Mwakyembe, Sitta 'walisafisha' nini Bandarini?

Mwakyembe, Sitta 'walisafisha' nini Bandarini?

ndio maana mwakyembe alivyoingia hao wote walikuwa wakikwepa kodi za bandari pia akawacalculatia wote na wakazilipa na ndio mwanzo wa shopping centre kuteteleka ila tra asingeweza kwenda maana ilikuwa ni wizara nyingine na ndio maana mfano airport wale wote waliokuwa wizara tofauti na yake alikuwa akiwarudisha wizara husika so asingeweza kuingia wizara ya fedha hiyo ilikuwa kwa bi mdada saada mkuya
 
Unaweza changia kwa kipande unachokubaliana nacho
Bade harudi tena....unaweza changia ili madudu haya yasijirudie

With great power (commissioner general-TRA) comes great responsibility. Bade hawezi kuachwa wakati makasha mengi kiasi hicho hayajalipishwa kodi. Na uzuri hajafukuzwa kazi, amewekwa pembeni ili ukweli upatikane. Kusimamishwa kwake ni kwa haki, ingawa namuonea huruma kama binadamu maana kwa nafasi yake wanasiasa wanamtumia kiasi cha kuharibu weledi wake. Ukwepaji mkubwa wa kodi kama huo hauwezi kukosa mkono wa wanasiasa.

Naungana nawe kuwa tunahitaji everlasting plans and strategies kwenye suala la kodi ili hata akija rais msela nchi isiathirike kimapato.Serikali ilichofanya so far ni cha muda mfupi na cha kujipatia umaarufu. Tunahitaji taasisi imara, sio viongozi imara. Ingawa pia taasisi imara hujengwa na viongozi imara. Tunahitaji mapinduzi ya kisera. Mfano badala ya TRA kujikadiria makusanyo, kinaweza kuundwa chombo kingine au kilichopo(mfano tume ya mipango) ili kitumike kuwakadiria makusanyo kwa mwezi,robo,nusu na mwaka mzima. Wabanwe kwa kutofikia malengo waliyopangiwa na malengo yawe ya juu kiasi kwamba hawatathubutu kupoteza mapato kizembe. Hiyo ni namna moja ya kisera na inayoweza kuzaa matunda kwa muda mrefu.
 
Wote wamekuwa mawaziri wa Uchukuzi kwa mda na wameshindwa kuzuia mianya ya Rushwa bandarini. Zaidi ya kuwaona wakiwa wamepiga picha na walarushwa Ndani ya ndege!!!!
 
With great power (commissioner general-TRA) comes great responsibility. Bade hawezi kuachwa wakati makasha mengi kiasi hicho hayajalipishwa kodi. Na uzuri hajafukuzwa kazi, amewekwa pembeni ili ukweli upatikane. Kusimamishwa kwake ni kwa haki, ingawa namuonea huruma kama binadamu maana kwa nafasi yake wanasiasa wanamtumia kiasi cha kuharibu weledi wake. Ukwepaji mkubwa wa kodi kama huo hauwezi kukosa mkono wa wanasiasa.

Naungana nawe kuwa tunahitaji everlasting plans and strategies kwenye suala la kodi ili hata akija rais msela nchi isiathirike kimapato.Serikali ilichofanya so far ni cha muda mfupi na cha kujipatia umaarufu. Tunahitaji taasisi imara, sio viongozi imara. Ingawa pia taasisi imara hujengwa na viongozi imara. Tunahitaji mapinduzi ya kisera. Mfano badala ya TRA kujikadiria makusanyo, kinaweza kuundwa chombo kingine au kilichopo(mfano tume ya mipango) ili kitumike kuwakadiria makusanyo kwa mwezi,robo,nusu na mwaka mzima. Wabanwe kwa kutofikia malengo waliyopangiwa na malengo yawe ya juu kiasi kwamba hawatathubutu kupoteza mapato kizembe. Hiyo ni namna moja ya kisera na inayoweza kuzaa matunda kwa muda mrefu.



Sijui umeona ile link inayosema Masamaki aliteuliwa na bodi
huku akiwa tayari na kshafa ingine ya kupoteza makontena?
na hiyo ni mwaka 2013 Bade akiwa naibu kamishna
vitu viwili naviona hapa
1.upotevu wa makontena sio kitu kipya
2.kamishna hana mamlaka ya kuteua watendaji na wala sijui kama ana mamlaka ya kufukuza
 
Kwa mtazamo mwingine ni kuwa TPA walifanya kazi yao, walifanya records za containers na wenye containers walilipa custom duties kama kawaida ndio maana records zipo wazi TPA...
Shida ipo huko TRA, ICT ya TPA na walinzi wa TPA Gate 5, kuna rushwa zilitembezwa hapo ili containers zipitishwe bila TRA kulipwa kodi stahiki, maana yake inawezekana wafanyakazi wa TRA walikuwa na records zilizotumwa na TPA, lakini wao kwa kupewa rushwa wakatoa release order bila kupokea malipo...
Mchezo ulichezwa na maafisa wa TRA, ICT ya TPA na walinzi...huwezi kuihusisha TPA moja kwa moja coz tayari management ilipokea containers, walitoza custom duties na kurelease docs TRA..ndivyo nilivyoelewa!

Hapo ndo uhusika wa TPA ulipo...ili kutumbua jipu lisijeerudi tena sharti uongozi wa TPA nao uchunguzwe.
 
Sijui umeona ile link inayosema Masamaki aliteuliwa na bodi
huku akiwa tayari na kshafa ingine ya kupoteza makontena?
na hiyo ni mwaka 2013 Bade akiwa naibu kamishna
vitu viwili naviona hapa
1.upotevu wa makontena sio kitu kipya
2.kamishna hana mamlaka ya kuteua watendaji na wala sijui kama ana mamlaka ya kufukuza

Sure, tatizo hilo lipo sehemu nyingi serikalini. Mfano: Katibu Mkuu, Naibu, Waziri, Waziri Mkuu wote wanateuliwa na rais-hawa wanatofautiana vyeo lakini hawawezi kuwajibishana. Wakati tukiombea mfumo huu ubadilike, mtu aliyepewa mamlaka ya juu ataendelea kuwajibishwa kwa makosa ya walio chini yake. Bade kwa nafasi yake alipaswa kujua na kuripoti mamlaka ya juu kuhusu utendaji wa Masamaki. Kama alifanya hivyo hana haja ya kuwa na wasiwasi. Tena kwa nafasi yake alipaswa kupendekeza marekebisho ya sera/kanuni za utumishi za TRA ili aweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Nami nikurudishe nyuma kidogo, mbona Mzee Mwinyi amewahi kujiuzulu wakati kosa alifanya Askari Magereza? Japo nafasi ya Bade si ya kisiasa, uzito wa suala lenyewe unahalalisha yeye kukaa pembeni ili mbivu na mbichi zijulikane.
 
mwakyembe ni vema sasa akaachana na siasa , hali yake mbele ya macho ya jamii hairidhishi kabisa , angeandika Erythrocyte hapa angeibuka TRUVADA au Mgirik kusakama , haya sasa watu wengine wameyaona madudu yake !

hahahaaa! Mkuu kwenye mambo ya serikali kuna kitu kinaitwa ''chain of command''

hiki kitu kinaumiza sana watendaji wadogo. Mwakyembe yupo vzr kiutendaji ila sasa tatzo lilikuwa juu. Sasa hivi juu kupo vzr subir chin kutakapowaka moto
 
Last edited by a moderator:
Bandari ilikuwa chini ya akina Sitta na Mwakyembe kwa muda mrefu kwa nyakati tofauti kiasi cha kushindwa kuwatenganisha watu hawa na ubadhilifu, wizi na ufisadi unaobainika sasa chini ya rais Dr. Magufuli.

Jamii itashindwa kuwaelewa Magufuli na Majaliwa kama baraza lao litawajumuisha Sita na Mwakyembe pia.
 
Leo bodi ya TPA na kaimu mkurugenzi pamoja na katibu mkuu uchukuzi wote wametimuliwa
kuna watu kwenye hii thread mlisema tatizo liko TRA tu na sio bandari
sijui mseme nini sasa
 
Hao walikuwa mawaziri wa uchukuzi sio wizara ya fedha.
Bandari kwenye sakata hili inaonyesha walifanya kazi yao. Sehemu iliyobaki ilikuwa TRA. Waziri mmoja hawezi kuingilia wizara nyingine ndiyo mgawanyo wa kazi.

Ndiyo ile orodha Majaliwa kaipata bandarini. Inaelekea watu wamefanya reconciliation, wakaona madudu sehemu ya TRA.

Hahaa hebu jisome tena
 
Mkuu The Boss Hii issue ya container 300+ Bandari wako safe inawezekana hata port charges zote zililipwa ndio maana yanaonekana kwenye system ya TPA.

Tatizo liko TRA Kwa kuwa hayako kwenye system yao na wala Ushuru haujalipwa. Sujui kama kuna mfanyakazo wa TPA kawajibishwa zaidi ya kuambiwa wa review walinzi wa Gate 5.

wako safe?
 
Nadhani upeo wako wa kufikiri ni mdogo. Mimi kwa mtanzamo wangu Mwakyembe alisaidia sana kusafisha Bandari na kila mtanzania analijua hilo. Kabla ya Mwakyembe kuingia Wizara ya uchukuzi hali ilikuweje bandarini na baada ya kuingia ikaweje, tuache unafiki wa kisiasa. Pia elewa kuwa makontena yaliyopotea yaliyoibuliwa na Majaliwa yapo chini ya TRA ambao ndio wanayasimamia. TRA ipo chini ya Wizara ya Fedha na siyo Wizara ya Uchukuzi, nenda shule.

Nani sasa aende shule?
bandari ilishsafishwa sio?
na leo bodi imebunjwa na mkurugenzi out ina maaana gani?
 
Hahaa hebu jisome tena

Nimeisoma tena na tena. Kwa facts ambazo zilikuwepo wakati huo, hayo maandishi yangu yanabaki kama yalivyo.

Sasa kuna facts mpya. Kuna vimemo vinasemwa japo wahusika hawajatajwa (probably wakubwa mno !). Nadahni lazima tuwe flexible na tuwe guided na facts zilizopo mezani.

Mtumbua majipu anaendelea. Kama kuna majipu ya Sitta na Mwakyembe, lazima yatumbuliwe!
 
Back
Top Bottom