Mwanaharakati Albanie Marcossy atoweka kunusuru maisha yake

Dec 11, 2010
3,321
6,328
Mwanaharakati Marcosy Albanie ametoweka nyumbani kwake baada ya kufuatiliwa na watu wasio julikana kwa kipindi cha siku kadhaa.

Mtakumbuka mara ya mwisho Bwana huyu alionekana kwenye kipindi cha kipima joto kilicho rushwa kwenye runinga ya ITV kikimshirikisha yeye, mbunge wa Singida mashariki Mh Tundu Lissu pamoja na naibu spika Mh Job Ndugai.

Chanzo: Mabadiliko.

NB. Marcosy anajishughulisha na taasisi ya kiraia inayo fuatilia mwenendo wa shughuli za bunge pamoja na masuala mengine katika jamii.

attachment.php


Kutoka kwenye gazeti la Mwananchi ijumaa, Machi 15, 2013. Uk 8.

Akizungumza- jana kutoka alikokimbilia,- Marcossy alisema ameamua kuikimbia nyumba yake kwa ajili ya usalama na kubainisha kuwa taarifa ya vitisho vyake aliwasilisha kwa Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRD-Coalition,) Onesmo Olengurumwa.

Na Frederick Katulanda | Mwananchi | Ijumaa, Marchi 15 2013

Mwanaharakati Albanie Marcossy, Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Civil and Political Right Watch (CPW) ameondoka nyumbani kwake Kimara Dar es Slaam akidai kilichomwondoa ni kupokea vitisho kutoka kwa watu wasiojulikana.

Marcossy, awali aliwahi kufanya kazi kwenye Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC) ambako alikuwa mmoja wa waliopeleka mashtaka kwenye Mahakama ya Uhalifu wa Kimataifa (ICC), Septemba 28, 2012 dhidi ya serikali kutokana na mauaji yenye utata ya watu 23 akiwamo Mwandishi wa habari Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Daudi Mwangosi.

Akizungumza jana kutoka alikokimbilia, Marcossy alisema ameamua kuikimbia nyumba yake kwa ajili ya usalama na kubainisha kuwa taarifa ya vitisho vyake aliwasilisha kwa Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRD-Coalition,) Onesmo Olengurumwa.

Olengurumwa alithibitisha kupokea taarifa hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alipoulizwa jana alisema polisi hawana taarifa kuhusiana na kutoweka kwa mwanaharakati huyo wala kutishiwa kutokana na kutopokea taarifa yoyote kuhusiana na suala hilo


 
Nakubaliana na aliyesema Utawala wa KIkwete ni wakimafia ni kuuwa kila anayeukosoa kwa sasa namwamini kabisa na alichosema ,Kikwete mpaka aondoke atakuwa ameua wananchi wengi zaidi ya Risi yeyote aliyewahi kutawala hivi huwa najiuliza afanyavyo haya huwa anawashirikisha Jaji Othman,Mkuu wa Usalama Othman na msaidizi wake Jack Zoka,IGP-Saidi Mwema,Makamu wa Raisi Bilali,Kamishena wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es salaam -Selemani Kova akisaidiwa na Ahmed Msangi kama hawahusishi wanamshauri vipi hawa Raisi wetu
 
Mwache ajifiche namkaribisha hata Arusha kukimbia umafia ambao unafanywa na serikali. Serikali imeanza hunting ya wasema kweli na hiii ni dalili kwamba wamefeli ku deliver na hivyo kutaka kuwaondoa wanaowaangaza watu kuona ukweli. Kama amefanya kosa kwa nini wasimkamate waziwazi wakamfungulia mashtaka yanayoeleweka badala ya kufanya mambo kiu mafia
 
Akina Max wa JF wawe makini, kwani yawezekana kuwa wako kwenye pipeline!!

Mkuu. Naamini hawa manguli wanachukua hatua thabiti kuepusha macho na meno yao dhidi ya makoleo ya kina Joseph Mulundi.

Atakaye pona JF ni Invisible peke yake maana hawata muona au huenda wako naye lakini hawamuoni.
 
Last edited by a moderator:
View attachment 86844
Huyu hapa Mpiganaji na Bango lake wakati wa mgomo wa Madkatari na kabla ya Kuteswa kwa Dk. Ulimboka

Kwa bango kama hili kwanini hawa watu wasikutafute? Mimi naamini, ukweli utagundulika muda si mrefu. Na hakuna mahali popote na muda wowote katika historia ya dunia hii, tangu kuumbwa kwake, ambapo uongo ulifunika ukweli. Mara zote ukweli uwa unashinda.
 
Back
Top Bottom