Mwanakijiji, huu ni UDINI pia...

Mwanakijiji, huu ni UDINI pia...

Status
Not open for further replies.
Way forward ni njia yeyote ile inclusive
ambayo waislam wengi na wakristo wengi wataiunga mkono
na sio kumuomba Pengo atoe muongozo...Pengo ni kiongozi wa wakatoliki
waislam wanaopinga UDINI huu na vurugu hizi utawatenga ukimleta Pengo kwenye picture
Bora Pengo ajilete mwenyewe na sio kuombwa na Influential Writer kama Mwanakijiji
NI HATARI MNO,na ni udini pia

hakuna njia ya namna hiyo kwenye suala la kiimani kama hili,imagine tulikaa kimya pale Dr ulimboka alivyotekwa seuse hili la kuuawa kwa ''kafiri''
 
Kwa hiyo kama thread zote hapa JF zinahusu hilo huo ndio uthibitisho kwamba waislamu wamehusika?

Sijasema uthibitisho
nimezungumzia hatari ya watu hasa wakristo kuona wako
kwenye hatari ya kuona kuna waislam wanawaandama
na Kwa Mwanakijiji kumuomba Pengo atoe muongozo ni kuzidisha tu hisia hizo
 
Infact kuna baadhi ya hoja uko sawa kama kuendelea kwa vitendo hivi bila serikali kuchukua hatua ni uzembe wa serikali,hoja ya mwanakiji ni kwamba wakati serikali imekaa kimya na baadhi ya viongozi wa muslim wanaendelea na uchochezi pengo yuko kimya hali ilipofikia zisipochukuliwa hatua za dharura watu watashinikiza viongozi wao deni watoe tamko ili kulipiza kisasi.

Kauli ya Mwanakijiji ni kuws Pengo atoe kauli strong au astaafu
 
wewe utakuwa mwislamu,uliyeanzisha huu uzi
 
Bwana the boss, hii thread yako ina kila harufu ya wivu ulionao dhidi ya heshima aliyojijengea mwenzio Mwanakijiji humu JF. It dwells on me that you would have jumped at any opportunity to swap positions with him!Badala ya kwenye preamble yako kutanguliza personal attack dhidi ya Mwanakijiji (Mwanakijiji hivi, Mwanakijiji vile), ungekwenda straight kwenye crux of the matter. Otherwise mimi nakuona nawe pia ni MDINI tu ambaye amekuwa offended na MDINI mwenziwe!!!
 
Hesabu za Kikristu hazikokotolewi kwa njia za kiislamu. Upanga urudishwe alani kwake. na viongozi wetu hawahitaji kukurupuka na matamko. Wanachukua hatuahili stahili kulingana na mazingira na ukubwa wa tatizo. Kwa mbinu na njia za Kikristu zenye kulenga kudumisha amani.
Sisemi viongozi wa dini wa Kikristo wakurupuke na kutangaza tuwaue waislam kama ambavyo wao wanawatangazia waumini wao wawaue wakristo, huo siyo ustaarabu wa wakristo! Naamini kama walivyofundisha na kulelewa vema katika Kristo kamwe hawawezi kufanya hivyo. Njia za amani ndiyo mtizamo wa wakristo mahali pote duniani, na katika ukrito kuua ni dhambi.

Lakini tunayo nafasi pia ya kuwashauri viongozi wetu kutoa tamko juu ya jambo hili. Tamko si lazima liwe la kutangaza kwamba wakrito wajibu mapigo, lakini tunaweza kuwa na tamko dhidi ya serikali hii iliyochoka.

Hebu wasikilize viongozi wao wanavyosema; halafu angalia serikali imechukua hatua gani?


Zamani tulikuwa tunaambiwa kila penye mkusanyiko wa watu pana usalama wa taifa. Kama kweli nchi ina usalama wa taifa, hawakuyaona haya? Najiuliza, hivi serikali haiyaoni haya? Kuna sababu yoyote ya kusema tuna serikali kweli? No, tutoe tamko kwanza la kuionya serikali, na baadaye hatua zaidi ambazo sitaki kuziandika hapa, maana tayari mods wameshaanza kunitumia message za vitisho, zifuate. Lakini ukweli ni kwamba serikali ya Kikwete imepoteza uhalali wa kuongoza nchi, wakristo tutambue hilo.
 
Last edited by a moderator:
Ni mtihani mkubwa sana haya mambo yanatokea... Ni mtihani kwa Waislamu na Wakristo pia. I can understand Mwanakijiji ingawa sikubaliani naye; najaribu kufikiria katika nafasi yake ningekuwa na msimamo na mawazo gani... Najikuta siwezi pata jibu sababu circumstances zake na zangu ni tofauti... Na hali pia circumstances za tukio na matukio ni lazima yapeleke wengi huko na kuwafanya wawe wenye hasira, hasa kwa Imani ya Wakristo.

Boss I support you na uliyosema... I can understand the frustration for I am so frustrated right now na sielewi ni nani nimwelekezee. Sad.

For an influential writer like him
ni hatari mno kuwa carried out na emotions na kuanza
kushawishi watu....
mashabiki wa Mwanakijiji wakiwa convinced na Mwanakijiji kuwa kauli ya Pengo
ina umuhimu mkubwa......kwenye Taifa hili
Ikitokea huyo Pengo kashawishi watu walipize kisasi je?
umeona ilivyo hatari?
 
Sio kwamba napinga kwamba kuna tatizo la udini,ila is vyema kulikuza namna hii,kwa nini naona kila mtu anakimbilia conclusion kwamba waislamu wanahusika na hayo mauaji? Jakaya aliishawahi kusema kuna viongozi wa dini wanashiriki biashara ya madawa ya kulevya,what if this could be a reason? Nachoomba mimi ni uthibitisho tu basi,lakini sijasema kwamba hayajasababishwa na msukumo wa kidini.

yani unataka tuendelee kupritendi kuwa hili jambo ni dogo!!
 
Mkuu AshaDii hapo kwenye rangi matatizo yote ndani ya nchi yetu ikiwemo udini unaozidi kuota mizizi wa kulaumiwa ni Kikwete and his administration. Miaka ya nyuma dini haikuwa issue kabisa miongoni mwa Watanzania maana walishirikiana katika kila raha na huzuni bila hata kubaguana kwa lolote lile.

Hata kualikana majumbani watu hawakuangalia udini kabisa na wengine walikuwa ni kama familia moja jinsi walivyojenga undugu wa karibu. wakristo wanawaalika waislamu nyumbani na kama kuna chakula ambacho kitahusisha kuku au Mbuzi basi kulikuwa hakuna hiana kwa wakristo kutafuta shehe ili achinje kuku/mbuzi yule ili tu marafiki zao wasije kuuliza maswali kama hayo huyu Mbuzi/Kuku kachinja nani? Na Waislamu nao walikuwa hawana hiana kuwaalika wakristo katika sherehe mbali mbali majumbani mwao na kulikuwa hakuna la kubaguana kuwaona hawa ni makafiri hawastahili kualikwa.

Miaka ya karibuni kumekuwa na kundi dogo katika dini zote mbili ambalo taratibu limeanzisha chuki za kutisha kuhusu dini zote mbili. Kutoa kashfa, kejeli na hata matusi mazito kwa waumini wa dini zote. Viongozi walikaa kimya kwa muda mrefu bila kuchukua hatua zozote ili kukomesha kabisa hali hiyo. Sasa hali imekithiri na watu kuanza kuviziana katika mauaji yanayofanywa kwa mhusika kwa kuwa tu yeye ni wa dini tofauti.

Nchi yetu imefikia mahali ambapo hali inatisha sana na kama hatua za haraka hazitachukuliwa kukomesha udini uliokithiri basi mauaji haya ya kidini yataongezeka sana nchini na wa kulaumiwa si mwingine bali Kikwete.


Ni mtihani mkubwa sana haya mambo yanatokea... Ni mtihani kwa Waislamu na Wakristo pia. I can understand Mwanakijiji ingawa sikubaliani naye; najaribu kufikiria katika nafasi yake ningekuwa na msimamo na mawazo gani... Najikuta siwezi pata jibu sababu circumstances zake na zangu ni tofauti... Na hali pia circumstances za tukio na matukio ni lazima yapeleke wengi huko na kuwafanya wawe wenye hasira, hasa kwa Imani ya Wakristo.

Boss I support you na uliyosema... I can understand the frustration for I am so frustrated right now na sielewi ni nani nimwelekezee. Sad.
 
Lukolo,

Sina haja ya kusikiliza hii misukule. Wewe si uchukue hizo CD upeleke polisi au maelezo. Itatosha. Askofu mpakwa mafuta hashindani na ustadhi ambaye hafikii hekima ya ministranti! Kwani Pengo alitoa tamko ili Ponda au Faridi akamatwe? Tunasubiri tamko watoe hao hao waliomuua padri. Mengine ni ya kaisari
 
Kuuwa Wachunngaji na Mapadri sio udini, but anayehoji ndo anaambiwa anachochea udini.- Damn.!
 
Mwanakijiji amejidhalilisha sana kwa uzi wake ule uliojaa chuki. Yeye yuko maelfu ya maili lakini anajiona anajua kila kitu kilichotokea Zanzibar just this morning!!!
Viongozi wa kanisa katoliki wanajua wanalolifanya, they have always done whats right. They will do what is right.
 
For an influential writer like him
ni hatari mno kuwa carried out na emotions na kuanza
kushawishi watu....
mashabiki wa Mwanakijiji wakiwa convinced na Mwanakijiji kuwa kauli ya Pengo
ina umuhimu mkubwa......kwenye Taifa hili
Ikitokea huyo Pengo kashawishi watu walipize kisasi je?
umeona ilivyo hatari?

Sijaona kosa la Pengo kutoa kauli na inapobidi yampasa iwe hivyo
Labda kumtaka ajiuzulu its too extreme lakini kamwe hatoacha kusemea hili na weww kwa nafasi yako na Wananchi wengine wenye mapenzi na Taifa hili watasemea kuhusiana na hili.
Kumbuka aliyeuwawa ni Padri wa Kanisa Katoliki na wala si tukio la kwanza. Kwahiyo hauwezi kuzuia kauli ya Kiongozi wa Kanisa kisa Udini. Jukumu la kutuunganisha ni la Viongozi wa Taifa lakini wanashindwa refer kwenye suala la uchinjaji.
 
Kuua mapadri na wachungaji sio udini but anayehoji mauaji hayo ndio anaonekana anachochea udini. Damn.!
 


Wana JF nilikuwa sujawahi kumsikia wala simjui huyu Sheikh! Niko Rwanda kikazi Lakini nimebaki Mdomo wazi kusikia vitu Kama hivi. Hivi kweli huyu ni mtanzania? Sidhani na wala siamini kuwa huyu ni mtanzania! Nina marafiki wengi sana waislaam bara na huko Zanzibar ambako Nina rafiki ambaye ni ndugu kwa jinsi tunavyothaminiana na kuheshimiana including ndugu na wazazi wetu. Haya siyo maneno ya uchochezi ya kiongozi wa dini ila ni uhalifu ambao hauhitaji kupewa hata sekunde! Ni lazima akamatwe mara moja na kushitakiwa. Huyu si mtanzania, kwa hili naapa kabisa kuwa si mtanzania maana sioni ule moyo wa kitanzania hata chembe tu!
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom