kuomba miongozo, je ulitaka waende wapi? Kama ni serikali..unaiongelea serikali ipi? Tusikariri wajibu wa serikali bali tutambue uwezo wa serikali iliyopo.
If we are destined to vurugu, then let that one be...si kwa kushambulia walio kinyume na imani yetu, bali kwa kuwatafuta wahuni hawa wachache watumiao mwamvuli wa dini....na ni lazima viongozi watoe kauli mapema sana kuliko kusubiri hisia zigeuke kuwa imani na ukweli vichwani mwa wengi.

Sasa wewe ukiambiwa uchukue hatua utachukua hatua zipi?
waliomuua mwandishi wa habari ni waislam?
Wassira ni muislam?
Waliomteka Ulimboka ni Waislam?
Una hakika gani waliomuua Padri ni waislam?
Mbona Naibu Mufti alimwagiwa Tindikali Zanzibar na hakuna aliesema ni wakristo?

Ishu hapa ni kujiepusha na UDINI huku unapambana na UDINI.
Hata kama serikali ni zembe huwezi halalisha 'visasi na kuchukua hatua kienyeji'
huku hujui nani hasaa yuko nyuma ya vurugu....Kauli za viongozi wa dini zaweza chochea badala ya kupunguza

Idea ya kuwasikiliza na kuwaabudu viongozi wa dini ni Udini wa aina nyingine
 
Ni bora kuitisha maandamano ya waislam na wakristo pamoja kulaani haya
kuliko mtu kukimbilia kwa kiongozi wa dini yake

next time unapolenga kuleta na kujenga mahusiano au unapokuwa na lengo hasa la kuzuia Mass Hysteria, hizi ndiyo statement za kutoa...well balanced, but not as per thread posted.
 
Nashukuru kwa kuona UDINI wa MZEE MWANAKIJIJI na mimi nimemuonya kama ifuatavyo:

Huu ni uzushi na hatushangai kusikia haya baada ya CDM kuona ufinyu wa kushinda uchaguzi! sasa mnaanza kujaza wananchi uoga na kuanza kuchochea machafuko ambayo kiuhalisia haupo!

Waislamu na Wakristo wa nchi hii hawana mgogoro ila chuki na chokochoko zote hizi tunazoshuhudia zinapaliliwa na Wana siasa kwa faida zao binafsi!

Umeonyesha ubaguzi wazi kabisa kwa kuegemea upande mmoja tu wa kutetea mapdri wanaokamatwa na Serikali lakini humtaji hata Shehe mmoja anaesota rumande! huu sio uadilifu hata kidogo! mwaka 1993 Shehe Mkuu wa msikiti wa Mtoro Shekh Kassim bin Jumaa alikamatwa na Lyatonga Mrema na kuteswa vibaya sana na baadae kuachiwa akiwa hoi na baadae kufariki! hakuna kiongozi wa dini hata mmoja alielaani unyama huu!

Mwaka 1998 waislamu waliuwawa na Serikali ya Mkapa ktk Msikiti wa Mkwajuni nani alihoji au hata kudai uchunguzi ufanyike! alipouwawa mbwa ikaundwa tume ya kuchunguza mauaji ya mbwa kwa kuwa mmiliki alikuwa Mjerumani!

Mwaka 2001 Wafuasi wa CUF ambao wengi wao ni Waislamu waliuwawa na Serikali ya Mkapa huko Zanzibar kwa kuandamana na wengine kukimbia nchi! waliouwa walipandishwa vyeo na Kiongozi mkuu wa Kanisa kuu alitoa kauli ya kuwalaani marehemu kwa kusema walijitakia wenyewe!

Wa TZ kwa sasa tunatakiwa kutumia akili sana na hatuna budi kuanzisha tume ya maradhiano ili tuweze kuishi kwa amani na uadilifu! nchi yetu ni kubwa na inatutosha wote! leo tukiibomoa TZ tutakimbilia wapi? kila nchi inawaka moto!

Unafiki ni kiti kibaya sana! inatia uchungu!
 
Kwanza nani anauthibitisho kwamba haya mauaji yamefanyika kutokana na msukumo wa kidini? Au kwa vile kauwawa kiongozi wa dini?

Perseption kama hizi ndo zinafanya daily watu wanachinjwa...we try too hard kujifanya hatuoni tatizo
 
The Boss hizi 'busara' zako ndizo zimekuwa zikitumiwa na wakristu kwa miaka mingi sana naona 'busara' hizi ndizo zinazoendeleza matukio ya kichokonozi kama haya ya mauaji.
sijaelewa mantiki ya thread yako kwani umeshakiri uongozi wa kitaifa ni dhaifu halafu hapohapo unataka tuwaache washughulikie suala hili-WAMESHINDWA NA HAWATAWEZA!
 
Last edited by a moderator:
Wewe unaita 'ku tame' christians
wakati hata waislam wanapopigana,mfano kesi za viwanja za BAKWATA'
wenye busara husema haya haya....
watu wajiepushe na kukimbilia viongozi wao wa dini na kuwachukulia wote wasio wa dini zao ni maadui...
police case ibaki police case,wote tushirikiane 'wahalifu' washughulikiwe'

Mkuu, kama background ingekuwa sivyo ilivyo leo perspective yako ningeiunga mkono, lakini given the kind of background in the Isles we have today yes I agree first and foremost hii ni police case, lakini bado Pengo anahitajika kusema kitu.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hapa mi nafikiri interligensia inafanya kazi yake hii ni kazi ya serikali sasa
aliuwawa RPC je pandri nae hawezi kuwa na mahasimu wakamuua ila waliofanya hicho kitendo lazima wakamatwe.
Serikali inatakiwa itoe tamko kuhusu mauaji ya viongozi wa dini kwani italeta shida kama litaendelea kuwa igizo hii ni mara ya nne hivi tukio la kitu kizito kumuelekea padri baada ya ile ya peramiho na ya zenji na sasa imejirudia zenji na mtu kupoteza uhai usalama wa raia na mali zao uko wapi?
 
Boss hudhani pia kutokaana na tension iliyopo sasa mtaani viongozi wakristo wakisimama na kutuomba tuwe wavumilivu kipindi hiki wakati serikali inafanya jitihada za kuwakamata waatuhumiwa?


Hicho ndo Pengo alichokuwa anasema kila mara
sasa Mwanakijiji anataka ajiuzulu au atoe kauli nyingine kali
kwangu mimi huu ni UDINI wa waziwazi.....
Huhitaji kauli ya kiongozi wako wa dini,kama unajua nini maana ya utaifa
kwenye tatizo la kitaifa
 
The Boss hizi 'busara' zako ndizo zimekuwa zikitumiwa na wakristu kwa miaka mingi sana naona 'busara' hizi ndizo zinazoendeleza matukio ya kichokonozi kama haya ya mauaji.
sijaelewa mantiki ya thread yako kwani umeshakiri uongozi wa kitaifa ni dhaifu halafu hapohapo unataka tuwaache washughulikie suala hili-WAMESHINDWA NA HAWATAWEZA!


Mantiki iko hivi
kama viongozi wa serikali wameshindwa,hakuna njia nyingine?
hatuwezi wote waislam na wakristo tusiopenda vurugu tukashirikiana kutatua hili?
Mkristo akikimbilia kwa Pengo?na Muislam asiependa vurugu akimbilie wapi?
 
Mantiki iko hivi
kama viongozi wa serikali wameshindwa,hakuna njia nyingine?
hatuwezi wote waislam na wakristo tusiopenda vurugu tukashirikiana kutatua hili?
Mkristo akikimbilia kwa Pengo?na Muislam asiependa vurugu akimbilie wapi?
njia nyingine ipi hiyo?tuwe wakweli!
 
Hicho ndo Pengo alichokuwa anasema kila mara
sasa Mwanakijiji anataka ajiuzulu au atoe kauli nyingine kali
kwangu mimi huu ni UDINI wa waziwazi.....
Huhitaji kauli ya kiongozi wako wa dini,kama unajua nini maana ya utaifa
kwenye tatizo la kitaifa

ni heri pengo akatoka na kauli kali kuliko kuwaacha waamini walioko nyuma yake kujiamulia watakavyo!mimi naona hatari ni pale kiongozi huyu atakapokaa kimya kwani huku mtaani zitatembea messages za chuki na mwisho wa siku kutatokea 'vijana' ndani ya teksi na kuishia kumrushia risasi shekhe flani.
 
Uzi huu Replies: 20
Uzi ule Replies: 195

Nahamia airtel. Ntapata mawazo tofauti.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom