Mwanafunzi wa mwaka wa nne kitivo cha sheria kwa jina la ALEX, amepigwa risasi tumbon na majambazi. Tukio hlo limetokea saa nane na nusu usiku, ktk ukumbi wa yombo 1 ambapo alikuwa na wenzake watatu wakijisomea kwa ajili ya mtihani wa kesho. Majambaz hayo yamepora laptop 3, simu na pesa. Ulinz hapa chuo ni mdogo sana,na kuna maaskari lakini hawakuwapo na walijifisha. Tukio hlo limesababisha wanafunz kuandamana usiku mzima, wakitaka kujua haki zao za kulindwa na hao mapolsi ambao wamekuwa hawawajibiki. Toka saa nane mlio wa risasi ulilia na waliusikia lakini hawakutokea na wakati wapo mita kama 200 kutokea sehemu ya tukio. Majeruh alifikishwa hospitali ya chuo na wanafunz wenyewe, sasa amepelekwa moi, na mungu atamsaidia. Baba professor mkandala tunaomba usikie kilio chetu na muimarishe ulinzi. Sijui kama mwanafunz huyo angekuwa foreina Udsm ingekuaje. TUMEWACHOKA MApolisi. Inasikitisha sana